< Amosi 4 >

1 Sikilizeni neno hili, ninyi ngʼombe wa Bashani mlioko juu ya Mlima Samaria, ninyi wanawake mnaowaonea maskini, na kuwagandamiza wahitaji, na kuwaambia wanaume wenu, “Tuleteeni vinywaji!”
Hear this word, ye cows of Bashan, who are in the mountain of Samaria, who oppress the poor, who crush the needy, who say to their lords, Bring, and let us drink.
2 Bwana Mwenyezi ameapa kwa utakatifu wake: “Hakika wakati utakuja mtakapochukuliwa na kulabu, na wanaosalia kwa ndoana za samaki.
The lord Jehovah has sworn by his holiness, that, lo, the days shall come upon you, that they shall take you away with hooks, and your residue with fish-hooks.
3 Nanyi mtakwenda moja kwa moja kupitia mahali palipobomolewa kwenye ukuta, nanyi mtatupwa nje kuelekea Harmoni,” asema Bwana.
And ye shall go out at the breaches, each one straight before her, and ye shall cast yourselves into Harmon, says Jehovah.
4 “Nendeni Betheli mkatende dhambi; nendeni Gilgali mkazidi kutenda dhambi. Leteni dhabihu zenu kila asubuhi, zaka zenu kila mwaka wa tatu.
Come to Bethel and transgress, to Gilgal and multiply transgression. And bring your sacrifices every morning, and your tithes every three days.
5 Mchome mkate uliotiwa chachu kama sadaka ya shukrani, jisifuni kuhusu sadaka zenu za hiari: jigambeni kwa ajili ya sadaka hizo, enyi Waisraeli, kwa kuwa hili ndilo mnalopenda kulitenda,” asema Bwana Mwenyezi.
And offer a sacrifice of thanksgiving of that which is leavened, and proclaim freewill offerings, and publish them. For this pleases you, O ye sons of Israel, says the lord Jehovah.
6 “Niliwapa njaa kwenye kila mji, na ukosefu wa chakula katika kila mji, hata hivyo bado hamjanirudia mimi,” asema Bwana.
And I also have given you cleanness of teeth in all your cities, and want of bread in all your places, yet ye have not returned to me, says Jehovah.
7 “Pia niliwazuilia ninyi mvua miezi mitatu kabla ya kufikia mavuno. Nilinyesha mvua kwenye mji mmoja, lakini niliizuia mvua isinyeshe mji mwingine. Shamba moja lilipata mvua, na lingine halikupata, nalo likakauka.
And I also have withheld the rain from you, when there were yet three months to the harvest. And I caused it to rain upon one city, and caused it not to rain upon another city. One piece was rained upon, and the piece upon which it did not rain withered.
8 Watu walitangatanga mji hata mji kutafuta maji, lakini hawakupata ya kuwatosha kunywa, hata hivyo hamjanirudia mimi,” asema Bwana.
So two or three cities wandered to one city to drink water, and were not satisfied. Yet ye have not returned to me, says Jehovah.
9 “Mara nyingi nilizipiga bustani zenu na mashamba ya mizabibu, niliyapiga kwa kutu na ukungu. Nzige walitafuna tini zenu na miti ya mizeituni, hata hivyo hamjanirudia mimi,” asema Bwana.
I have smitten you with blasting and mildew. The multitude of your gardens and your vineyards and your fig trees and your olive trees the palmer-worm has devoured. Yet ye have not returned to me, says Jehovah.
10 “Niliwapelekea tauni miongoni mwenu kama nilivyofanya kule Misri. Niliwaua vijana wenu wa kiume kwa upanga, niliwachukua farasi wenu. Nilijaza pua zenu kwa uvundo kutoka kwenye kambi zenu, hata hivyo hamjanirudia mimi,” asema Bwana.
I have sent among you the pestilence according to the manner of Egypt. I have slain your young men with the sword, and have carried away your horses, and I have made the stench of your camp to come up even into your nostrils. Yet ye have not returned to me, says Jehovah.
11 “Niliwaangamiza baadhi yenu kama nilivyoangamiza Sodoma na Gomora. Mlikuwa kama kijiti kiwakacho kilichonyakuliwa motoni, hata hivyo hamjanirudia,” asema Bwana.
I have overthrown cities among you, as when God overthrew Sodom and Gomorrah, and ye were as a brand plucked out of the burning. Yet ye have not returned to me, says Jehovah.
12 “Kwa hiyo hili ndilo nitakalowafanyia, Israeli, na kwa sababu nitawafanyia hili, jiandaeni kukutana na Mungu wenu, ee Israeli.”
Therefore thus I will do to thee, O Israel, and because I will do this to thee, prepare to meet thy God, O Israel.
13 Yeye ambaye hufanya milima, anaumba upepo, na kufunua mawazo yake kwa mwanadamu, yeye ageuzaye asubuhi kuwa giza, na kukanyaga mahali pa juu pa nchi: Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake.
For, lo, he who forms the mountains, and creates the wind, and declares to man what is his thought, who makes the morning darkness, and treads upon the high places of the earth-Jehovah, the God of hosts, is his name.

< Amosi 4 >