< Amosi 3 >
1 Sikilizeni neno hili alilosema Bwana dhidi yenu, enyi watu wa Israeli, dhidi ya jamaa nzima niliowapandisha toka Misri:
Hør dette ord som Herren har talt mot eder, Israels barn, mot hele den ætt jeg har ført op fra Egyptens land:
2 “Ni ninyi tu niliowachagua kati ya jamaa zote za dunia; kwa hiyo nitawaadhibu kwa ajili ya dhambi zenu zote.”
Eder alene har jeg villet kjennes ved blandt alle jordens ætter; derfor vil jeg hjemsøke eder for alle eders misgjerninger.
3 Je, watu wawili hutembea pamoja wasipokubaliana kufanya hivyo?
Går vel to sammen uten at de har avtalt det med hverandre?
4 Je, simba hunguruma katika kichaka wakati hana mawindo? Aweza kuvuma katika pango wakati ambao hajakamata chochote?
Brøler vel løven i skogen uten at den har funnet noget rov? Lar vel ungløven sin røst høre fra sin hule uten at den har fanget noget?
5 Je, ndege aweza kuanguka kwenye mtego ulio ardhini ambapo hajategewa chambo? Je, mtego unaweza kufyatuka toka ardhini wakati ambapo hakuna chochote cha kunasa?
Faller vel fuglen i en snare på marken uten at det er satt nogen snare for den? Spretter vel snaren op fra marken uten at den fanger noget?
6 Je, tarumbeta inapopigwa mjini kujulisha hatari, watu hawatetemeki? Mji upatwapo na maafa, je, si Bwana amesababisha?
Eller støtes det vel i basun i en by uten at folket forferdes? Eller skjer det vel en ulykke i en by uten at Herren har gjort det?
7 Hakika Bwana Mwenyezi hatafanya neno lolote bila kuwafunulia watumishi wake manabii siri yake.
For Herren, Israels Gud, gjør ikke noget uten at han har åpenbaret sitt lønnlige råd for sine tjenere profetene.
8 Simba amenguruma: je, ni nani ambaye hataogopa? Bwana Mwenyezi ametamka: je, ni nani awezaye kukosa kutoa unabii?
Når løven brøler, hvem skulde ikke da reddes? Når Herren, Israels Gud, taler, hvem skulde ikke da profetere?
9 Tangazeni katika ngome za Ashdodi na katika ngome za Misri: “Kusanyikeni juu ya milima ya Samaria; angalieni wingi wa wasiwasi ulio ndani yake, na uonevu ulio miongoni mwa watu wake.”
Rop ut i palassene i Asdod og i palassene i Egyptens land og si: Samle eder på Samaria-fjellene og se hvor stor forvirring det er der inne, og hvor megen undertrykkelse der råder!
10 Bwana asema: “Hawajui kutenda lililo jema, wale ambao hujilundikia nyara na vitu vilivyotekwa katika ngome zao.”
De vet ikke å gjøre det som rett er, sier Herren, de som dynger op vold og ødeleggelse i sine palasser.
11 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: “Adui ataizingira nchi; ataangusha chini ngome zenu na kuteka nyara maboma yenu.”
Derfor sier Herren, Israels Gud, så: Fiender skal komme og omringe hele landet. Og de skal styrte ned din borg, så du mister ditt vern, og dine palasser skal bli plyndret.
12 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kama vile mchungaji aokoavyo kinywani mwa simba vipande viwili tu vya mfupa wa mguu au kipande cha sikio, hivyo ndivyo Waisraeli watakavyookolewa, wale wakaao Samaria kwenye kingo za vitanda vyao, na katika Dameski kwenye viti vyao vya fahari.”
Så sier Herren: Likesom en hyrde berger to leggeben eller en ørelapp av løvens gap, således skal Israels barn berges, de som sitter i Samaria i sofahjørnet og på damaskes hynder.
13 “Sikia hili na ushuhudie dhidi ya nyumba ya Yakobo,” asema Bwana, Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote.
Hør og vidne mot Jakobs hus, sier Herren, Israels Gud, hærskarenes Gud:
14 “Siku nitakapomwadhibu Israeli kwa sababu ya dhambi zake, nitaharibu madhabahu za Betheli; pembe za madhabahu zitakatiliwa mbali na kuanguka chini.
På den dag jeg hjemsøker Israel for dets misgjerninger, da vil jeg hjemsøke Betels altere, så alterhornene blir avhugget og faller til jorden,
15 Nitabomoa nyumba ya wakati wa masika, pamoja na nyumba ya wakati wa kiangazi; nyumba zilizonakshiwa kwa pembe za ndovu na majumba makubwa ya fahari yatabomolewa,” asema Bwana.
og jeg vil sønderslå både vinterhusene og sommerhusene, og elfenbenshusene skal gå til grunne, og mange hus rives bort, sier Herren.