< Amosi 7 >
1 Hili ndilo alilonionyesha Bwana Mwenyezi katika maono: Alikuwa anaandaa makundi ya nzige baada ya kuvunwa fungu la mfalme na wakati ule tu mimea ya pili ilipokuwa ikichipua.
Tämän näytti minulle Herra, Herra: Katso, hän loi heinäsirkkoja, kun äpäreheinä alkoi nousta; ja katso, se oli äpäreheinä kuninkaan niitosten jälkeen.
2 Wakati nzige walikuwa wamekula mimea yote ya nchi, nililia kwa sauti kuu, “Bwana Mwenyezi, samehe! Je, Yakobo atawezaje kuendelea kuishi? Yeye ni mdogo sana!”
Ja kun ne olivat syöneet loppuun maan kasvit, sanoin minä: "Herra, Herra, anna anteeksi. Kuinka voi Jaakob pysyä, sillä hän on vähäinen?"
3 Kwa hiyo Bwana akaghairi. Kisha Bwana akasema, “Hili halitatokea.”
Niin Herra katui sitä. "Ei se ole tapahtuva", sanoi Herra.
4 Hili ndilo Bwana Mwenyezi alilonionyesha katika maono: Bwana Mwenyezi alikuwa akiita hukumu ya moto; nao ulikausha vilindi vikuu, ukateketeza nchi.
Tämän näytti minulle Herra, Herra: Katso, Herra, Herra kutsui tulen toimittamaan tuomiota, ja se kulutti suuren syvyyden, ja se kulutti peltomaan.
5 Ndipo nikalia, “Bwana Mwenyezi, nakusihi, zuia! Je, Yakobo atawezaje kuendelea kuishi? Yeye ni mdogo sana!”
Niin minä sanoin: "Herra, Herra, lakkaa jo. Kuinka voi Jaakob pysyä, sillä hän on vähäinen?"
6 Kwa hiyo Bwana akaghairi. Bwana Mwenyezi akasema, “Hili nalo halitatokea.”
Niin Herra katui sitä. "Ei sekään ole tapahtuva", sanoi Herra, Herra.
7 Hili ndilo alilonionyesha katika maono: Bwana alikuwa amesimama karibu na ukuta ambao ulikuwa umejengwa kwa timazi, akiwa na uzi wa timazi mkononi mwake.
Tämän hän näytti minulle: Katso, Herra seisoi pystysuoralla muurilla, kädessänsä luotilanka.
8 Naye Bwana akaniuliza, “Je, Amosi unaona nini?” Nikamjibu, “Uzi wa timazi.” Kisha Bwana akasema, “Tazama, ninaweka uzi wa timazi miongoni mwa watu wangu Israeli; sitawahurumia tena.
Ja Herra sanoi minulle: "Mitä sinä näet, Aamos?" Minä vastasin: "Luotilangan". Ja Herra sanoi minulle: "Katso, minä olen laskenut luotilangan kansani Israelin keskelle. Minä en enää mene säästäen sen ohitse,
9 “Mahali pa Isaki pa juu pa kuabudia miungu pataangamizwa, na mahali patakatifu pa Israeli pa kuabudia pataharibiwa; kwa upanga wangu nitainuka dhidi ya nyumba ya Yeroboamu.”
vaan Iisakin uhrikukkulat tulevat autioiksi ja Israelin pyhäköt raunioiksi. Ja minä nousen ja nostan miekan Jerobeamin sukua vastaan."
10 Kisha Amazia kuhani wa Betheli akatuma ujumbe kwa Yeroboamu mfalme wa Israeli, akisema: “Amosi analeta fitina juu yako katikati ya Israeli. Nchi haiwezi kuvumilia maneno yake yote.
Silloin Amasja, Beetelin pappi, lähetti Jerobeamille, Israelin kuninkaalle, tämän sanan: "Aamos on tehnyt salaliiton sinua vastaan Israelin heimon keskuudessa. Ei maa kestä kaikkea, mitä hän puhuu.
11 Kwa kuwa hili ndilo Amosi analosema: “‘Yeroboamu atakufa kwa upanga, na kwa hakika Israeli watakwenda uhamishoni, mbali na nchi yao.’”
Sillä näin on Aamos sanonut: 'Jerobeam kuolee miekkaan, ja Israel viedään pakkosiirtolaisuuteen, pois omasta maastansa'."
12 Kisha Amazia akamwambia Amosi, “Nenda zako, ewe mwonaji! Urudi katika nchi ya Yuda. Ujipatie riziki yako huko na kutoa unabii wako.
Ja Amasja sanoi Aamokselle: "Sinä näkijä, mene matkaasi ja pakene Juudan maahan, syö leipäsi siellä ja ennusta siellä.
13 Usiendelee kutoa unabii katika Betheli, kwa sababu hapa ni mahali pa mfalme pa kuabudia na Hekalu la ufalme huu.”
Mutta Beetelissä älä ennusta enää, sillä se on kuninkaan pyhäkkö ja valtakunnan temppeli."
14 Amosi akamjibu Amazia, “Mimi sikuwa nabii wala mwana wa nabii, lakini nilikuwa mchungaji wa kondoo na mtunza mikuyu.
Niin Aamos vastasi ja sanoi Amasjalle: "En minä ole profeetta enkä profeetanoppilas, vaan minä olen paimen ja metsäviikunapuiden viljelijä.
15 Lakini Bwana akanitoa kutoka kuchunga kondoo na kuniambia, ‘Nenda, ukawatabirie watu wangu Israeli.’
Ja Herra otti minut laumojeni äärestä, ja Herra sanoi minulle: 'Mene ja ennusta minun kansaani Israelia vastaan'.
16 Sasa basi, sikieni neno la Bwana. Ninyi mnasema, “‘Usitabiri dhidi ya Israeli, na uache kuhubiri dhidi ya nyumba ya Isaki.’
Kuule siis nyt Herran sana: Sinä sanot: 'Älä ennusta Israelia vastaan, äläkä saarnaa Iisakin heimoa vastaan'.
17 “Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana: “‘Mke wako atakuwa kahaba mjini, nao wana wako na binti zako watauawa kwa upanga. Shamba lako litapimwa na kugawanywa, na wewe mwenyewe utafia katika nchi ya kipagani. Nayo Israeli kwa hakika itakwenda uhamishoni, mbali na nchi yao.’”
Sentähden, näin sanoo Herra: Sinun vaimosi joutuu portoksi kaupungissa, sinun poikasi ja tyttäresi kaatuvat miekkaan, sinun maasi jaetaan mittanuoralla, sinä itse kuolet saastaisessa maassa, ja Israel viedään pakkosiirtolaisuuteen, pois omasta maastansa."