< Amosi 9 >

1 Nilimwona Bwana akiwa amesimama kando ya madhabahu, naye akasema: “Piga vichwa vya nguzo ili vizingiti vitikisike. Viangushe juu ya vichwa vya watu wote; na wale watakaosalia nitawaua kwa upanga. Hakuna awaye yote atakayekimbia, hakuna atakayetoroka.
I saw [the] Lord standing on the altar and he said strike the capital so they may shake the thresholds and break off them on [the] head of all of them and posterity their by the sword I will kill not he will flee of them [one who] flees and not he will escape of them an escapee.
2 Wajapojichimbia chini mpaka kwenye vina vya kuzimu, kutoka huko mkono wangu utawatoa. Wajapopanda juu hadi kwenye mbingu, kutoka huko nitawashusha. (Sheol h7585)
If they will dig in Sheol from there hand my it will take them and if they will go up the heavens from there I will bring down them. (Sheol h7585)
3 Wajapojificha juu ya kilele cha Karmeli, huko nitawawinda na kuwakamata. Wajapojificha kutoka kwenye uso wangu katika vilindi vya bahari, huko nako nitaamuru joka kuwauma.
And if they will hide themselves on [the] top of Carmel from there I will search for [them] and I will take them and if they will hide themselves from before eyes my at [the] bottom of the sea from there I will command the snake and it will bite them.
4 Wajapopelekwa uhamishoni na adui zao, huko nako nitaamuru upanga uwaue. Nitawakazia macho yangu kwa mabaya wala si kwa mazuri.”
And if they will go in captivity before enemies their from there I will command the sword and it will kill them and I will set eye my on them for evil and not for good.
5 Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, yeye agusaye dunia nayo ikayeyuka, na wote wakaao ndani mwake wakaomboleza: nayo nchi yote huinuka kama Naili, kisha hushuka kama mto wa Misri;
And [the] Lord Yahweh of hosts who touches the earth and it melted and they mourn all [the] inhabitants in it and it rises like the River all of it and it sinks like [the] River (of Egypt *L(abh)*)
6 yeye ambaye hujenga jumba lake la kifalme katika mbingu na kuisimika misingi yake juu ya dunia, yeye aitaye maji ya bahari na kuyamwaga juu ya uso wa nchi: Bwana ndilo jina lake.
who builds in the heavens (stairs his *Q(K)*) and vault his on [the] earth he has founds it who summons [the] waters of the sea and he poured out them on [the] surface of the earth [is] Yahweh name his.
7 “Je, Waisraeli, ninyi si sawa kwangu kama Wakushi?” asema Bwana. “Je, sikuleta Israeli kutoka Misri, Wafilisti kutoka Kaftori, na Washamu kutoka Kiri?
¿ Not like [the] sons of [the] Cushites [are] you to me O people of Israel [the] utterance of Yahweh ¿ not Israel did I bring up from [the] land of Egypt and [the] Philistines from Caphtor and Aram from Kir.
8 “Hakika macho ya Bwana Mwenyezi yako juu ya ufalme wenye dhambi. Nami nitauangamiza kutoka kwenye uso wa dunia: hata hivyo sitaiangamiza kabisa nyumba ya Yakobo,” asema Bwana.
Here! [the] eyes of - [the] Lord Yahweh [are] on the kingdom sinful and I will destroy it from on [the] surface of the ground nevertheless for not certainly I will destroy [the] house of Jacob [the] utterance of Yahweh.
9 “Kwa kuwa nitatoa amri, na nitaipepeta nyumba ya Israeli miongoni mwa mataifa yote, kama vile nafaka ipepetwavyo katika ungo, na hakuna hata punje moja itakayoanguka chini.
That here! I [am] about to command and I will shake among all the nations [the] house of Israel just as it is shaken in sieve and not it will fall a pebble [the] ground.
10 Watenda dhambi wote miongoni mwa watu wangu watauawa kwa upanga, wale wote wasemao, ‘Maafa hayatatupata wala kutukuta.’
By the sword they will die all [the] sinners of people my who say not it will bring near and it may meet through us the calamity.
11 “Katika siku ile nitaisimamisha hema ya Daudi iliyoanguka. Nitakarabati mahali palipobomoka na kujenga upya magofu yake, na kuijenga kama ilivyokuwa awali,
On the day that I will raise up [the] booth of David falling and I will wall up breaches their and ruins his I will raise up and I will rebuild it like [the] days of antiquity.
12 ili wapate kuyamiliki mabaki ya Edomu, na mataifa yote yale yanayobeba Jina langu,” asema Bwana ambaye atafanya mambo haya.
So that they may dispossess [the] remnant of Edom and all the nations which it is called name my on them [the] utterance of Yahweh [who is] about to do this.
13 “Siku zinakuja,” asema Bwana, “wakati mvunaji atatanguliwa na mkulima, naye mpanzi atatanguliwa na yeye akamuaye zabibu. Divai mpya itadondoka kutoka milimani, na kutiririka kutoka vilima vyote.
Here! days [are] coming [the] utterance of Yahweh and he will approach [the] plowman the reaper and [the] treader of grapes [the] sower of the seed and they will drip the mountains sweet wine and all the hills they will flow with [it].
14 Nitawarejesha tena watu wangu Israeli waliohamishwa; wataijenga tena miji iliyoachwa magofu, nao wataishi ndani mwake. Watapanda mizabibu na kunywa divai yake; watalima bustani na kula matunda yake.
And I will turn back [the] captivity of people my Israel and they will rebuild cities desolated and they will dwell [in them] and they will plant vineyards and they will drink wine their and they will make gardens and they will eat fruit their.
15 Nitaipanda Israeli katika nchi yao wenyewe, hawatangʼolewa tena kutoka nchi ambayo nimewapa,” asema Bwana Mungu wenu.
And I will plant them on own land their and not they will be plucked up again from on land their which I have given to them he says Yahweh God your.

< Amosi 9 >