< Amosi 6 >
1 Ole wenu ninyi mnaostarehe na kuridhika katika Sayuni, na ninyi mnaojisikia salama juu ya Mlima Samaria, ninyi watu mashuhuri wa taifa lililoendelea kuliko mataifa mengine, ambao watu wa Israeli wanawategemea!
Malheur à vous, qui vous croyez en sécurité à Sion, et à vous, si pleins de quiétude sur le mont de Samarie, qui formez l’élite de la première des nations et attirez à vous la maison d’Israël!
2 Nendeni Kalne mkaone kutoka huko; mwende hadi Hamathi iliyo kuu, kisha mshuke hadi Gathi ya Wafilisti. Je, wao ni bora kuliko falme zenu mbili? Je, nchi yao ni kubwa kuliko yenu?
Passez donc à Calné et regardez; de là, rendez-vous à Hamath-la-Grande, puis descendez à Gath au pays des Philistins: sont-ils plus prospères que ces royaumes-ci, leur territoire est-il plus considérable que le vôtre?
3 Mnaiweka mbali siku iliyo mbaya na kuleta karibu utawala wa kuogofya.
Vous vous imaginez reculer le jour du malheur et vous avancez le règne de la violence!
4 Ninyi mnalala juu ya vitanda vilivyofunikwa kwa pembe za ndovu, na kujinyoosha juu ya viti vya fahari. Mnajilisha kwa wana-kondoo wazuri na ndama walionenepeshwa.
Couchés sur des lits d’ivoire, étendus sur leurs divans, nourris d’agneaux choisis dans le troupeau, de veaux mis à l’engrais,
5 Ninyi mnapiga vinubi kama Daudi, huku mkitunga nyimbo za vinanda mbalimbali.
fredonnant au son du luth, comme David inventant à leur usage des instruments de musique,
6 Mnakunywa mvinyo kwa bakuli zilizojazwa, na mnajipaka mafuta mazuri, lakini hamhuzuniki kwa maangamizi ya Yosefu.
ils boivent du vin à même les amphores, se frottent d’huiles de choix et ne s’affligent guère du désastre de Joseph!
7 Kwa hiyo mtakuwa miongoni mwa watu wa kwanza kwenda uhamishoni; karamu zenu na kustarehe kutakoma.
C’Est pourquoi, tantôt, ils s’en iront en tête des déportés; alors c’en sera fini des chants bruyants de ces voluptueux.
8 Bwana Mwenyezi ameapa kwa nafsi yake mwenyewe: Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote asema: “Nachukia kiburi cha Yakobo, nachukia ngome zake; nitautoa mji wao na kila kitu kilichomo ndani mwake.”
"Le Seigneur a juré par lui-même, c’est la parole de l’Eternel Dieu-Cebaot: Je déteste l’orgueil de Jacob, je hais ses palais, je livrerai donc en proie la ville et ce qu’elle renferme.
9 Kama watu kumi watabaki katika nyumba moja, wao pia watakufa.
Que s’il reste dix hommes dans une maison, ils mourront.
10 Kama jamaa ambaye atachoma miili akija ili kuitoa nje ya nyumba, na kumuuliza yeyote ambaye bado anajificha humo, “Je, yuko mtu yeyote pamoja nawe?” Naye akisema, “Hapana,” ndipo atakaposema, “Nyamaza kimya! Haturuhusiwi kutaja jina la Bwana.”
Et quand le proche parent, chargé de l’incinération, emportera le corps afin de débarrasser la maison des ossements, il demandera à celui qui se trouve au fond de l’appartement: "Y a-t-il encore quelqu’un?", et l’autre répondra: "Non, personne!" et ajoutera: "Silence!" car ce ne sera pas le moment de prononcer le nom de l’Eternel."
11 Kwa kuwa Bwana ameamuru, naye atabomoa jumba kubwa vipande vipande na nyumba ndogo vipande vidogo vidogo.
En vérité, l’Eternel donne des ordres: il fera tomber en ruines les grandes maisons et mettra en morceaux les petites.
12 Je, farasi waweza kukimbia kwenye miamba mikali? Je, aweza mtu kulima huko kwa maksai? Lakini mmegeuza haki kuwa sumu na matunda ya uadilifu kuwa uchungu:
Est-ce que les chevaux courent sur le roc? Le laboure-t-on avec des bœufs? Mais vous, vous avez changé le bon droit en poison, et l’œuvre de la justice en plante vénéneuse.
13 ninyi mnaoshangilia kushindwa kwa Lo-Debari na kusema, “Je, hatukuteka Karnaimu kwa nguvu zetu wenyewe?”
Vous trouvez votre joie dans ce qui est néant, vous dites: "N’Est-ce pas grâce à notre énergie que nous avons conquis la puissance?"
14 Maana Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote asema, “Nitainua taifa dhidi yenu, ee nyumba ya Israeli, nalo litawatesa kuanzia Lebo-Hamathi hadi Bonde la Araba.”
Eh bien! Me voici, suscitant contre vous, maison d’Israël, dit l’Eternel, Dieu-Cebaot, un peuple qui vous serrera de près dès la région de Hamath jusqu’au torrent de la Plaine.