< Amosi 8 >

1 Hili ndilo alilonionyesha Bwana Mwenyezi katika maono: kikapu cha matunda yaliyoiva.
The Lord God schewide to me these thingis; and lo! an hook of applis.
2 Akaniuliza, “Amosi, unaona nini?” Nikajibu, “Kikapu chenye matunda yaliyoiva.” Ndipo Bwana akaniambia, “Wakati umewadia kwa watu wangu Israeli; sitawahurumia zaidi.”
And the Lord seide, What seist thou, Amos? And Y seide, An hook of applis. And the Lord seide to me, The ende is comun on my puple Israel; Y schal no more putte to, that Y passe bi hym.
3 Bwana Mwenyezi asema, “Katika siku ile, nyimbo katika Hekalu zitageuka kuwa maombolezo. Miili mingi, mingi sana: itatupwa kila mahali! Kimya!”
And the herris, ether twistis, of the temple schulen greetli sowne in that dai, seith the Lord God. Many men schulen die, silence schal be cast forth in ech place.
4 Lisikieni hili, ninyi ambao mnawagandamiza wahitaji, na kuwaonea maskini wa nchi,
Here ye this thing, whiche al to-breken a pore man, and maken nedi men of the lond for to faile;
5 mkisema, “Ni lini Mwezi Mwandamo utakapopita ili tupate kuuza nafaka, na Sabato itakwisha lini ili tuweze kuuza ngano?” Mkipunguza vipimo, na kuongeza bei, na kudanganya kwa mizani zisizo sawa,
and ye seien, Whanne schal heruest passe, and we schulen sille marchaundises? and the sabat, and we schulen opene wheete? that we make lesse the mesure, and encreesse the cicle, and `vndur put gileful balauncis;
6 mkiwanunua maskini kwa fedha, na wahitaji kwa jozi ya viatu, na mkiuza hata takataka za ngano pamoja na ngano.
that we welde bi siluer nedi men and pore men for schoon, and we sille outcastyngis of wheete?
7 Bwana ameapa kwake mwenyewe, aliye Kiburi cha Yakobo: “Kamwe sitasahau chochote ambacho wamefanya.
The Lord swoor ayens the pride of Jacob, Y schal not foryete til to the ende alle the werkis of hem.
8 “Je, nchi haitatetemeka kwa ajili ya hili, nao wote waishio ndani mwake hawataomboleza? Nchi yote itainuka kama Naili; itapanda na kushuka kama mto wa Misri.
Whether on this thing the erthe schal not be mouyd togidere, and eche dwellere therof schal mourene? And it schal stie vp as al the flood, and schal be cast out, and schal flete awei as the stronde of Egipt.
9 “Katika siku ile,” asema Bwana Mwenyezi, “Nitalifanya jua litue alasiri na kuifanya dunia iwe giza wakati wa mchana mwangavu.
And it schal be, seith the Lord, in that dai the sunne schal go doun in myddai, and Y schal make the erthe for to be derk in the dai of liyt.
10 Nitageuza sikukuu zenu za kidini kuwa maombolezo, na kuimba kwenu kote kuwe kilio. Nitawafanya ninyi nyote mvae nguo ya gunia na kunyoa nywele zenu. Nitaufanya wakati ule uwe kama wa kuombolezea mwana wa pekee, na mwisho wake kama siku ya uchungu.
And Y schal conuerte youre feeste daies in to mourenyng, and alle youre songis in to weilyng; and Y schal brynge yn on ech bac of you a sak, and on ech heed of you ballidnesse; and Y schal put it as the mourenyng of oon bigetun sone, and the laste thingis therof as a bittir dai.
11 “Siku zinakuja,” asema Bwana Mwenyezi, “wakati nitakapotuma njaa katika nchi yote: si njaa ya chakula wala kiu ya maji, lakini njaa ya kusikia maneno ya Bwana.
Lo! the daies comen, seith the Lord, and Y schal sende out hungur in to erthe; not hungur of breed, nether thirst of watir, but of herynge the word of God.
12 Wanaume watayumbayumba kutoka bahari hadi bahari na kutangatanga kutoka kaskazini mpaka mashariki, wakitafuta neno la Bwana, lakini hawatalipata.
And thei schulen be mouyd to gidere fro the see til to the see, and fro the north til to the eest thei schulen cumpasse, sekynge the word of the Lord, and thei schulen not fynde.
13 “Katika siku ile “wasichana wazuri na vijana wanaume wenye nguvu watazimia kwa sababu ya kiu.
In that dai faire maidens schulen faile, and yonge men in thirst, whiche sweren in trespas of Samarie,
14 Wale waapao kwa aibu ya Samaria, au kusema, ‘Hakika kama miungu yenu iishivyo, ee Dani,’ au ‘Hakika kama mungu wa Beer-Sheba aishivyo’: wataanguka, wala hawatasimama tena.”
and seien, Dan, thi god lyueth, and the weie of Bersabee lyueth; and thei schulen falle, and thei schulen no more rise ayen.

< Amosi 8 >