< Amosi 8 >
1 Hili ndilo alilonionyesha Bwana Mwenyezi katika maono: kikapu cha matunda yaliyoiva.
Le Seigneur, l'Éternel, me fit voir ceci: voici, je vis une corbeille de fruits mûrs.
2 Akaniuliza, “Amosi, unaona nini?” Nikajibu, “Kikapu chenye matunda yaliyoiva.” Ndipo Bwana akaniambia, “Wakati umewadia kwa watu wangu Israeli; sitawahurumia zaidi.”
Et il dit: Que vois-tu Amos? Et je répondis: Un panier de fruits mûrs. Et l'Éternel me dit: La fin est venue pour mon peuple d'Israël; je ne continuerai plus à lui pardonner.
3 Bwana Mwenyezi asema, “Katika siku ile, nyimbo katika Hekalu zitageuka kuwa maombolezo. Miili mingi, mingi sana: itatupwa kila mahali! Kimya!”
En ce jour-là, les chants du palais seront des gémissements, dit le Seigneur, l'Éternel. En tout lieu il y aura beaucoup de cadavres, qu'on jettera en silence.
4 Lisikieni hili, ninyi ambao mnawagandamiza wahitaji, na kuwaonea maskini wa nchi,
Écoutez ceci, vous qui dévorez les pauvres et qui faites périr les misérables du pays;
5 mkisema, “Ni lini Mwezi Mwandamo utakapopita ili tupate kuuza nafaka, na Sabato itakwisha lini ili tuweze kuuza ngano?” Mkipunguza vipimo, na kuongeza bei, na kudanganya kwa mizani zisizo sawa,
Qui dites: Quand la nouvelle lune sera-t-elle passée, pour que nous vendions le blé? et le sabbat, pour que nous ouvrions les greniers, en diminuant l'épha, en augmentant le sicle, et en faussant la balance pour tromper.
6 mkiwanunua maskini kwa fedha, na wahitaji kwa jozi ya viatu, na mkiuza hata takataka za ngano pamoja na ngano.
Nous achèterons les misérables pour de l'argent, et le pauvre pour une paire de souliers; et nous vendrons la criblure du froment.
7 Bwana ameapa kwake mwenyewe, aliye Kiburi cha Yakobo: “Kamwe sitasahau chochote ambacho wamefanya.
L'Éternel l'a juré par la gloire de Jacob: Jamais je n'oublierai toutes leurs actions!
8 “Je, nchi haitatetemeka kwa ajili ya hili, nao wote waishio ndani mwake hawataomboleza? Nchi yote itainuka kama Naili; itapanda na kushuka kama mto wa Misri.
La terre, à cause d'elles, ne tremblera-t-elle pas? Et tous ses habitants n'en mèneront-ils pas deuil? Le pays tout entier montera comme le fleuve, il se soulèvera et s'affaissera comme le fleuve d'Égypte.
9 “Katika siku ile,” asema Bwana Mwenyezi, “Nitalifanya jua litue alasiri na kuifanya dunia iwe giza wakati wa mchana mwangavu.
Et il arrivera dans ce jour-là, dit le Seigneur, l'Éternel, que je ferai coucher le soleil à midi, et que j'obscurcirai la terre en plein jour.
10 Nitageuza sikukuu zenu za kidini kuwa maombolezo, na kuimba kwenu kote kuwe kilio. Nitawafanya ninyi nyote mvae nguo ya gunia na kunyoa nywele zenu. Nitaufanya wakati ule uwe kama wa kuombolezea mwana wa pekee, na mwisho wake kama siku ya uchungu.
Je changerai vos fêtes en deuil, et tous vos chants en complaintes; je mettrai le sac sur tous les reins, et je rendrai chauves toutes les têtes; et je mettrai le pays dans le deuil comme pour un fils unique, et sa fin sera comme un jour d'amertume.
11 “Siku zinakuja,” asema Bwana Mwenyezi, “wakati nitakapotuma njaa katika nchi yote: si njaa ya chakula wala kiu ya maji, lakini njaa ya kusikia maneno ya Bwana.
Voici, les jours viennent, dit le Seigneur, l'Éternel, où j'enverrai la famine dans le pays; non une famine de pain ni une soif d'eau, mais celle d'entendre les paroles de l'Éternel.
12 Wanaume watayumbayumba kutoka bahari hadi bahari na kutangatanga kutoka kaskazini mpaka mashariki, wakitafuta neno la Bwana, lakini hawatalipata.
Ils erreront d'une mer à l'autre, et du nord au levant; ils iront çà et là pour chercher la parole de l'Éternel, et ils ne la trouveront pas.
13 “Katika siku ile “wasichana wazuri na vijana wanaume wenye nguvu watazimia kwa sababu ya kiu.
En ce jour-là, les belles vierges et les jeunes hommes défailliront de soif;
14 Wale waapao kwa aibu ya Samaria, au kusema, ‘Hakika kama miungu yenu iishivyo, ee Dani,’ au ‘Hakika kama mungu wa Beer-Sheba aishivyo’: wataanguka, wala hawatasimama tena.”
Ceux qui jurent par le péché de Samarie, qui disent: Vive ton dieu, ô Dan! Et vive la voie de Béer-Shéba! Ils tomberont, et ne se relèveront plus.