< Amosi 8 >

1 Hili ndilo alilonionyesha Bwana Mwenyezi katika maono: kikapu cha matunda yaliyoiva.
خداوند یهوه به من چنین نمودار ساخت واینک سبدی پر از میوه‌ها.۱
2 Akaniuliza, “Amosi, unaona nini?” Nikajibu, “Kikapu chenye matunda yaliyoiva.” Ndipo Bwana akaniambia, “Wakati umewadia kwa watu wangu Israeli; sitawahurumia zaidi.”
و گفت: «ای عاموس چه می‌بینی؟» من جواب دادم که «سبدی از میوه.» و خداوند به من گفت: «انتها بر قوم من اسرائیل رسیده است و از ایشان دیگر درنخواهم گذشت.»۲
3 Bwana Mwenyezi asema, “Katika siku ile, nyimbo katika Hekalu zitageuka kuwa maombolezo. Miili mingi, mingi sana: itatupwa kila mahali! Kimya!”
خداوند یهوه می‌گوید که در آن روزسرودهای هیکل به ولوله مبدل خواهد شد ولاشهای بسیار خواهد بود و آنها را در هر جا به خاموشی بیرون خواهند انداخت.۳
4 Lisikieni hili, ninyi ambao mnawagandamiza wahitaji, na kuwaonea maskini wa nchi,
‌ای شما که می‌خواهید فقیران را ببلعید ومسکینان زمین را هلاک کنید این را بشنوید.۴
5 mkisema, “Ni lini Mwezi Mwandamo utakapopita ili tupate kuuza nafaka, na Sabato itakwisha lini ili tuweze kuuza ngano?” Mkipunguza vipimo, na kuongeza bei, na kudanganya kwa mizani zisizo sawa,
ومی گویید که غره ماه کی خواهد گذشت تا غله رابفروشیم و روز سبت تا انبارهای گندم را بگشاییم و ایفا را کوچک و مثقال را بزرگ ساخته، میزانهارا قلب و معوج نماییم.۵
6 mkiwanunua maskini kwa fedha, na wahitaji kwa jozi ya viatu, na mkiuza hata takataka za ngano pamoja na ngano.
و مسکینان را به نقره و فقیران را به نعلین بخریم و پس مانده گندم رابفروشیم.۶
7 Bwana ameapa kwake mwenyewe, aliye Kiburi cha Yakobo: “Kamwe sitasahau chochote ambacho wamefanya.
خداوند به جلال یعقوب قسم خورده است که هیچکدام از اعمال ایشان را هرگزفراموش نخواهم کرد.۷
8 “Je, nchi haitatetemeka kwa ajili ya hili, nao wote waishio ndani mwake hawataomboleza? Nchi yote itainuka kama Naili; itapanda na kushuka kama mto wa Misri.
آیا به این سبب زمین متزلزل نخواهد شد و همه ساکنانش ماتم نخواهند گرفت و تمامش مثل نهر برنخواهد آمدو مثل نیل مصر سیلان نخواهد کرد و فرو نخواهدنشست.۸
9 “Katika siku ile,” asema Bwana Mwenyezi, “Nitalifanya jua litue alasiri na kuifanya dunia iwe giza wakati wa mchana mwangavu.
و خداوند یهوه می‌گوید: «که در آن روزآفتاب را در وقت ظهر فرو خواهم برد و زمین رادر روز روشن تاریک خواهم نمود.۹
10 Nitageuza sikukuu zenu za kidini kuwa maombolezo, na kuimba kwenu kote kuwe kilio. Nitawafanya ninyi nyote mvae nguo ya gunia na kunyoa nywele zenu. Nitaufanya wakati ule uwe kama wa kuombolezea mwana wa pekee, na mwisho wake kama siku ya uchungu.
و عیدهای شما را به ماتم و همه سرودهای شما را به مرثیه هامبدل خواهم ساخت. و بر هر کمر پلاس و بر هرسر گری برخواهم آورد و آن را مثل ماتم پسریگانه و آخرش را مانند روز تلخی خواهم گردانید.»۱۰
11 “Siku zinakuja,” asema Bwana Mwenyezi, “wakati nitakapotuma njaa katika nchi yote: si njaa ya chakula wala kiu ya maji, lakini njaa ya kusikia maneno ya Bwana.
اینک خداوند یهوه می‌گوید: «ایامی می‌آید که گرسنگی بر زمین خواهم فرستاد نه گرسنگی از نان و نه تشنگی از آب بلکه از شنیدن کلام خداوند.۱۱
12 Wanaume watayumbayumba kutoka bahari hadi bahari na kutangatanga kutoka kaskazini mpaka mashariki, wakitafuta neno la Bwana, lakini hawatalipata.
و ایشان از دریا تا دریا و ازشمال تا مشرق پراکنده خواهند شد و گردش خواهند کرد تا کلام خداوند را بطلبند اما آن رانخواهند یافت.۱۲
13 “Katika siku ile “wasichana wazuri na vijana wanaume wenye nguvu watazimia kwa sababu ya kiu.
در آن روز دوشیزگان جمیل وجوانان از تشنگی ضعف خواهند کرد.۱۳
14 Wale waapao kwa aibu ya Samaria, au kusema, ‘Hakika kama miungu yenu iishivyo, ee Dani,’ au ‘Hakika kama mungu wa Beer-Sheba aishivyo’: wataanguka, wala hawatasimama tena.”
آنانی که به گناه سامره قسم خورده، می‌گویند که «ای دان به حیات خدای تو و به طریقت بئرشبع قسم می‌خوریم»، خواهند افتاد و بار دیگر نخواهندبرخاست.۱۴

< Amosi 8 >