< Amosi 6 >

1 Ole wenu ninyi mnaostarehe na kuridhika katika Sayuni, na ninyi mnaojisikia salama juu ya Mlima Samaria, ninyi watu mashuhuri wa taifa lililoendelea kuliko mataifa mengine, ambao watu wa Israeli wanawategemea!
Sorrow awaits who are carefree in Zion, overconfident on the mountain of Samaria! The elite of this, the best of nations, on whom the people of Israel rest their hopes!
2 Nendeni Kalne mkaone kutoka huko; mwende hadi Hamathi iliyo kuu, kisha mshuke hadi Gathi ya Wafilisti. Je, wao ni bora kuliko falme zenu mbili? Je, nchi yao ni kubwa kuliko yenu?
You say to the people: Cross over to Calneh and see, go from there to Hamath the great, then go down to Gath of the Philistines: Are they better than these kingdoms? Is their territory larger than yours?
3 Mnaiweka mbali siku iliyo mbaya na kuleta karibu utawala wa kuogofya.
You push away all thoughts of the evil day, yet have instituted a rule of violence.
4 Ninyi mnalala juu ya vitanda vilivyofunikwa kwa pembe za ndovu, na kujinyoosha juu ya viti vya fahari. Mnajilisha kwa wana-kondoo wazuri na ndama walionenepeshwa.
They lie on ivory couches, sprawl on their divans, eat choice lambs from the flock, and fattened calves from the stall.
5 Ninyi mnapiga vinubi kama Daudi, huku mkitunga nyimbo za vinanda mbalimbali.
They idly sing to the sound of the lyre, thinking themselves songwriters like David,
6 Mnakunywa mvinyo kwa bakuli zilizojazwa, na mnajipaka mafuta mazuri, lakini hamhuzuniki kwa maangamizi ya Yosefu.
they drink bowlfuls of wine, and anoint themselves with the finest of oil. But they do not grieve over the ruin of Joseph.
7 Kwa hiyo mtakuwa miongoni mwa watu wa kwanza kwenda uhamishoni; karamu zenu na kustarehe kutakoma.
Therefore now they must go into exile at the head of the captives, and hushed will be the revelry of the sprawlers.
8 Bwana Mwenyezi ameapa kwa nafsi yake mwenyewe: Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote asema: “Nachukia kiburi cha Yakobo, nachukia ngome zake; nitautoa mji wao na kila kitu kilichomo ndani mwake.”
The Lord God, the Lord, the God of hosts, has sworn by himself: I abhor the pride of Jacob, I hate his palaces, therefore I will deliver up the city and all that is in it to their enemies.
9 Kama watu kumi watabaki katika nyumba moja, wao pia watakufa.
If ten people remain in one house, then they will die.
10 Kama jamaa ambaye atachoma miili akija ili kuitoa nje ya nyumba, na kumuuliza yeyote ambaye bado anajificha humo, “Je, yuko mtu yeyote pamoja nawe?” Naye akisema, “Hapana,” ndipo atakaposema, “Nyamaza kimya! Haturuhusiwi kutaja jina la Bwana.”
When the uncle and another member of the family of a dead man come to carry the body out of the house for burial, they will call to someone in a corner of the house, ‘Any more there?’ and he will answer, ‘No’, and then he will add, ‘Be quiet!’ – for the name of the Lord must not be mentioned.
11 Kwa kuwa Bwana ameamuru, naye atabomoa jumba kubwa vipande vipande na nyumba ndogo vipande vidogo vidogo.
Look! The Lord is giving the command! He will smash the large house to bits, the small house into fragments.
12 Je, farasi waweza kukimbia kwenye miamba mikali? Je, aweza mtu kulima huko kwa maksai? Lakini mmegeuza haki kuwa sumu na matunda ya uadilifu kuwa uchungu:
Do horses gallop on crags? Does one plow the sea with oxen? Yet you turn justice into poison weed, and the fruit of righteousness into bitter wormwood.
13 ninyi mnaoshangilia kushindwa kwa Lo-Debari na kusema, “Je, hatukuteka Karnaimu kwa nguvu zetu wenyewe?”
You who are so proud of capturing Lo-debar, who say, ‘Have we not by our own strength taken Karnaim for ourselves?’
14 Maana Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote asema, “Nitainua taifa dhidi yenu, ee nyumba ya Israeli, nalo litawatesa kuanzia Lebo-Hamathi hadi Bonde la Araba.”
I am now raising up against you, Israel, a nation, says the Lord, the God of hosts. They will oppress you, from the entrance of Hamath to the brook of the Arabah.

< Amosi 6 >