< Amosi 9 >

1 Nilimwona Bwana akiwa amesimama kando ya madhabahu, naye akasema: “Piga vichwa vya nguzo ili vizingiti vitikisike. Viangushe juu ya vichwa vya watu wote; na wale watakaosalia nitawaua kwa upanga. Hakuna awaye yote atakayekimbia, hakuna atakayetoroka.
I siy the Lord stondynge on the auter, and he seide, Smyte thou the herre, and the ouer threshfoldis be mouyd togidere; for aueryce is in the heed of alle, and Y schal sle bi swerd the laste of hem; ther schal no fliyt be to hem, and he that schal fle of hem, schal not be sauyd.
2 Wajapojichimbia chini mpaka kwenye vina vya kuzimu, kutoka huko mkono wangu utawatoa. Wajapopanda juu hadi kwenye mbingu, kutoka huko nitawashusha. (Sheol h7585)
If thei schulen go doun til to helle, fro thennus myn hond schal lede out hem; and if thei schulen `stie til in to heuene, fro thennus Y schal drawe hem doun. (Sheol h7585)
3 Wajapojificha juu ya kilele cha Karmeli, huko nitawawinda na kuwakamata. Wajapojificha kutoka kwenye uso wangu katika vilindi vya bahari, huko nako nitaamuru joka kuwauma.
And if thei schulen be hid in the cop of Carmele, fro thennus Y sekynge schal do awei hem; and if thei schulen hide hem silf fro myn iyen in the depnesse of the see, there Y shal comaunde to a serpente, and it schal bite hem.
4 Wajapopelekwa uhamishoni na adui zao, huko nako nitaamuru upanga uwaue. Nitawakazia macho yangu kwa mabaya wala si kwa mazuri.”
And if thei schulen go awei in to caitifte bifore her enemyes, there Y schal comaunde to swerd, and it schal sle hem. And Y schal putte myn iyen on hem in to yuel, and not in to good.
5 Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, yeye agusaye dunia nayo ikayeyuka, na wote wakaao ndani mwake wakaomboleza: nayo nchi yote huinuka kama Naili, kisha hushuka kama mto wa Misri;
And the Lord God of oostis schal do these thingis, that touchith erthe, and it schal faile, and alle men dwellynge ther ynne schulen mourene; and it schal stie vp as ech stronde, and it schal flete awei as flood of Egipt.
6 yeye ambaye hujenga jumba lake la kifalme katika mbingu na kuisimika misingi yake juu ya dunia, yeye aitaye maji ya bahari na kuyamwaga juu ya uso wa nchi: Bwana ndilo jina lake.
He that bildith his stiyng vp in heuene, schal do these thingis, and foundide his birthun on erthe; which clepith watris of the see, and heldith out hem on the face of erthe; the Lord is name of hym.
7 “Je, Waisraeli, ninyi si sawa kwangu kama Wakushi?” asema Bwana. “Je, sikuleta Israeli kutoka Misri, Wafilisti kutoka Kaftori, na Washamu kutoka Kiri?
Whether not as sones of Ethiopiens ye ben to me, the sones of Israel? seith the Lord God. Whether Y made not Israel for to stie vp fro the lond of Egipt, and Palestines fro Capodosie, and Siriens fro Cirenen?
8 “Hakika macho ya Bwana Mwenyezi yako juu ya ufalme wenye dhambi. Nami nitauangamiza kutoka kwenye uso wa dunia: hata hivyo sitaiangamiza kabisa nyumba ya Yakobo,” asema Bwana.
Lo! the iyen of the Lord God ben on the rewme synnynge, and Y schal al to-breke it fro the face of erthe; netheles Y al to-brekynge schal not al to-breke the hous of Jacob, seith the Lord.
9 “Kwa kuwa nitatoa amri, na nitaipepeta nyumba ya Israeli miongoni mwa mataifa yote, kama vile nafaka ipepetwavyo katika ungo, na hakuna hata punje moja itakayoanguka chini.
For lo! Y schal comaunde, and schal schake the hous of Israel in alle folkis, as wheete is in a riddil, and a litil stoon schal not falle on erthe.
10 Watenda dhambi wote miongoni mwa watu wangu watauawa kwa upanga, wale wote wasemao, ‘Maafa hayatatupata wala kutukuta.’
Alle synneris of my puple schulen die bi swerd, whiche seien, Yuel schal not neiy, and schal not come on vs.
11 “Katika siku ile nitaisimamisha hema ya Daudi iliyoanguka. Nitakarabati mahali palipobomoka na kujenga upya magofu yake, na kuijenga kama ilivyokuwa awali,
In that dai Y schal reise the tabernacle of Dauith, that felle doun, and Y schal ayen bilde openyngis of wallis therof, and Y schal restore the thingis that fellen doun; and Y schal ayen bilde it,
12 ili wapate kuyamiliki mabaki ya Edomu, na mataifa yote yale yanayobeba Jina langu,” asema Bwana ambaye atafanya mambo haya.
as in olde daies, that thei welde the remenauntis of Idume, and alle naciouns; for that my name is clepun to help on hem, seith the Lord doynge these thingis.
13 “Siku zinakuja,” asema Bwana, “wakati mvunaji atatanguliwa na mkulima, naye mpanzi atatanguliwa na yeye akamuaye zabibu. Divai mpya itadondoka kutoka milimani, na kutiririka kutoka vilima vyote.
Lo! daies comen, seith the Lord, and the erere schal take the repere, and `the stampere of grape schal take the man sowynge seed; and mounteyns schulen droppe swetnesse, and alle smale hillis schulen be tilid.
14 Nitawarejesha tena watu wangu Israeli waliohamishwa; wataijenga tena miji iliyoachwa magofu, nao wataishi ndani mwake. Watapanda mizabibu na kunywa divai yake; watalima bustani na kula matunda yake.
And Y schal conuerte the caitifte of my puple Israel, and thei schulen bilde forsakun citees, and schulen dwelle; and schulen plaunte vyneyerdis, and thei schulen drynke wyn of hem; and schulen make gardyns, and schulen ete fruitis of hem.
15 Nitaipanda Israeli katika nchi yao wenyewe, hawatangʼolewa tena kutoka nchi ambayo nimewapa,” asema Bwana Mungu wenu.
And Y schal plaunte hem on her lond, and Y schal no more drawe out hem of her lond, which Y yaf to hem, seith the Lord thi God.

< Amosi 9 >