< Amosi 6 >

1 Ole wenu ninyi mnaostarehe na kuridhika katika Sayuni, na ninyi mnaojisikia salama juu ya Mlima Samaria, ninyi watu mashuhuri wa taifa lililoendelea kuliko mataifa mengine, ambao watu wa Israeli wanawategemea!
Hola! vous qui êtes à votre aise en Sion, et vous qui vous confiez en la montagne de Samarie, [lieux] les plus renommés d'entre les principaux des nations, auxquels va la maison d'Israël.
2 Nendeni Kalne mkaone kutoka huko; mwende hadi Hamathi iliyo kuu, kisha mshuke hadi Gathi ya Wafilisti. Je, wao ni bora kuliko falme zenu mbili? Je, nchi yao ni kubwa kuliko yenu?
Passez jusqu'à Calne, et regardez; et vous en allez de là à Hamath la grande; puis descendez à Gath des Philistins; n'étaient-ils pas plus excellents que ces Royaumes-ci? Leur pays n'était-il pas plus étendu que votre pays?
3 Mnaiweka mbali siku iliyo mbaya na kuleta karibu utawala wa kuogofya.
Vous qui éloignez les jours de la calamité, et qui approchez de vous le siège de violence;
4 Ninyi mnalala juu ya vitanda vilivyofunikwa kwa pembe za ndovu, na kujinyoosha juu ya viti vya fahari. Mnajilisha kwa wana-kondoo wazuri na ndama walionenepeshwa.
Qui vous couchez sur des lits d'ivoire, et vous étendez sur vos couches; qui mangez les agneaux [choisis] du troupeau, et les veaux pris du lieu où on les engraisse;
5 Ninyi mnapiga vinubi kama Daudi, huku mkitunga nyimbo za vinanda mbalimbali.
Qui fredonnez au son de la musette; qui inventez des instruments de musique, comme David;
6 Mnakunywa mvinyo kwa bakuli zilizojazwa, na mnajipaka mafuta mazuri, lakini hamhuzuniki kwa maangamizi ya Yosefu.
Qui buvez le vin dans des bassins, et vous parfumez des parfums les plus exquis, et qui n'êtes point malades pour la plaie de Joseph.
7 Kwa hiyo mtakuwa miongoni mwa watu wa kwanza kwenda uhamishoni; karamu zenu na kustarehe kutakoma.
A cause de cela ils s'en iront incessamment en captivité, entre les premiers qui s'en iront en captivité, et le luxe de ces personnes voluptueuses prendra fin.
8 Bwana Mwenyezi ameapa kwa nafsi yake mwenyewe: Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote asema: “Nachukia kiburi cha Yakobo, nachukia ngome zake; nitautoa mji wao na kila kitu kilichomo ndani mwake.”
Le Seigneur l'Eternel a juré par soi-même, l'Eternel Dieu des armées dit ainsi: J'ai en détestation l'orgueil de Jacob, et j'ai en haine ses palais, c'est pourquoi je livrerai la ville, et tout ce qui est en elle.
9 Kama watu kumi watabaki katika nyumba moja, wao pia watakufa.
Et s'il arrive qu'il y ait dix hommes de reste dans une maison, ils mourront.
10 Kama jamaa ambaye atachoma miili akija ili kuitoa nje ya nyumba, na kumuuliza yeyote ambaye bado anajificha humo, “Je, yuko mtu yeyote pamoja nawe?” Naye akisema, “Hapana,” ndipo atakaposema, “Nyamaza kimya! Haturuhusiwi kutaja jina la Bwana.”
Et l'oncle de chacun d'eux les prendra, et les brûlera pour en mettre les os hors de la maison; et il dira à celui qui sera au fond de la maison: y a-t-il encore quelqu'un avec toi? Et il répondra: C'en est la fin. Puis [son oncle lui] dira: Tais-toi; car [aussi] ils n'eussent point fait commémoration du nom de l'Eternel.
11 Kwa kuwa Bwana ameamuru, naye atabomoa jumba kubwa vipande vipande na nyumba ndogo vipande vidogo vidogo.
Car voici l'Eternel commande, et il frappera les grandes maisons par des débordements d'eau, et les petites maisons par des fentes.
12 Je, farasi waweza kukimbia kwenye miamba mikali? Je, aweza mtu kulima huko kwa maksai? Lakini mmegeuza haki kuwa sumu na matunda ya uadilifu kuwa uchungu:
Les chevaux courront-ils par les rochers? ou y labourera-t-on avec des bœufs? mais vous avez changé le jugement en fiel, et le fruit de la justice en absinthe.
13 ninyi mnaoshangilia kushindwa kwa Lo-Debari na kusema, “Je, hatukuteka Karnaimu kwa nguvu zetu wenyewe?”
Vous vous réjouissez en des choses de néant, [et] vous dites: Ne nous sommes-nous pas acquis de l'élévation par notre force?
14 Maana Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote asema, “Nitainua taifa dhidi yenu, ee nyumba ya Israeli, nalo litawatesa kuanzia Lebo-Hamathi hadi Bonde la Araba.”
Mais, ô maison d'Israël! voici, j'élèverai contre vous une nation, dit l'Eternel le Dieu des armées, laquelle vous opprimera depuis l'entrée de Hamath jusqu'au torrent du désert.

< Amosi 6 >