< Amosi 7 >

1 Hili ndilo alilonionyesha Bwana Mwenyezi katika maono: Alikuwa anaandaa makundi ya nzige baada ya kuvunwa fungu la mfalme na wakati ule tu mimea ya pili ilipokuwa ikichipua.
Voici ce que m’a montré le Seigneur Dieu: or voici qu’il formait la sauterelle, lorsque les plantes commençaient à germer par la pluie de l’arrière-saison; et voici la pluie de l’arrière-saison après la coupe du roi.
2 Wakati nzige walikuwa wamekula mimea yote ya nchi, nililia kwa sauti kuu, “Bwana Mwenyezi, samehe! Je, Yakobo atawezaje kuendelea kuishi? Yeye ni mdogo sana!”
Et il arriva que lorsque la sauterelle eut achevé de manger l’herbe de la terre, je dis: Seigneur Dieu, soyez propice, je vous conjure; qui rétablira Jacob, car il est bien faible?
3 Kwa hiyo Bwana akaghairi. Kisha Bwana akasema, “Hili halitatokea.”
Sur cela, le Seigneur a eu pitié: Ce que tu crains ne sera pas, dit le Seigneur.
4 Hili ndilo Bwana Mwenyezi alilonionyesha katika maono: Bwana Mwenyezi alikuwa akiita hukumu ya moto; nao ulikausha vilindi vikuu, ukateketeza nchi.
Voici ce que m’a montré le Seigneur Dieu; or, voici que le Seigneur Dieu appelait le feu pour exercer le jugement, et il dévora un grand abîme, et consuma en même temps une partie de la plaine.
5 Ndipo nikalia, “Bwana Mwenyezi, nakusihi, zuia! Je, Yakobo atawezaje kuendelea kuishi? Yeye ni mdogo sana!”
Et je dis: Seigneur Dieu, apaisez-vous, je vous conjure; qui rétablira Jacob, car il est bien faible?
6 Kwa hiyo Bwana akaghairi. Bwana Mwenyezi akasema, “Hili nalo halitatokea.”
Sur cela, le Seigneur eut pitié: Il n’en sera pas ainsi, dit le Seigneur Dieu.
7 Hili ndilo alilonionyesha katika maono: Bwana alikuwa amesimama karibu na ukuta ambao ulikuwa umejengwa kwa timazi, akiwa na uzi wa timazi mkononi mwake.
Voici ce que m’a montré le Seigneur Dieu; voici que le Seigneur se tenait debout sur une muraille crépie, et que dans sa main était une truelle de maçon.
8 Naye Bwana akaniuliza, “Je, Amosi unaona nini?” Nikamjibu, “Uzi wa timazi.” Kisha Bwana akasema, “Tazama, ninaweka uzi wa timazi miongoni mwa watu wangu Israeli; sitawahurumia tena.
Et le Seigneur me dit: Que vois-tu, Amos? Et je dis: Une truelle de maçon. Et le Seigneur dit: Voici que moi je déposerai la truelle au milieu de mon peuple d’Israël; et je ne le crépirai plus à l’avenir.
9 “Mahali pa Isaki pa juu pa kuabudia miungu pataangamizwa, na mahali patakatifu pa Israeli pa kuabudia pataharibiwa; kwa upanga wangu nitainuka dhidi ya nyumba ya Yeroboamu.”
Et les hauts lieux consacrés à l’idole seront détruits, et les sanctuaires d’Israël seront désolés; et je m’élèverai avec le glaive contre la maison de Jéroboam.
10 Kisha Amazia kuhani wa Betheli akatuma ujumbe kwa Yeroboamu mfalme wa Israeli, akisema: “Amosi analeta fitina juu yako katikati ya Israeli. Nchi haiwezi kuvumilia maneno yake yote.
Et Amasias, prêtre de Béthel, envoya vers Jéroboam, roi d’Israël, disant: Amos s’est révolté contre toi au sein de la maison d’Israël. Ta terre ne pourra supporter tous ses discours.
11 Kwa kuwa hili ndilo Amosi analosema: “‘Yeroboamu atakufa kwa upanga, na kwa hakika Israeli watakwenda uhamishoni, mbali na nchi yao.’”
Car voici ce que dit Amos: Par le glaive mourra Jéroboam, et Israël émigrera de sa terre;
12 Kisha Amazia akamwambia Amosi, “Nenda zako, ewe mwonaji! Urudi katika nchi ya Yuda. Ujipatie riziki yako huko na kutoa unabii wako.
Et Amasias dit à Amos: Toi qui vois, va, fuis dans la terre de Juda et mange là ton pain, et tu prophétiseras là.
13 Usiendelee kutoa unabii katika Betheli, kwa sababu hapa ni mahali pa mfalme pa kuabudia na Hekalu la ufalme huu.”
Mais dans Béthel tu ne prophétiseras plus à l’avenir, parce que c’est le sanctuaire du roi, et le siège du royaume.
14 Amosi akamjibu Amazia, “Mimi sikuwa nabii wala mwana wa nabii, lakini nilikuwa mchungaji wa kondoo na mtunza mikuyu.
Et Amos répondit et dit à Amasias: Je ne suis pas fils de prophète, mais je suis pâtre, effeuillant des sycomores.
15 Lakini Bwana akanitoa kutoka kuchunga kondoo na kuniambia, ‘Nenda, ukawatabirie watu wangu Israeli.’
Et le Seigneur m’a pris lorsque je suivais mon troupeau, et le Seigneur m’a dit: Va, prophétise à mon peuple d’Israël.
16 Sasa basi, sikieni neno la Bwana. Ninyi mnasema, “‘Usitabiri dhidi ya Israeli, na uache kuhubiri dhidi ya nyumba ya Isaki.’
Et maintenant écoute la parole du Seigneur: Tu dis: Tu ne prophétiseras pas sur Israël, et tu ne répandras pas tes oracles sur la maison de l’idole.
17 “Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana: “‘Mke wako atakuwa kahaba mjini, nao wana wako na binti zako watauawa kwa upanga. Shamba lako litapimwa na kugawanywa, na wewe mwenyewe utafia katika nchi ya kipagani. Nayo Israeli kwa hakika itakwenda uhamishoni, mbali na nchi yao.’”
À cause de cela, voici ce que dit le Seigneur: Ta femme dans la cité forniquera; tes fils et tes filles sous le glaive tomberont; ton sol sera mesuré au cordeau; et toi, c’est sur une terre souillée que tu mourras, et Israël captif émigrera de sa terre.

< Amosi 7 >