< Amosi 7 >
1 Hili ndilo alilonionyesha Bwana Mwenyezi katika maono: Alikuwa anaandaa makundi ya nzige baada ya kuvunwa fungu la mfalme na wakati ule tu mimea ya pili ilipokuwa ikichipua.
Följande syn lät Herren, HERREN mig se; Jag såg gräshoppor skapas, när sommargräset begynte växa upp; och det var sommargräset efter kungsslåttern.
2 Wakati nzige walikuwa wamekula mimea yote ya nchi, nililia kwa sauti kuu, “Bwana Mwenyezi, samehe! Je, Yakobo atawezaje kuendelea kuishi? Yeye ni mdogo sana!”
När så dessa hade ätit upp alla markens örter, sade jag: "Herre, HERRE, förlåt. Huru skall Jakob kunna bestå, han som är så ringa?"
3 Kwa hiyo Bwana akaghairi. Kisha Bwana akasema, “Hili halitatokea.”
Då ångrade HERREN detta. "Det skall icke ske", sade HERREN.
4 Hili ndilo Bwana Mwenyezi alilonionyesha katika maono: Bwana Mwenyezi alikuwa akiita hukumu ya moto; nao ulikausha vilindi vikuu, ukateketeza nchi.
Följande syn lät Herren, HERREN mig se: Jag såg Herren, HERREN nalkas för att utföra sin sak genom eld; och elden förtärde det stora djupet och höll på att förtära arvedelslandet.
5 Ndipo nikalia, “Bwana Mwenyezi, nakusihi, zuia! Je, Yakobo atawezaje kuendelea kuishi? Yeye ni mdogo sana!”
Då sade jag: "Herre, HERRE, håll upp. Huru skall Jakob kunna bestå, han som är så ringa?"
6 Kwa hiyo Bwana akaghairi. Bwana Mwenyezi akasema, “Hili nalo halitatokea.”
Då ångrade HERREN detta. "Icke heller detta skall ske", sade Herren, HERREN.
7 Hili ndilo alilonionyesha katika maono: Bwana alikuwa amesimama karibu na ukuta ambao ulikuwa umejengwa kwa timazi, akiwa na uzi wa timazi mkononi mwake.
Följande syn lät han mig se: Jag såg Herren stå på en mur, uppförd efter sänklod, och i sin hand höll han ett sänklod.
8 Naye Bwana akaniuliza, “Je, Amosi unaona nini?” Nikamjibu, “Uzi wa timazi.” Kisha Bwana akasema, “Tazama, ninaweka uzi wa timazi miongoni mwa watu wangu Israeli; sitawahurumia tena.
Och HERREN sade till mig: "Vad ser du, Amos?" Jag svarade: "Ett sänklod." Då sade Herren: "Se, jag skall hänga upp ett sänklod mitt ibland mitt folk Israel; jag kan icke vidare tillgiva dem.
9 “Mahali pa Isaki pa juu pa kuabudia miungu pataangamizwa, na mahali patakatifu pa Israeli pa kuabudia pataharibiwa; kwa upanga wangu nitainuka dhidi ya nyumba ya Yeroboamu.”
Isaks offerhöjder skola bliva ödelagda och Israels helgedomar förstörda, och mot Jerobeams hus skall jag uppresa mig med svärdet."
10 Kisha Amazia kuhani wa Betheli akatuma ujumbe kwa Yeroboamu mfalme wa Israeli, akisema: “Amosi analeta fitina juu yako katikati ya Israeli. Nchi haiwezi kuvumilia maneno yake yote.
Men Amasja, prästen i Betel, sände till Jerobeam, Israels konung, och lät säga: "Amos förehar en sammansvärjning mot dig, mitt i Israels hus. Landet kan icke härda ut med allt hans ordande.
11 Kwa kuwa hili ndilo Amosi analosema: “‘Yeroboamu atakufa kwa upanga, na kwa hakika Israeli watakwenda uhamishoni, mbali na nchi yao.’”
Ty så har Amos sagt: 'Jerobeam skall dö för svärd, och Israel skall föras bort i fångenskap ur sitt land.'"
12 Kisha Amazia akamwambia Amosi, “Nenda zako, ewe mwonaji! Urudi katika nchi ya Yuda. Ujipatie riziki yako huko na kutoa unabii wako.
Och Amasja sade till Amos: "Du siare, gå din väg och sök din tillflykt i Juda land; där må du äta ditt bröd, och där må du profetera.
13 Usiendelee kutoa unabii katika Betheli, kwa sababu hapa ni mahali pa mfalme pa kuabudia na Hekalu la ufalme huu.”
Men i Betel får du icke vidare profetera, ty det är en konungslig helgedom och ett rikets tempel."
14 Amosi akamjibu Amazia, “Mimi sikuwa nabii wala mwana wa nabii, lakini nilikuwa mchungaji wa kondoo na mtunza mikuyu.
Då svarade Amos och sade till Amasja: "Jag är varken en profet eller en profetlärljunge, jag är en boskapsherde, som lever av mullbärsfikon.
15 Lakini Bwana akanitoa kutoka kuchunga kondoo na kuniambia, ‘Nenda, ukawatabirie watu wangu Israeli.’
Men HERREN tog mig från hjorden; HERREN sade till mig: 'Gå åstad och profetera för mitt folk Israel.'
16 Sasa basi, sikieni neno la Bwana. Ninyi mnasema, “‘Usitabiri dhidi ya Israeli, na uache kuhubiri dhidi ya nyumba ya Isaki.’
Så hör nu HERRENS ord. Du säger: 'Profetera icke mot Israel och predika icke mot Isaks hus.'
17 “Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana: “‘Mke wako atakuwa kahaba mjini, nao wana wako na binti zako watauawa kwa upanga. Shamba lako litapimwa na kugawanywa, na wewe mwenyewe utafia katika nchi ya kipagani. Nayo Israeli kwa hakika itakwenda uhamishoni, mbali na nchi yao.’”
Därför säger HERREN så: Din hustru skall bliva en sköka i staden, dina söner och döttrar skola falla för svärd, ditt land skall bliva utskiftat med mätsnöre, själv skall du dö i ett orent land, och Israel skall föras bort i fångenskap ur sitt land."