< Amosi 6 >

1 Ole wenu ninyi mnaostarehe na kuridhika katika Sayuni, na ninyi mnaojisikia salama juu ya Mlima Samaria, ninyi watu mashuhuri wa taifa lililoendelea kuliko mataifa mengine, ambao watu wa Israeli wanawategemea!
Malheur à ceux qui vivent tranquilles dans Sion, et en sécurité sur la montagne de Samarie, les plus nobles du premier des peuples, auprès desquels va la maison d'Israël!
2 Nendeni Kalne mkaone kutoka huko; mwende hadi Hamathi iliyo kuu, kisha mshuke hadi Gathi ya Wafilisti. Je, wao ni bora kuliko falme zenu mbili? Je, nchi yao ni kubwa kuliko yenu?
Passez à Calné et voyez; allez de là à Hamath la grande; descendez à Geth des Philistins; Ces villes sont-elles plus prospères que ces royaumes, et leur territoire est-il plus étendu que le vôtre?
3 Mnaiweka mbali siku iliyo mbaya na kuleta karibu utawala wa kuogofya.
Vous éloignez le jour du malheur, et vous faites approcher le règne de la violence!
4 Ninyi mnalala juu ya vitanda vilivyofunikwa kwa pembe za ndovu, na kujinyoosha juu ya viti vya fahari. Mnajilisha kwa wana-kondoo wazuri na ndama walionenepeshwa.
Ils sont couchés sur des lits d'ivoire, et s'étendent sur leurs divans; ils mangent les agneaux du troupeau, et les veaux engraissés dans l'étable.
5 Ninyi mnapiga vinubi kama Daudi, huku mkitunga nyimbo za vinanda mbalimbali.
Ils folâtrent au son de la harpe; comme David, ils ont inventé des instruments de musique.
6 Mnakunywa mvinyo kwa bakuli zilizojazwa, na mnajipaka mafuta mazuri, lakini hamhuzuniki kwa maangamizi ya Yosefu.
Ils boivent le vin dans de larges coupes, ils se parfument avec les huiles les plus exquises. Et ils ne sont pas malades de la plaie de Joseph.
7 Kwa hiyo mtakuwa miongoni mwa watu wa kwanza kwenda uhamishoni; karamu zenu na kustarehe kutakoma.
C'est pourquoi ils iront en exil, à la tête des captifs, et les cris de joie des voluptueux disparaîtront.
8 Bwana Mwenyezi ameapa kwa nafsi yake mwenyewe: Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote asema: “Nachukia kiburi cha Yakobo, nachukia ngome zake; nitautoa mji wao na kila kitu kilichomo ndani mwake.”
Le Seigneur Yahweh l'a juré par lui-même, — oracle de Yahweh, le Dieu des armées: J'ai en abomination l'orgueil de Jacob, et je hais ses palais; je livrerai la ville et ce qu'elle renferme.
9 Kama watu kumi watabaki katika nyumba moja, wao pia watakufa.
Et s'il reste dix hommes dans une seule maison, ils mourront.
10 Kama jamaa ambaye atachoma miili akija ili kuitoa nje ya nyumba, na kumuuliza yeyote ambaye bado anajificha humo, “Je, yuko mtu yeyote pamoja nawe?” Naye akisema, “Hapana,” ndipo atakaposema, “Nyamaza kimya! Haturuhusiwi kutaja jina la Bwana.”
Un parent avec celui qui brûle les cadavres enlèvera le mort, et emportera de la maison les ossements; et l'un dira à celui qui est au fond de la maison: " Y en a-t-il encore avec toi? " Il répondra: " Plus personne! " Et le premier dira: " Silence! " Car il ne faut pas prononcer le nom de Yahweh.
11 Kwa kuwa Bwana ameamuru, naye atabomoa jumba kubwa vipande vipande na nyumba ndogo vipande vidogo vidogo.
Car voici que Yahweh commande, et il fait tomber en ruines la grande maison, et en débris la petite maison.
12 Je, farasi waweza kukimbia kwenye miamba mikali? Je, aweza mtu kulima huko kwa maksai? Lakini mmegeuza haki kuwa sumu na matunda ya uadilifu kuwa uchungu:
Les chevaux courent-ils sur le rocher, où y laboure-t-on avec des bœufs, que vous avez changé le droit en poison, et le fruit de la justice en absinthe?
13 ninyi mnaoshangilia kushindwa kwa Lo-Debari na kusema, “Je, hatukuteka Karnaimu kwa nguvu zetu wenyewe?”
Vous vous réjouissez de ce qui n'est rien, vous dites: " N'est-ce pas par notre force que nous avons acquis de la puissance? "
14 Maana Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote asema, “Nitainua taifa dhidi yenu, ee nyumba ya Israeli, nalo litawatesa kuanzia Lebo-Hamathi hadi Bonde la Araba.”
Car voici que je suscite contre vous, maison d'Israël, — oracle de Yahweh, le Dieu des armées! — une nation qui vous opprimera depuis l'entrée de Hamath jusqu'au torrent du désert.

< Amosi 6 >