< Amosi 6 >

1 Ole wenu ninyi mnaostarehe na kuridhika katika Sayuni, na ninyi mnaojisikia salama juu ya Mlima Samaria, ninyi watu mashuhuri wa taifa lililoendelea kuliko mataifa mengine, ambao watu wa Israeli wanawategemea!
Malheur à ceux qui vivent tranquilles dans Sion, et à ceux qui sont en sécurité sur la montagne de Samarie! Aux principaux de la première des nations, et vers lesquels va la maison d'Israël!
2 Nendeni Kalne mkaone kutoka huko; mwende hadi Hamathi iliyo kuu, kisha mshuke hadi Gathi ya Wafilisti. Je, wao ni bora kuliko falme zenu mbili? Je, nchi yao ni kubwa kuliko yenu?
Passez à Calné, et voyez; allez de là à Hamath la grande, et descendez à Gath des Philistins. Sont-ils plus prospères que ces royaumes-ci, ou leur territoire est-il plus grand que votre territoire?
3 Mnaiweka mbali siku iliyo mbaya na kuleta karibu utawala wa kuogofya.
Vous qui repoussez le jour de la calamité, et qui rapprochez le siège de la violence!
4 Ninyi mnalala juu ya vitanda vilivyofunikwa kwa pembe za ndovu, na kujinyoosha juu ya viti vya fahari. Mnajilisha kwa wana-kondoo wazuri na ndama walionenepeshwa.
Ils se couchent sur des lits d'ivoire, et s'étendent sur leurs coussins; ils mangent les agneaux du troupeau, et les veaux pris du lieu où on les engraisse;
5 Ninyi mnapiga vinubi kama Daudi, huku mkitunga nyimbo za vinanda mbalimbali.
Ils divaguent au son du luth; comme David, ils inventent des instruments de musique;
6 Mnakunywa mvinyo kwa bakuli zilizojazwa, na mnajipaka mafuta mazuri, lakini hamhuzuniki kwa maangamizi ya Yosefu.
Ils boivent le vin dans de grands vases; ils s'oignent avec la meilleure huile, et ne sont pas dans la douleur pour la ruine de Joseph.
7 Kwa hiyo mtakuwa miongoni mwa watu wa kwanza kwenda uhamishoni; karamu zenu na kustarehe kutakoma.
C'est pourquoi ils vont être emmenés à la tête des captifs, et les clameurs des voluptueux cesseront.
8 Bwana Mwenyezi ameapa kwa nafsi yake mwenyewe: Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote asema: “Nachukia kiburi cha Yakobo, nachukia ngome zake; nitautoa mji wao na kila kitu kilichomo ndani mwake.”
Le Seigneur, l'Éternel, l'a juré par lui-même, dit l'Éternel, le Dieu des armées: Je déteste l'orgueil de Jacob, et je hais ses palais; je livrerai la ville et ce qu'elle contient.
9 Kama watu kumi watabaki katika nyumba moja, wao pia watakufa.
Que s'il reste dix hommes dans une maison, ils mourront aussi.
10 Kama jamaa ambaye atachoma miili akija ili kuitoa nje ya nyumba, na kumuuliza yeyote ambaye bado anajificha humo, “Je, yuko mtu yeyote pamoja nawe?” Naye akisema, “Hapana,” ndipo atakaposema, “Nyamaza kimya! Haturuhusiwi kutaja jina la Bwana.”
Et le proche parent d'un mort, et celui qui doit le brûler, le prendra pour emporter les os hors de la maison, et il dira à celui qui est au fond de la maison: Y a-t-il encore quelqu'un auprès de toi? Et il répondra: Il n'y en a plus! Puis il dira: Silence! ce n'est pas le moment de prononcer le nom de l'Éternel.
11 Kwa kuwa Bwana ameamuru, naye atabomoa jumba kubwa vipande vipande na nyumba ndogo vipande vidogo vidogo.
Car voici, l'Éternel donne ses ordres, et il fera tomber la grande maison en ruines, et la petite maison en débris.
12 Je, farasi waweza kukimbia kwenye miamba mikali? Je, aweza mtu kulima huko kwa maksai? Lakini mmegeuza haki kuwa sumu na matunda ya uadilifu kuwa uchungu:
Des chevaux courent-ils sur le rocher, ou y laboure-t-on avec des bœufs, que vous ayez changé le droit en poison, et le fruit de la justice en absinthe?
13 ninyi mnaoshangilia kushindwa kwa Lo-Debari na kusema, “Je, hatukuteka Karnaimu kwa nguvu zetu wenyewe?”
Vous qui vous réjouissez en ce qui n'est rien, vous qui dites: N'est-ce pas par notre force que nous avons acquis de la puissance?
14 Maana Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote asema, “Nitainua taifa dhidi yenu, ee nyumba ya Israeli, nalo litawatesa kuanzia Lebo-Hamathi hadi Bonde la Araba.”
Car voici, je vais faire lever contre vous, maison d'Israël, dit l'Éternel, le Dieu des armées, une nation qui vous opprimera, depuis l'entrée de Hamath jusqu'au torrent du désert.

< Amosi 6 >