< Amosi 6 >
1 Ole wenu ninyi mnaostarehe na kuridhika katika Sayuni, na ninyi mnaojisikia salama juu ya Mlima Samaria, ninyi watu mashuhuri wa taifa lililoendelea kuliko mataifa mengine, ambao watu wa Israeli wanawategemea!
Woe to those who are at ease in Zion, and to those who are secure in the mountain of Samaria, the notable men of the chief of the nations, to whom the house of Israel come!
2 Nendeni Kalne mkaone kutoka huko; mwende hadi Hamathi iliyo kuu, kisha mshuke hadi Gathi ya Wafilisti. Je, wao ni bora kuliko falme zenu mbili? Je, nchi yao ni kubwa kuliko yenu?
Pass ye to Calneh, and see, and from there go ye to Hamath the great, then go down to Gath of the Philistines. Are they better than these kingdoms? Or is their border greater than your border?
3 Mnaiweka mbali siku iliyo mbaya na kuleta karibu utawala wa kuogofya.
Ye who put far away the evil day, and cause the seat of violence to come near,
4 Ninyi mnalala juu ya vitanda vilivyofunikwa kwa pembe za ndovu, na kujinyoosha juu ya viti vya fahari. Mnajilisha kwa wana-kondoo wazuri na ndama walionenepeshwa.
who lie upon beds of ivory, and stretch themselves upon their couches, and eat the lambs out of the flock, and the calves out of the midst of the stall,
5 Ninyi mnapiga vinubi kama Daudi, huku mkitunga nyimbo za vinanda mbalimbali.
who sing idle songs to the sound of the viol, who invent for themselves instruments of music, like David,
6 Mnakunywa mvinyo kwa bakuli zilizojazwa, na mnajipaka mafuta mazuri, lakini hamhuzuniki kwa maangamizi ya Yosefu.
who drink wine in bowls, and anoint themselves with the chief oils, but they are not grieved for the affliction of Joseph.
7 Kwa hiyo mtakuwa miongoni mwa watu wa kwanza kwenda uhamishoni; karamu zenu na kustarehe kutakoma.
Therefore they shall now go captive with the first who go captive, and the revelry of those who stretched themselves shall pass away.
8 Bwana Mwenyezi ameapa kwa nafsi yake mwenyewe: Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote asema: “Nachukia kiburi cha Yakobo, nachukia ngome zake; nitautoa mji wao na kila kitu kilichomo ndani mwake.”
The lord Jehovah has sworn by himself, says Jehovah, the God of hosts: I abhor the excellency of Jacob, and hate his palaces, therefore I will deliver up the city with all that is therein.
9 Kama watu kumi watabaki katika nyumba moja, wao pia watakufa.
And it shall come to pass, if there remain ten men in one house, that they shall die.
10 Kama jamaa ambaye atachoma miili akija ili kuitoa nje ya nyumba, na kumuuliza yeyote ambaye bado anajificha humo, “Je, yuko mtu yeyote pamoja nawe?” Naye akisema, “Hapana,” ndipo atakaposema, “Nyamaza kimya! Haturuhusiwi kutaja jina la Bwana.”
And when a man's uncle shall take him up, even he who burns him, to bring out the bones out of the house, and shall say to him who is in the innermost parts of the house, Is there yet any with thee? and he shall say, No, then he shall say, Hold thy peace, for we may not make mention of the name of Jehovah.
11 Kwa kuwa Bwana ameamuru, naye atabomoa jumba kubwa vipande vipande na nyumba ndogo vipande vidogo vidogo.
For, behold, Jehovah commands, and the great house shall be smitten with breaches, and the little house with clefts.
12 Je, farasi waweza kukimbia kwenye miamba mikali? Je, aweza mtu kulima huko kwa maksai? Lakini mmegeuza haki kuwa sumu na matunda ya uadilifu kuwa uchungu:
Shall horses run upon the rock? Will a man plow there with oxen? That ye have turned justice into gall, and the fruit of righteousness into wormwood,
13 ninyi mnaoshangilia kushindwa kwa Lo-Debari na kusema, “Je, hatukuteka Karnaimu kwa nguvu zetu wenyewe?”
ye who rejoice in a thing of nothing, who say, Have we not taken to us horns by our own strength?
14 Maana Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote asema, “Nitainua taifa dhidi yenu, ee nyumba ya Israeli, nalo litawatesa kuanzia Lebo-Hamathi hadi Bonde la Araba.”
For, behold, I will raise up against you a nation, O house of Israel, says Jehovah, the God of hosts, and they shall afflict you from the entrance of Hamath to the brook of the Arabah.