< Amosi 3 >
1 Sikilizeni neno hili alilosema Bwana dhidi yenu, enyi watu wa Israeli, dhidi ya jamaa nzima niliowapandisha toka Misri:
Hear these words, which Jehovah speaketh against you, ye sons of Israel; Against the whole family which I brought up out of the land of Egypt!
2 “Ni ninyi tu niliowachagua kati ya jamaa zote za dunia; kwa hiyo nitawaadhibu kwa ajili ya dhambi zenu zote.”
You only have I known of all the families of the earth; Therefore will I punish you for all your iniquities.
3 Je, watu wawili hutembea pamoja wasipokubaliana kufanya hivyo?
Can two walk together, Unless they agree together?
4 Je, simba hunguruma katika kichaka wakati hana mawindo? Aweza kuvuma katika pango wakati ambao hajakamata chochote?
Will the lion roar in the forest, When he seeth no prey? Will the young lion cry aloud from his den, If he have seized nothing?
5 Je, ndege aweza kuanguka kwenye mtego ulio ardhini ambapo hajategewa chambo? Je, mtego unaweza kufyatuka toka ardhini wakati ambapo hakuna chochote cha kunasa?
Can a bird fall into a snare upon the earth, Where none is set for him? Will a snare spring up from the ground, When it hath caught nothing?
6 Je, tarumbeta inapopigwa mjini kujulisha hatari, watu hawatetemeki? Mji upatwapo na maafa, je, si Bwana amesababisha?
Shall a trumpet be blown in the city, And the people not be afraid? Shall there be evil upon a city, And Jehovah not have done it?
7 Hakika Bwana Mwenyezi hatafanya neno lolote bila kuwafunulia watumishi wake manabii siri yake.
Surely the Lord Jehovah doeth nothing, But he revealeth his secret To his servants the prophets.
8 Simba amenguruma: je, ni nani ambaye hataogopa? Bwana Mwenyezi ametamka: je, ni nani awezaye kukosa kutoa unabii?
When the lion roareth, who will not fear? When the Lord Jehovah speaketh, who will not prophesy?
9 Tangazeni katika ngome za Ashdodi na katika ngome za Misri: “Kusanyikeni juu ya milima ya Samaria; angalieni wingi wa wasiwasi ulio ndani yake, na uonevu ulio miongoni mwa watu wake.”
Proclaim ye, in the palaces in Ashdod, And in the palaces in the land of Egypt, And say, Assemble yourselves upon the mountains of Samaria; Behold the great tumults in the midst of her, And the oppressions within her!
10 Bwana asema: “Hawajui kutenda lililo jema, wale ambao hujilundikia nyara na vitu vilivyotekwa katika ngome zao.”
For they have no care to do right, saith Jehovah; They treasure up rapine and robbery in their palaces.
11 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: “Adui ataizingira nchi; ataangusha chini ngome zenu na kuteka nyara maboma yenu.”
Therefore thus saith the Lord Jehovah: An enemy shall encompass the land. And shall bring down thy strength from thee, And thy palaces shall be plundered.
12 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kama vile mchungaji aokoavyo kinywani mwa simba vipande viwili tu vya mfupa wa mguu au kipande cha sikio, hivyo ndivyo Waisraeli watakavyookolewa, wale wakaao Samaria kwenye kingo za vitanda vyao, na katika Dameski kwenye viti vyao vya fahari.”
Thus saith Jehovah: As the shepherd taketh out of the lion's mouth Two legs, or a portion of an ear, So shall the children of Israel be taken out, Who in Samaria sit in the corners of their sofas, And upon their damask couches.
13 “Sikia hili na ushuhudie dhidi ya nyumba ya Yakobo,” asema Bwana, Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote.
Hear ye, and testify to the house of Jacob, Saith the Lord, Jehovah, God of hosts!
14 “Siku nitakapomwadhibu Israeli kwa sababu ya dhambi zake, nitaharibu madhabahu za Betheli; pembe za madhabahu zitakatiliwa mbali na kuanguka chini.
In the day when I punish the transgressions of Israel, Then will I punish the altars of Bethel; The horns of the altar shall be cut off, And fall to the ground.
15 Nitabomoa nyumba ya wakati wa masika, pamoja na nyumba ya wakati wa kiangazi; nyumba zilizonakshiwa kwa pembe za ndovu na majumba makubwa ya fahari yatabomolewa,” asema Bwana.
and I will smite the winter-house together with the summer-house, And the houses of ivory shall be destroyed, And the great houses shall be brought to the ground, saith Jehovah.