< Amosi 7 >

1 Hili ndilo alilonionyesha Bwana Mwenyezi katika maono: Alikuwa anaandaa makundi ya nzige baada ya kuvunwa fungu la mfalme na wakati ule tu mimea ya pili ilipokuwa ikichipua.
Telle fut la vision qu'offrit à ma vue le Seigneur, l'Éternel: Voici, Il fit naître des sauterelles au commencement de la crue du regain, et voici, le regain poussait après les fenaisons du roi;
2 Wakati nzige walikuwa wamekula mimea yote ya nchi, nililia kwa sauti kuu, “Bwana Mwenyezi, samehe! Je, Yakobo atawezaje kuendelea kuishi? Yeye ni mdogo sana!”
et quand elles eurent entièrement dévoré l'herbe de la terre, je dis: Ah! pardonne, Seigneur Éternel! Comment Jacob tiendra-t-il? car il est chétif.
3 Kwa hiyo Bwana akaghairi. Kisha Bwana akasema, “Hili halitatokea.”
L'Éternel se repentit de cela. Cela n'arrivera pas, dit l'Éternel.
4 Hili ndilo Bwana Mwenyezi alilonionyesha katika maono: Bwana Mwenyezi alikuwa akiita hukumu ya moto; nao ulikausha vilindi vikuu, ukateketeza nchi.
Telle fut la vision qu'offrit à ma vue le Seigneur, l'Éternel. Voici, le Seigneur, l'Éternel appela le feu pour punir, et le feu dévora le grand abîme, et dévora le champ.
5 Ndipo nikalia, “Bwana Mwenyezi, nakusihi, zuia! Je, Yakobo atawezaje kuendelea kuishi? Yeye ni mdogo sana!”
Alors je dis: Ah! Seigneur, Éternel, arrête! Comment Jacob tiendra-t-il? car il est chétif.
6 Kwa hiyo Bwana akaghairi. Bwana Mwenyezi akasema, “Hili nalo halitatokea.”
L'Éternel se repentit de cela. Cela non plus n'arrivera pas, dit le Seigneur, l'Éternel.
7 Hili ndilo alilonionyesha katika maono: Bwana alikuwa amesimama karibu na ukuta ambao ulikuwa umejengwa kwa timazi, akiwa na uzi wa timazi mkononi mwake.
Telle fut la vision qu'il offrit à ma vue. Voici, le Seigneur était debout sur une muraille tombant à plomb, et dans sa main Il avait un plomb.
8 Naye Bwana akaniuliza, “Je, Amosi unaona nini?” Nikamjibu, “Uzi wa timazi.” Kisha Bwana akasema, “Tazama, ninaweka uzi wa timazi miongoni mwa watu wangu Israeli; sitawahurumia tena.
Et l'Éternel me dit: Que vois-tu, Amos? Et je dis: Un plomb. Et le Seigneur dit: Voici, je ferai passer un plomb par-dessus mon peuple d'Israël; désormais je ne lui pardonnerai plus,
9 “Mahali pa Isaki pa juu pa kuabudia miungu pataangamizwa, na mahali patakatifu pa Israeli pa kuabudia pataharibiwa; kwa upanga wangu nitainuka dhidi ya nyumba ya Yeroboamu.”
et les hauteurs d'Isaac seront ravagées, et les sanctuaires d'Israël dévastés, et je me lèverai contre la maison de Jéroboam avec l'épée.
10 Kisha Amazia kuhani wa Betheli akatuma ujumbe kwa Yeroboamu mfalme wa Israeli, akisema: “Amosi analeta fitina juu yako katikati ya Israeli. Nchi haiwezi kuvumilia maneno yake yote.
Alors Amatsia, prêtre de Béthel, fit dire à Jéroboam, roi d'Israël: Amos conspire contre toi au sein de la maison d'Israël; le pays ne peut supporter tous ses discours;
11 Kwa kuwa hili ndilo Amosi analosema: “‘Yeroboamu atakufa kwa upanga, na kwa hakika Israeli watakwenda uhamishoni, mbali na nchi yao.’”
car ainsi a parlé Amos: Jéroboam périra par l'épée, et Israël sera emmené captif loin de son pays.
12 Kisha Amazia akamwambia Amosi, “Nenda zako, ewe mwonaji! Urudi katika nchi ya Yuda. Ujipatie riziki yako huko na kutoa unabii wako.
Cependant Amatsia dit à Amos: Voyant, va-t'en, fuis au pays de Juda, et manges-y ton pain et y prophétise!
13 Usiendelee kutoa unabii katika Betheli, kwa sababu hapa ni mahali pa mfalme pa kuabudia na Hekalu la ufalme huu.”
Mais à Béthel ne prophétise pas davantage, car c'est un sanctuaire royal, et une résidence royale.
14 Amosi akamjibu Amazia, “Mimi sikuwa nabii wala mwana wa nabii, lakini nilikuwa mchungaji wa kondoo na mtunza mikuyu.
Alors Amos répondit et dit à Amatsia: Je ne suis point prophète, ni fils de prophète, mais un berger, et je cultive des sycomores;
15 Lakini Bwana akanitoa kutoka kuchunga kondoo na kuniambia, ‘Nenda, ukawatabirie watu wangu Israeli.’
et l'Éternel m'a fait quitter les troupeaux, et l'Éternel m'a dit: Va prophétiser contre mon peuple d'Israël.
16 Sasa basi, sikieni neno la Bwana. Ninyi mnasema, “‘Usitabiri dhidi ya Israeli, na uache kuhubiri dhidi ya nyumba ya Isaki.’
Or maintenant, écoute la parole de l'Éternel. Tu dis: « Ne prophétise plus contre Israël, et ne parle plus contre la maison d'Isaac! »
17 “Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana: “‘Mke wako atakuwa kahaba mjini, nao wana wako na binti zako watauawa kwa upanga. Shamba lako litapimwa na kugawanywa, na wewe mwenyewe utafia katika nchi ya kipagani. Nayo Israeli kwa hakika itakwenda uhamishoni, mbali na nchi yao.’”
c'est pourquoi ainsi parle l'Éternel: Ta femme sera violée dans la ville, et tes fils et tes filles périront par l'épée, et ton pays sera partagé au cordeau, et toi tu mourras sur une terre impure, et Israël sera emmené captif loin de son pays.

< Amosi 7 >