< Amosi 6 >
1 Ole wenu ninyi mnaostarehe na kuridhika katika Sayuni, na ninyi mnaojisikia salama juu ya Mlima Samaria, ninyi watu mashuhuri wa taifa lililoendelea kuliko mataifa mengine, ambao watu wa Israeli wanawategemea!
Teško bezbrižnima u Sionu i onima koji su bez straha u gori Samarijskoj, koji su na glasu izmeðu poglavica narodima, ka kojima dolazi dom Izrailjev.
2 Nendeni Kalne mkaone kutoka huko; mwende hadi Hamathi iliyo kuu, kisha mshuke hadi Gathi ya Wafilisti. Je, wao ni bora kuliko falme zenu mbili? Je, nchi yao ni kubwa kuliko yenu?
Proðite u Halnu i vidite, i odande idite u veliki Emat, poslije siðite u Gat Filistejski; je li koje carstvo bolje od ovijeh? jesu li im meðe prostranije od vaših meða?
3 Mnaiweka mbali siku iliyo mbaya na kuleta karibu utawala wa kuogofya.
Teško vama koji mislite da je daleko zli dan, a primièete stolicu na kojoj je nasilje;
4 Ninyi mnalala juu ya vitanda vilivyofunikwa kwa pembe za ndovu, na kujinyoosha juu ya viti vya fahari. Mnajilisha kwa wana-kondoo wazuri na ndama walionenepeshwa.
Koji liježete na odrima od slonove kosti i pružate se na posteljama svojim, i jedete jaganjce iz stada i teoce ugojene;
5 Ninyi mnapiga vinubi kama Daudi, huku mkitunga nyimbo za vinanda mbalimbali.
Koji pjevate uza psaltire, i izmišljate sprave muzièke kao David;
6 Mnakunywa mvinyo kwa bakuli zilizojazwa, na mnajipaka mafuta mazuri, lakini hamhuzuniki kwa maangamizi ya Yosefu.
Koji pijete vino velikim èašama, i mažete se skupocjenijem mirisima, a ne marite za polom Josifov.
7 Kwa hiyo mtakuwa miongoni mwa watu wa kwanza kwenda uhamishoni; karamu zenu na kustarehe kutakoma.
Zato æe sada otiæi u ropstvo meðu prvima koji æe otiæi u ropstvo, i prestaæe radost onijeh koji se goste.
8 Bwana Mwenyezi ameapa kwa nafsi yake mwenyewe: Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote asema: “Nachukia kiburi cha Yakobo, nachukia ngome zake; nitautoa mji wao na kila kitu kilichomo ndani mwake.”
Zakle se Gospod Gospod sobom, govori Gospod Bog nad vojskama: ja se gadim na ponos Jakovljev i mrzim na dvorove njegove; zato æu predati grad i sve što je u njemu.
9 Kama watu kumi watabaki katika nyumba moja, wao pia watakufa.
I ako deset ljudi ostane u jednoj kuæi, umrijeæe.
10 Kama jamaa ambaye atachoma miili akija ili kuitoa nje ya nyumba, na kumuuliza yeyote ambaye bado anajificha humo, “Je, yuko mtu yeyote pamoja nawe?” Naye akisema, “Hapana,” ndipo atakaposema, “Nyamaza kimya! Haturuhusiwi kutaja jina la Bwana.”
I kad uzme koga stric mu ili koji æe ga spaliti da iznese kosti njegove iz kuæe, reæi æe onome koji bude u kutu u kuæi: ima li jošte ko kod tebe? A on æe reæi: nema nikoga. A on æe reæi: muèi; jer ne pominjaše imena Gospodnjega.
11 Kwa kuwa Bwana ameamuru, naye atabomoa jumba kubwa vipande vipande na nyumba ndogo vipande vidogo vidogo.
Jer evo, Gospod zapovijeda i udariæe dom veliki da se razvali i mali dom da popuca.
12 Je, farasi waweza kukimbia kwenye miamba mikali? Je, aweza mtu kulima huko kwa maksai? Lakini mmegeuza haki kuwa sumu na matunda ya uadilifu kuwa uchungu:
Trèe li konji po stijeni i ore li se volovima? jer vi pretvoriste sud u žuè, i plod od pravde u pelen.
13 ninyi mnaoshangilia kushindwa kwa Lo-Debari na kusema, “Je, hatukuteka Karnaimu kwa nguvu zetu wenyewe?”
Vi se radujete onome što nije ništa, i govorite: nijesmo li svojom snagom dobili rogove?
14 Maana Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote asema, “Nitainua taifa dhidi yenu, ee nyumba ya Israeli, nalo litawatesa kuanzia Lebo-Hamathi hadi Bonde la Araba.”
Jer, gle, ja æu podignuti na vas, dome Izrailjev, govori Gospod Bog nad vojskama, narod, koji æe vas pritijesniti od ulaska u Emat do potoka u pustinji.