< Amosi 8 >

1 Hili ndilo alilonionyesha Bwana Mwenyezi katika maono: kikapu cha matunda yaliyoiva.
Le Seigneur l'Eternel me fit voir cette vision, et voici, un panier de fruits d'Eté.
2 Akaniuliza, “Amosi, unaona nini?” Nikajibu, “Kikapu chenye matunda yaliyoiva.” Ndipo Bwana akaniambia, “Wakati umewadia kwa watu wangu Israeli; sitawahurumia zaidi.”
Et il dit: Que vois-tu, Amos? Et je répondis: Un panier de fruits d'Eté. Et l'Eternel me dit: La fin est venue sur mon peuple d'Israël, je ne lui en passerai plus.
3 Bwana Mwenyezi asema, “Katika siku ile, nyimbo katika Hekalu zitageuka kuwa maombolezo. Miili mingi, mingi sana: itatupwa kila mahali! Kimya!”
Les cantiques du Temple seront des hurlements en ce temps-là, dit le Seigneur l'Eternel. Il y aura grand nombre de corps morts que l'on jettera en tous lieux en silence.
4 Lisikieni hili, ninyi ambao mnawagandamiza wahitaji, na kuwaonea maskini wa nchi,
Ecoutez ceci vous qui engloutissez les pauvres, même jusqu'à désoler les affligés du pays;
5 mkisema, “Ni lini Mwezi Mwandamo utakapopita ili tupate kuuza nafaka, na Sabato itakwisha lini ili tuweze kuuza ngano?” Mkipunguza vipimo, na kuongeza bei, na kudanganya kwa mizani zisizo sawa,
Et qui dites: Quand sera passé ce mois? et nous débiterons le blé; et [quand sera passé] ce sabbat? et nous mettrons en vente le froment, en faisant l'épha plus petit, augmentant le sicle, et falsifiant les balances pour tromper.
6 mkiwanunua maskini kwa fedha, na wahitaji kwa jozi ya viatu, na mkiuza hata takataka za ngano pamoja na ngano.
Afin que nous acquérions les chétifs par argent, et le pauvre pour une paire de souliers, et que nous débitions les criblures du froment.
7 Bwana ameapa kwake mwenyewe, aliye Kiburi cha Yakobo: “Kamwe sitasahau chochote ambacho wamefanya.
L'Eternel a juré par la magnificence de Jacob: Si j'oublie jamais aucune de leurs actions!
8 “Je, nchi haitatetemeka kwa ajili ya hili, nao wote waishio ndani mwake hawataomboleza? Nchi yote itainuka kama Naili; itapanda na kushuka kama mto wa Misri.
La terre ne sera-t-elle point émue d'une telle chose, et tous ses habitants ne lamenteront-ils point? Ne s'écoulera-t-elle pas toute comme un fleuve, et ne sera-t-elle pas emportée et submergée comme par le fleuve d'Egypte?
9 “Katika siku ile,” asema Bwana Mwenyezi, “Nitalifanya jua litue alasiri na kuifanya dunia iwe giza wakati wa mchana mwangavu.
Et il arrivera en ce jour-là, dit le Seigneur l'Eternel, que je ferai coucher le soleil en plein Midi, et que je ferai venir les ténèbres sur la terre en un jour serein.
10 Nitageuza sikukuu zenu za kidini kuwa maombolezo, na kuimba kwenu kote kuwe kilio. Nitawafanya ninyi nyote mvae nguo ya gunia na kunyoa nywele zenu. Nitaufanya wakati ule uwe kama wa kuombolezea mwana wa pekee, na mwisho wake kama siku ya uchungu.
Je changerai vos fêtes solennelles en deuil, et tous vos cantiques en lamentation; je mettrai le sac sur tous les reins, et je rendrai chauves toutes les têtes; et je mettrai le [pays] en une telle lamentation, que celle d'un fils unique; et sa fin sera telle que d'un jour amer.
11 “Siku zinakuja,” asema Bwana Mwenyezi, “wakati nitakapotuma njaa katika nchi yote: si njaa ya chakula wala kiu ya maji, lakini njaa ya kusikia maneno ya Bwana.
Voici, les jours viennent, dit le Seigneur l'Eternel, que j'enverrai la famine sur le pays, non la famine du pain, ni la soif de l'eau, mais [la famine] d'ouïr les paroles de l'Eternel.
12 Wanaume watayumbayumba kutoka bahari hadi bahari na kutangatanga kutoka kaskazini mpaka mashariki, wakitafuta neno la Bwana, lakini hawatalipata.
Ils courront depuis une mer jusqu'à l'autre, et ils iront de tous côtés depuis l'Aquilon jusqu'à l'Orient, pour chercher la parole de l'Eternel; mais ils ne la trouveront point.
13 “Katika siku ile “wasichana wazuri na vijana wanaume wenye nguvu watazimia kwa sababu ya kiu.
En ce jour-là, pâmeront de soif les belles vierges et les jeunes hommes,
14 Wale waapao kwa aibu ya Samaria, au kusema, ‘Hakika kama miungu yenu iishivyo, ee Dani,’ au ‘Hakika kama mungu wa Beer-Sheba aishivyo’: wataanguka, wala hawatasimama tena.”
qui jurent par le délit de Samarie, et disent: ô Dan! Ton Dieu est vivant: et, vive la voie de Béersébah; ils tomberont donc, et ne se relèveront plus.

< Amosi 8 >