< Amosi 6 >

1 Ole wenu ninyi mnaostarehe na kuridhika katika Sayuni, na ninyi mnaojisikia salama juu ya Mlima Samaria, ninyi watu mashuhuri wa taifa lililoendelea kuliko mataifa mengine, ambao watu wa Israeli wanawategemea!
Malheur à ceux qui sont à l'aise dans Sion, et à ceux qui sont en sécurité sur la montagne de Samarie, les hommes remarquables du chef des nations, vers qui la maison d'Israël vient!
2 Nendeni Kalne mkaone kutoka huko; mwende hadi Hamathi iliyo kuu, kisha mshuke hadi Gathi ya Wafilisti. Je, wao ni bora kuliko falme zenu mbili? Je, nchi yao ni kubwa kuliko yenu?
Va à Calneh, et regarde. De là, allez à Hamath la grande. Puis descends à Gath des Philistins. Sont-ils meilleurs que ces royaumes? Leur frontière est-elle plus grande que la vôtre?
3 Mnaiweka mbali siku iliyo mbaya na kuleta karibu utawala wa kuogofya.
Hélas pour vous qui repoussez loin le jour mauvais, et faire en sorte que le siège de la violence s'approche,
4 Ninyi mnalala juu ya vitanda vilivyofunikwa kwa pembe za ndovu, na kujinyoosha juu ya viti vya fahari. Mnajilisha kwa wana-kondoo wazuri na ndama walionenepeshwa.
qui reposent sur des lits d'ivoire, et s'étirent sur leur canapé, et manger les agneaux du troupeau, et les veaux au milieu de la stalle,
5 Ninyi mnapiga vinubi kama Daudi, huku mkitunga nyimbo za vinanda mbalimbali.
qui grattent les cordes d'une harpe, qui s'inventent des instruments de musique, comme David;
6 Mnakunywa mvinyo kwa bakuli zilizojazwa, na mnajipaka mafuta mazuri, lakini hamhuzuniki kwa maangamizi ya Yosefu.
qui boivent du vin dans des bols, et s'oignent avec les meilleures huiles, mais ils ne sont pas affligés par l'affliction de Joseph.
7 Kwa hiyo mtakuwa miongoni mwa watu wa kwanza kwenda uhamishoni; karamu zenu na kustarehe kutakoma.
C'est pourquoi ils iront maintenant en captivité avec les premiers qui iront en captivité. Le festin et le farniente prendront fin.
8 Bwana Mwenyezi ameapa kwa nafsi yake mwenyewe: Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote asema: “Nachukia kiburi cha Yakobo, nachukia ngome zake; nitautoa mji wao na kila kitu kilichomo ndani mwake.”
« Le Seigneur Yahvé l'a juré par lui-même », dit Yahvé, le Dieu des armées: « Je déteste l'orgueil de Jacob, et détester ses forteresses. C'est pourquoi je livrerai la ville et tout ce qu'elle contient.
9 Kama watu kumi watabaki katika nyumba moja, wao pia watakufa.
Il arrivera que si dix hommes restent dans une maison, ils mourront.
10 Kama jamaa ambaye atachoma miili akija ili kuitoa nje ya nyumba, na kumuuliza yeyote ambaye bado anajificha humo, “Je, yuko mtu yeyote pamoja nawe?” Naye akisema, “Hapana,” ndipo atakaposema, “Nyamaza kimya! Haturuhusiwi kutaja jina la Bwana.”
« Lorsque le parent d'un homme le porte, même celui qui le brûle, pour faire sortir des cadavres de la maison, et qu'il demande à celui qui est dans les entrailles de la maison: 'Y a-t-il encore quelqu'un avec toi?'. Et qu'il répond: 'Non', alors il dira: 'Chut! En effet, nous ne devons pas mentionner le nom de Yahvé.'
11 Kwa kuwa Bwana ameamuru, naye atabomoa jumba kubwa vipande vipande na nyumba ndogo vipande vidogo vidogo.
« Car voici que Yahvé ordonne, et la grande maison sera réduite en miettes, et la petite maison en morceaux.
12 Je, farasi waweza kukimbia kwenye miamba mikali? Je, aweza mtu kulima huko kwa maksai? Lakini mmegeuza haki kuwa sumu na matunda ya uadilifu kuwa uchungu:
Les chevaux courent-ils sur les rochers? Est-ce qu'on y laboure avec des bœufs? Mais vous avez transformé la justice en poison, et le fruit de la justice en amertume,
13 ninyi mnaoshangilia kushindwa kwa Lo-Debari na kusema, “Je, hatukuteka Karnaimu kwa nguvu zetu wenyewe?”
vous qui vous réjouissez d'une chose de rien, qui dites, « N'avons-nous pas pris pour nous-mêmes des cornes par notre propre force?
14 Maana Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote asema, “Nitainua taifa dhidi yenu, ee nyumba ya Israeli, nalo litawatesa kuanzia Lebo-Hamathi hadi Bonde la Araba.”
Car voici que je vais susciter contre vous une nation, la maison d'Israël ». dit Yahvé, le Dieu des Armées; « et ils te feront souffrir depuis l'entrée de Hamath jusqu'au ruisseau de la plaine. »

< Amosi 6 >