< Amosi 7 >
1 Hili ndilo alilonionyesha Bwana Mwenyezi katika maono: Alikuwa anaandaa makundi ya nzige baada ya kuvunwa fungu la mfalme na wakati ule tu mimea ya pili ilipokuwa ikichipua.
Ainsi me fit voir le Seigneur Yahweh, et voici qu’il formait des sauterelles, au commencement de la pousse des regains; c’était le regain après la coupe du roi.
2 Wakati nzige walikuwa wamekula mimea yote ya nchi, nililia kwa sauti kuu, “Bwana Mwenyezi, samehe! Je, Yakobo atawezaje kuendelea kuishi? Yeye ni mdogo sana!”
Quand elles eurent achevé de dévorer l’herbe de la terre, je dis: « Seigneur Yahweh, daignez pardonner! Comment Jacob tiendra-t-il? Car il est petit. »
3 Kwa hiyo Bwana akaghairi. Kisha Bwana akasema, “Hili halitatokea.”
Et Yahweh se repentit de cela: « Cela ne sera pas », dit Yahweh.
4 Hili ndilo Bwana Mwenyezi alilonionyesha katika maono: Bwana Mwenyezi alikuwa akiita hukumu ya moto; nao ulikausha vilindi vikuu, ukateketeza nchi.
Ainsi me fit voir le Seigneur Yahweh, et voici que le Seigneur Yahweh venait châtier par le feu, et le feu dévorait le grand abîme, et il dévorait la portion du Seigneur.
5 Ndipo nikalia, “Bwana Mwenyezi, nakusihi, zuia! Je, Yakobo atawezaje kuendelea kuishi? Yeye ni mdogo sana!”
Et je dis: « Seigneur Yahweh, daignez cesser! Comment Jacob tiendra-t-il? Car il est petit. »
6 Kwa hiyo Bwana akaghairi. Bwana Mwenyezi akasema, “Hili nalo halitatokea.”
Yahweh se repentit: « Cela non plus ne sera pas », dit le Seigneur Yahweh.
7 Hili ndilo alilonionyesha katika maono: Bwana alikuwa amesimama karibu na ukuta ambao ulikuwa umejengwa kwa timazi, akiwa na uzi wa timazi mkononi mwake.
Ainsi me fit voir Yahweh, et voici que le Seigneur se tenait sur un mur vertical, et il avait dans sa main un fil à plomb.
8 Naye Bwana akaniuliza, “Je, Amosi unaona nini?” Nikamjibu, “Uzi wa timazi.” Kisha Bwana akasema, “Tazama, ninaweka uzi wa timazi miongoni mwa watu wangu Israeli; sitawahurumia tena.
Et Yahweh me dit: « Que vois-tu, Amos? » Je répondis: « Un fil à plomb. » Et le Seigneur me dit: « Voici que je mets le fil à plomb au milieu de mon peuple d’Israël; je ne lui pardonnerai pas plus longtemps.
9 “Mahali pa Isaki pa juu pa kuabudia miungu pataangamizwa, na mahali patakatifu pa Israeli pa kuabudia pataharibiwa; kwa upanga wangu nitainuka dhidi ya nyumba ya Yeroboamu.”
Les hauts lieux d’Isaac seront dévastés, et les sanctuaires d’Israël seront détruits, et je me lèverai contre la maison de Jéroboam, avec l’épée. »
10 Kisha Amazia kuhani wa Betheli akatuma ujumbe kwa Yeroboamu mfalme wa Israeli, akisema: “Amosi analeta fitina juu yako katikati ya Israeli. Nchi haiwezi kuvumilia maneno yake yote.
Et Amasias, prêtre de Béthel, envoya dire à Jéroboam, roi d’Israël: « Amos conspire contre toi au milieu de la maison d’Israël; le pays ne peut plus supporter toutes ses paroles.
11 Kwa kuwa hili ndilo Amosi analosema: “‘Yeroboamu atakufa kwa upanga, na kwa hakika Israeli watakwenda uhamishoni, mbali na nchi yao.’”
Car Amos a parlé ainsi: Jéroboam mourra par l’épée, et Israël sera emmené captif hors de son pays. »
12 Kisha Amazia akamwambia Amosi, “Nenda zako, ewe mwonaji! Urudi katika nchi ya Yuda. Ujipatie riziki yako huko na kutoa unabii wako.
Et Amasias dit à Amos: « Voyant, va-t-en, fuis au pays de Juda, et manges-y ton pain; là tu prophétiseras.
13 Usiendelee kutoa unabii katika Betheli, kwa sababu hapa ni mahali pa mfalme pa kuabudia na Hekalu la ufalme huu.”
Mais ne continue pas de prophétiser à Béthel, car c’est un sanctuaire du roi, et c’est une maison royale ».
14 Amosi akamjibu Amazia, “Mimi sikuwa nabii wala mwana wa nabii, lakini nilikuwa mchungaji wa kondoo na mtunza mikuyu.
Amos répondit et dit à Amasias: « Je ne suis pas un prophète, je ne suis pas un fils de prophète; je suis bouvier et je cultive les sycomores.
15 Lakini Bwana akanitoa kutoka kuchunga kondoo na kuniambia, ‘Nenda, ukawatabirie watu wangu Israeli.’
Et Yahweh m’a pris derrière le troupeau, et Yahweh m’a dit: Va, prophétise à mon peuple d’Israël.
16 Sasa basi, sikieni neno la Bwana. Ninyi mnasema, “‘Usitabiri dhidi ya Israeli, na uache kuhubiri dhidi ya nyumba ya Isaki.’
Et maintenant, écoute la parole de Yahweh: Tu dis: Tu ne prophétiseras pas contre Israël, et tu ne parleras pas contre la maison d’Isaac!…
17 “Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana: “‘Mke wako atakuwa kahaba mjini, nao wana wako na binti zako watauawa kwa upanga. Shamba lako litapimwa na kugawanywa, na wewe mwenyewe utafia katika nchi ya kipagani. Nayo Israeli kwa hakika itakwenda uhamishoni, mbali na nchi yao.’”
C’est pourquoi ainsi parle Yahweh: Ta femme sera prostituée dans la ville, tes fils et tes filles tomberont par l’épée, ta terre sera partagée au cordeau; et toi, tu mourras sur une terre impure, et Israël sera emmené captif hors de sa terre. »