< Amosi 8 >

1 Hili ndilo alilonionyesha Bwana Mwenyezi katika maono: kikapu cha matunda yaliyoiva.
Ainsi me fit voir le Seigneur Yahweh, et voici une corbeille de fruits mûrs.
2 Akaniuliza, “Amosi, unaona nini?” Nikajibu, “Kikapu chenye matunda yaliyoiva.” Ndipo Bwana akaniambia, “Wakati umewadia kwa watu wangu Israeli; sitawahurumia zaidi.”
Et il dit: " Que vois-tu, Amos? " Je répondis: " Une corbeille de fruits mûrs. " Et Yahweh me dit: " La fin est venue pour mon peuple d'Israël; je ne lui pardonnerai pas plus longtemps.
3 Bwana Mwenyezi asema, “Katika siku ile, nyimbo katika Hekalu zitageuka kuwa maombolezo. Miili mingi, mingi sana: itatupwa kila mahali! Kimya!”
Les chants du palais seront des hurlements en ce jour-là, — oracle du Seigneur Yahweh. Il y aura de nombreux cadavres, en tout lieu on les jette en silence. "
4 Lisikieni hili, ninyi ambao mnawagandamiza wahitaji, na kuwaonea maskini wa nchi,
Écoutez ceci, vous qui engloutissez le pauvre, et qui voudriez faire disparaître les humbles du pays,
5 mkisema, “Ni lini Mwezi Mwandamo utakapopita ili tupate kuuza nafaka, na Sabato itakwisha lini ili tuweze kuuza ngano?” Mkipunguza vipimo, na kuongeza bei, na kudanganya kwa mizani zisizo sawa,
en disant: " Quand la nouvelle lune sera-t-elle passée, afin que nous puissions vendre du froment, et le sabbat, pour que nous ouvrions nos magasins à blé, en diminuant l'épha et en grossissant le sicle, en faussant la balance pour tromper?
6 mkiwanunua maskini kwa fedha, na wahitaji kwa jozi ya viatu, na mkiuza hata takataka za ngano pamoja na ngano.
Nous achèterons pour de l'argent les misérables, et les pauvres à cause d'une paire de sandales, et nous vendrons la criblure du froment? "
7 Bwana ameapa kwake mwenyewe, aliye Kiburi cha Yakobo: “Kamwe sitasahau chochote ambacho wamefanya.
Yahweh l'a juré par l'orgueil de Jacob: Je n'oublierai pas jusqu'à la fin toutes leurs actions.
8 “Je, nchi haitatetemeka kwa ajili ya hili, nao wote waishio ndani mwake hawataomboleza? Nchi yote itainuka kama Naili; itapanda na kushuka kama mto wa Misri.
A cause de cela, la terre ne tremblera-t-elle pas, et tous ses habitants ne seront-ils pas dans le deuil? Elle montera tout entière comme le Nil, elle se soulèvera et s'affaissera, comme le Nil d'Egypte.
9 “Katika siku ile,” asema Bwana Mwenyezi, “Nitalifanya jua litue alasiri na kuifanya dunia iwe giza wakati wa mchana mwangavu.
Il arrivera en ce jour-là, — oracle du Seigneur Yahweh, je ferai coucher le soleil en plein midi, et j'envelopperai la terre de ténèbres en un jour serein.
10 Nitageuza sikukuu zenu za kidini kuwa maombolezo, na kuimba kwenu kote kuwe kilio. Nitawafanya ninyi nyote mvae nguo ya gunia na kunyoa nywele zenu. Nitaufanya wakati ule uwe kama wa kuombolezea mwana wa pekee, na mwisho wake kama siku ya uchungu.
Je changerai vos fêtes en deuil, et tous vos chants de joie en lamentations; je mettrai le sac sur tous les reins, et je rendrai chauve toute tête; je mettrai le pays comme en un deuil de fils unique, et sa fin sera comme un jour amer.
11 “Siku zinakuja,” asema Bwana Mwenyezi, “wakati nitakapotuma njaa katika nchi yote: si njaa ya chakula wala kiu ya maji, lakini njaa ya kusikia maneno ya Bwana.
Voici que des jours viennent, — oracle du Seigneur Yahweh, et j'enverrai une faim sur la terre, non une faim de pain, et non une soif d'eau, mais d'entendre les paroles de Yahweh.
12 Wanaume watayumbayumba kutoka bahari hadi bahari na kutangatanga kutoka kaskazini mpaka mashariki, wakitafuta neno la Bwana, lakini hawatalipata.
Et ils erreront d'une mer à l'autre, et du septentrion à l'orient; ils iront de côté et d'autre pour chercher la parole de Yahweh, et ils ne la trouveront pas.
13 “Katika siku ile “wasichana wazuri na vijana wanaume wenye nguvu watazimia kwa sababu ya kiu.
En ces jours-là seront épuisés les belles vierges et les jeunes hommes, par la soif.
14 Wale waapao kwa aibu ya Samaria, au kusema, ‘Hakika kama miungu yenu iishivyo, ee Dani,’ au ‘Hakika kama mungu wa Beer-Sheba aishivyo’: wataanguka, wala hawatasimama tena.”
Ceux qui jurent par le péché de Samarie et disent: " Par la vie de ton Dieu, ô Dan! Par la voie de Bersabée! " tomberont et ne se relèveront pas.

< Amosi 8 >