< Amosi 6 >
1 Ole wenu ninyi mnaostarehe na kuridhika katika Sayuni, na ninyi mnaojisikia salama juu ya Mlima Samaria, ninyi watu mashuhuri wa taifa lililoendelea kuliko mataifa mengine, ambao watu wa Israeli wanawategemea!
Woe to them that dwell at ease in Zion; That feel secure upon the mountain of Samaria; The honorable men of the chief of the nations, To whom the house of Israel resort!
2 Nendeni Kalne mkaone kutoka huko; mwende hadi Hamathi iliyo kuu, kisha mshuke hadi Gathi ya Wafilisti. Je, wao ni bora kuliko falme zenu mbili? Je, nchi yao ni kubwa kuliko yenu?
Pass over to Calneh, and see; And thence go to great Hamath; Then go down to Gath of the Philistines: Are they better than these kingdoms, Or is their border greater than your border?
3 Mnaiweka mbali siku iliyo mbaya na kuleta karibu utawala wa kuogofya.
Woe to them, that put far away the day of evil, And bring near the seat of oppression;
4 Ninyi mnalala juu ya vitanda vilivyofunikwa kwa pembe za ndovu, na kujinyoosha juu ya viti vya fahari. Mnajilisha kwa wana-kondoo wazuri na ndama walionenepeshwa.
That lie upon beds of ivory, And stretch themselves upon their couches; That eat lambs from the flock, And calves from the stall;
5 Ninyi mnapiga vinubi kama Daudi, huku mkitunga nyimbo za vinanda mbalimbali.
That chant to the sound of the harp, And invent for themselves instruments of music, like David;
6 Mnakunywa mvinyo kwa bakuli zilizojazwa, na mnajipaka mafuta mazuri, lakini hamhuzuniki kwa maangamizi ya Yosefu.
That drink wine in bowls, And anoint themselves with the most precious perfumes, But grieve not for the destruction of Joseph!
7 Kwa hiyo mtakuwa miongoni mwa watu wa kwanza kwenda uhamishoni; karamu zenu na kustarehe kutakoma.
Therefore now shall they go captive at the head of the captives; Yea, the shouting of them that stretch themselves upon their couches shall cease.
8 Bwana Mwenyezi ameapa kwa nafsi yake mwenyewe: Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote asema: “Nachukia kiburi cha Yakobo, nachukia ngome zake; nitautoa mji wao na kila kitu kilichomo ndani mwake.”
The Lord Jehovah hath sworn by himself, Thus saith Jehovah, the God of hosts: I abhor the pride of Jacob, And I hate his palaces; I will give up the city, and all that is therein.
9 Kama watu kumi watabaki katika nyumba moja, wao pia watakufa.
And if ten men remain in one house, These also shall die.
10 Kama jamaa ambaye atachoma miili akija ili kuitoa nje ya nyumba, na kumuuliza yeyote ambaye bado anajificha humo, “Je, yuko mtu yeyote pamoja nawe?” Naye akisema, “Hapana,” ndipo atakaposema, “Nyamaza kimya! Haturuhusiwi kutaja jina la Bwana.”
A man's relative, or a burner of the dead, shall take him up, To carry his bones out of the house, And he shall say to him that is in the innermost part of the house, Is there yet any one with thee? And he shall answer, No one! Then shall he say, Keep silence! For we may not make mention of the name of Jehovah.
11 Kwa kuwa Bwana ameamuru, naye atabomoa jumba kubwa vipande vipande na nyumba ndogo vipande vidogo vidogo.
For behold Jehovah hath commanded, And he will smite the great house with breaches, And the small house with clefts.
12 Je, farasi waweza kukimbia kwenye miamba mikali? Je, aweza mtu kulima huko kwa maksai? Lakini mmegeuza haki kuwa sumu na matunda ya uadilifu kuwa uchungu:
Shall horses run upon rocks, Or will one plough rocks with oxen, That ye change justice into hemlock, And the fruit of equity into wormwood,
13 ninyi mnaoshangilia kushindwa kwa Lo-Debari na kusema, “Je, hatukuteka Karnaimu kwa nguvu zetu wenyewe?”
Ye that rejoice in a thing of naught, And say, Have we not acquired dominion by our own strength?
14 Maana Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote asema, “Nitainua taifa dhidi yenu, ee nyumba ya Israeli, nalo litawatesa kuanzia Lebo-Hamathi hadi Bonde la Araba.”
Behold, O house of Israel, saith Jehovah, the God of hosts, I will raise against you a nation, That shall oppress you from Hamath Even to the brook of the desert.