< Amosi 6 >

1 Ole wenu ninyi mnaostarehe na kuridhika katika Sayuni, na ninyi mnaojisikia salama juu ya Mlima Samaria, ninyi watu mashuhuri wa taifa lililoendelea kuliko mataifa mengine, ambao watu wa Israeli wanawategemea!
Wo to you, that ben ful of richessis in Sion, and tristen in the hil of Samarie, ye principal men, the heedis of puplis, that goen proudli in to the hous of Israel.
2 Nendeni Kalne mkaone kutoka huko; mwende hadi Hamathi iliyo kuu, kisha mshuke hadi Gathi ya Wafilisti. Je, wao ni bora kuliko falme zenu mbili? Je, nchi yao ni kubwa kuliko yenu?
Go ye in to Calamye, and se ye, and go ye fro thennus in to Emath the greet; and go ye doun in to Geth of Palestyns, and to alle the beste rewmes of hem, if her terme be broddere than youre terme.
3 Mnaiweka mbali siku iliyo mbaya na kuleta karibu utawala wa kuogofya.
And ye ben departid in to yuel dai, and neiyen to the seete of wickidnesse;
4 Ninyi mnalala juu ya vitanda vilivyofunikwa kwa pembe za ndovu, na kujinyoosha juu ya viti vya fahari. Mnajilisha kwa wana-kondoo wazuri na ndama walionenepeshwa.
and ye slepen in beddis of yuer, and doen letcherie in youre beddis; and ye eten a lomb of the flok, and calues of the myddil of droue;
5 Ninyi mnapiga vinubi kama Daudi, huku mkitunga nyimbo za vinanda mbalimbali.
and ye syngen at vois of sautree. As Dauid thei gessiden hem for to haue instrumentis of song, and drynken wyn in viols;
6 Mnakunywa mvinyo kwa bakuli zilizojazwa, na mnajipaka mafuta mazuri, lakini hamhuzuniki kwa maangamizi ya Yosefu.
and with beste oynement thei weren anoynted; and in no thing thei hadden compassioun on the sorewe, ether defoulyng, of Joseph.
7 Kwa hiyo mtakuwa miongoni mwa watu wa kwanza kwenda uhamishoni; karamu zenu na kustarehe kutakoma.
Wherfor now thei schulen passe in the heed of men passynge ouer, and the doyng of men doynge letcherie schal be don awei.
8 Bwana Mwenyezi ameapa kwa nafsi yake mwenyewe: Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote asema: “Nachukia kiburi cha Yakobo, nachukia ngome zake; nitautoa mji wao na kila kitu kilichomo ndani mwake.”
The Lord God swoor in his soule, seith the Lord God of oostis, Y wlate the pride of Jacob, and Y hate the housis of hym, and Y schal bitake the citee with hise dwelleris;
9 Kama watu kumi watabaki katika nyumba moja, wao pia watakufa.
that if ten men ben left in oon hous, and thei schulen die.
10 Kama jamaa ambaye atachoma miili akija ili kuitoa nje ya nyumba, na kumuuliza yeyote ambaye bado anajificha humo, “Je, yuko mtu yeyote pamoja nawe?” Naye akisema, “Hapana,” ndipo atakaposema, “Nyamaza kimya! Haturuhusiwi kutaja jina la Bwana.”
And his neiybore schal take hym, and schal brenne hym, that he bere out boonys of the hous. And he schal seie to hym, that is in the priuy places of the hous, Whether ther is yit anentis thee? And he schal answer, An ende is. And he schal seie to hym, Be thou stille, and thenke thou not on the name of the Lord.
11 Kwa kuwa Bwana ameamuru, naye atabomoa jumba kubwa vipande vipande na nyumba ndogo vipande vidogo vidogo.
For lo! the Lord schal comaunde, and schal smyte the grettere hous with fallyngis, and the lesse hous with brekyngis.
12 Je, farasi waweza kukimbia kwenye miamba mikali? Je, aweza mtu kulima huko kwa maksai? Lakini mmegeuza haki kuwa sumu na matunda ya uadilifu kuwa uchungu:
Whether horsis moun renne in stoonys, ether it mai be eerid with wielde oxun? For ye turneden doom in to bitternesse, and the fruyt of riytfulnesse in to wermod.
13 ninyi mnaoshangilia kushindwa kwa Lo-Debari na kusema, “Je, hatukuteka Karnaimu kwa nguvu zetu wenyewe?”
And ye ben glad in nouyt, and ye seien, Whether not in oure strengthe we token to vs hornes?
14 Maana Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote asema, “Nitainua taifa dhidi yenu, ee nyumba ya Israeli, nalo litawatesa kuanzia Lebo-Hamathi hadi Bonde la Araba.”
Lo! Y schal reise on you, the hous of Israel, seith the Lord God of oostis, a folc; and it schal al to-breke you fro entre of Emath `til to the streem of desert.

< Amosi 6 >