< Amosi 6 >
1 Ole wenu ninyi mnaostarehe na kuridhika katika Sayuni, na ninyi mnaojisikia salama juu ya Mlima Samaria, ninyi watu mashuhuri wa taifa lililoendelea kuliko mataifa mengine, ambao watu wa Israeli wanawategemea!
Malheur à ces insouciants de Sion, à ces présomptueux de la montagne de Samarie, nobles du premier des peuples, à qui vient la maison d'Israël!
2 Nendeni Kalne mkaone kutoka huko; mwende hadi Hamathi iliyo kuu, kisha mshuke hadi Gathi ya Wafilisti. Je, wao ni bora kuliko falme zenu mbili? Je, nchi yao ni kubwa kuliko yenu?
Passez à Calné et voyez; de là allez à Hamath la grande, puis descendez à Gath dans la Philistie! Ces États sont-ils plus prospères que ces royaumes, ou leur territoire est-il plus grand que votre territoire?
3 Mnaiweka mbali siku iliyo mbaya na kuleta karibu utawala wa kuogofya.
Vous croyez éloigné le jour du malheur, et vous mettez la violence sur le trône;
4 Ninyi mnalala juu ya vitanda vilivyofunikwa kwa pembe za ndovu, na kujinyoosha juu ya viti vya fahari. Mnajilisha kwa wana-kondoo wazuri na ndama walionenepeshwa.
ils sont couchés sur des lits d'ivoire et étendus sur leurs divans, et ils mangent les agneaux du troupeau et les veaux attachés dans l'étable;
5 Ninyi mnapiga vinubi kama Daudi, huku mkitunga nyimbo za vinanda mbalimbali.
ils poussent des éclats de voix au son du luth, et comme David composent des modulations;
6 Mnakunywa mvinyo kwa bakuli zilizojazwa, na mnajipaka mafuta mazuri, lakini hamhuzuniki kwa maangamizi ya Yosefu.
ils boivent dans des cratères à vin, et s'oignent de la meilleure huile, et ils sont insensibles à la plaie de Joseph.
7 Kwa hiyo mtakuwa miongoni mwa watu wa kwanza kwenda uhamishoni; karamu zenu na kustarehe kutakoma.
Aussi maintenant ils s'en iront captifs à la tête des captifs; leurs bruyants propos de table cesseront.
8 Bwana Mwenyezi ameapa kwa nafsi yake mwenyewe: Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote asema: “Nachukia kiburi cha Yakobo, nachukia ngome zake; nitautoa mji wao na kila kitu kilichomo ndani mwake.”
Le Seigneur, l'Éternel, le jure par lui-même; c'est l'arrêt de l'Éternel, Dieu des armées: J'abhorre l'orgueil de Jacob, et ses palais me sont odieux, et je livre la ville et ce qu'elle renferme.
9 Kama watu kumi watabaki katika nyumba moja, wao pia watakufa.
Que s'il reste dix hommes dans une maison, ils mourront aussi.
10 Kama jamaa ambaye atachoma miili akija ili kuitoa nje ya nyumba, na kumuuliza yeyote ambaye bado anajificha humo, “Je, yuko mtu yeyote pamoja nawe?” Naye akisema, “Hapana,” ndipo atakaposema, “Nyamaza kimya! Haturuhusiwi kutaja jina la Bwana.”
L'un d'eux est emporté par son parent, et celui qui doit brûler les corps enlève ses os de la maison, et dit à celui qui est au dedans de la maison: Y a-t-il encore quelqu'un avec toi? Celui-ci lui répond: Personne!… Et il reprend: Silence! ce n'est pas le lieu de louer le nom de l'Éternel.
11 Kwa kuwa Bwana ameamuru, naye atabomoa jumba kubwa vipande vipande na nyumba ndogo vipande vidogo vidogo.
Car voici, l'Éternel l'a décidé, Il fait tomber en ruines la grande maison, et la petite en débris.
12 Je, farasi waweza kukimbia kwenye miamba mikali? Je, aweza mtu kulima huko kwa maksai? Lakini mmegeuza haki kuwa sumu na matunda ya uadilifu kuwa uchungu:
Fait-on courir des chevaux sur un rocher, ou y laboure-t-on avec le bœuf, que vous transformez le droit en poison et le fruit de la justice en absinthe?
13 ninyi mnaoshangilia kushindwa kwa Lo-Debari na kusema, “Je, hatukuteka Karnaimu kwa nguvu zetu wenyewe?”
Vous qui faites votre joie du néant et qui dites: N'est-ce pas par notre force que nous conquîmes la puissance?
14 Maana Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote asema, “Nitainua taifa dhidi yenu, ee nyumba ya Israeli, nalo litawatesa kuanzia Lebo-Hamathi hadi Bonde la Araba.”
Car voici, je vais faire lever contre vous, maison d'Israël, dit l'Éternel, Dieu des armées, un peuple qui vous accablera depuis Hamath jusqu'à la rivière de la plaine.