< Amosi 8 >
1 Hili ndilo alilonionyesha Bwana Mwenyezi katika maono: kikapu cha matunda yaliyoiva.
Thus he showed me [the] Lord Yahweh and there! a basket of summer fruit.
2 Akaniuliza, “Amosi, unaona nini?” Nikajibu, “Kikapu chenye matunda yaliyoiva.” Ndipo Bwana akaniambia, “Wakati umewadia kwa watu wangu Israeli; sitawahurumia zaidi.”
And he said what? [are] you seeing O Amos and I said a basket of summer fruit and he said Yahweh to me it has come the end to people my Israel not I will repeat again to pass by it.
3 Bwana Mwenyezi asema, “Katika siku ile, nyimbo katika Hekalu zitageuka kuwa maombolezo. Miili mingi, mingi sana: itatupwa kila mahali! Kimya!”
And they will wail songs of [the] temple on the day that [the] utterance of [the] Lord Yahweh many the corpse[s] in every place someone will throw hush!
4 Lisikieni hili, ninyi ambao mnawagandamiza wahitaji, na kuwaonea maskini wa nchi,
Hear this O those [who] trample on [the] needy and to put an end to ([the] afflicted [people] of *Q(K)*) [the] land.
5 mkisema, “Ni lini Mwezi Mwandamo utakapopita ili tupate kuuza nafaka, na Sabato itakwisha lini ili tuweze kuuza ngano?” Mkipunguza vipimo, na kuongeza bei, na kudanganya kwa mizani zisizo sawa,
Saying when? will it pass the new moon so we may sell grain grain and the sabbath so we may open grain to make small an ephah and to make great a shekel and to falsify balances of deceit.
6 mkiwanunua maskini kwa fedha, na wahitaji kwa jozi ya viatu, na mkiuza hata takataka za ngano pamoja na ngano.
To buy for silver poor [people] and [the] needy for sake of a pair of sandals and refuse of grain we will sell grain.
7 Bwana ameapa kwake mwenyewe, aliye Kiburi cha Yakobo: “Kamwe sitasahau chochote ambacho wamefanya.
He has sworn Yahweh by [the] pride of Jacob if I will forget to perpetuity all deeds their.
8 “Je, nchi haitatetemeka kwa ajili ya hili, nao wote waishio ndani mwake hawataomboleza? Nchi yote itainuka kama Naili; itapanda na kushuka kama mto wa Misri.
¿ On this not will it tremble the land and he will mourn every [one who] dwells in it and it will rise like the light all of it and it will be tossed (and it will sink *Q(K)*) like [the] River of Egypt.
9 “Katika siku ile,” asema Bwana Mwenyezi, “Nitalifanya jua litue alasiri na kuifanya dunia iwe giza wakati wa mchana mwangavu.
And it will be - on the day that [the] utterance of [the] Lord Yahweh and I will cause to go the sun at noon and I will make dark the earth in a day of light.
10 Nitageuza sikukuu zenu za kidini kuwa maombolezo, na kuimba kwenu kote kuwe kilio. Nitawafanya ninyi nyote mvae nguo ya gunia na kunyoa nywele zenu. Nitaufanya wakati ule uwe kama wa kuombolezea mwana wa pekee, na mwisho wake kama siku ya uchungu.
And I will turn feasts your into mourning and all songs your into lamentation and I will bring up on all loins sackcloth and on every head baldness and I will make it like [the] mourning of an only [son] and end its [will be] like a day bitter.
11 “Siku zinakuja,” asema Bwana Mwenyezi, “wakati nitakapotuma njaa katika nchi yote: si njaa ya chakula wala kiu ya maji, lakini njaa ya kusikia maneno ya Bwana.
Here! - days [are] coming [the] utterance of [the] Lord Yahweh and I will send a famine in the land not a famine for bread and not a thirst for water that except for hearing [the] words of Yahweh.
12 Wanaume watayumbayumba kutoka bahari hadi bahari na kutangatanga kutoka kaskazini mpaka mashariki, wakitafuta neno la Bwana, lakini hawatalipata.
And people will stagger from sea to sea and from [the] north and to [the] east they will rove about to seek [the] word of Yahweh and not they will find [it].
13 “Katika siku ile “wasichana wazuri na vijana wanaume wenye nguvu watazimia kwa sababu ya kiu.
In the day that they will become faint the virgins beautiful and the young men by thirst.
14 Wale waapao kwa aibu ya Samaria, au kusema, ‘Hakika kama miungu yenu iishivyo, ee Dani,’ au ‘Hakika kama mungu wa Beer-Sheba aishivyo’: wataanguka, wala hawatasimama tena.”
Those [who] swear by [the] guilt of Samaria and they will say [by] [the] life of gods your O Dan and [by] [the] life of [the] way of Beer Sheba and they will fall and not they will rise again.