< Amosi 2 >

1 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Moabu, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu alichoma mifupa ya mfalme wa Edomu, ikawa kama chokaa.
Сия глаголет Господь: за три нечестия Моавля и за четыри не отвращуся его, понеже сожгоша кости царя Идумейска в пепел:
2 Nitatuma moto juu ya Moabu ambao utateketeza ngome za Keriothi. Moabu ataanguka kwa ghasia kubwa katikati ya vilio vya vita na mlio wa tarumbeta.
и послю огнь на Моава, и пояст основания градов его, и умрет со безсилием Моав, с воплем и гласом трубным:
3 Nitamwangamiza mtawala wake na kuwaua maafisa wake wote pamoja naye,” asema Bwana.
и потреблю судию из него и вся князи его избию с ним, глаголет Господь.
4 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Yuda, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu wameikataa sheria ya Bwana na hawakuzishika amri zake, kwa sababu wamepotoshwa na miungu ya uongo, miungu ambayo babu zao waliifuata.
Сия глаголет Господь: за три нечестия сынов Иудиных и за четыри не отвращуся их, понеже отринуша закон Господень и повелений Его не сохраниша, и прельстиша их суетная их, яже сотвориша, имже последоваша отцы их вслед их:
5 Nitatuma moto juu ya Yuda ambao utateketeza ngome za Yerusalemu.”
и послю огнь на Иуду, и пояст основания Иерусалимля.
6 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Israeli, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Wanawauza wenye haki kwa fedha, na maskini kwa jozi ya viatu.
Сия глаголет Господь: за три нечестия Израиля и за четыри не отвращуся его, понеже продаша праведнаго на сребре и убогаго на сапозех,
7 Wanakanyaga juu ya vichwa vya maskini, kama vile juu ya mavumbi ya nchi, na kukataa haki kwa walioonewa. Baba na mwanawe hushiriki msichana mmoja, kwa hivyo hulinajisi Jina langu takatifu.
ходящих на прасе земнем, и бияху пястию во главы убогих, и путь смиренных совращаху: и сын и отец его влазяста ко единей рабыни, яко да осквернавят имя Бога своего:
8 Watu hulala kando ya kila madhabahu juu ya nguo zilizowekwa rehani. Katika nyumba ya mungu wao hunywa mvinyo ulionunuliwa kwa fedha walizotozwa watu.
и ризы своя связующе ужами, и завесы творяху держащыяся требища, и вино от оболганий пияху в дому бога своего.
9 “Nilimwangamiza Mwamori mbele yao, ingawa alikuwa mrefu kama mierezi, na mwenye nguvu kama mialoni. Niliyaangamiza matunda yake juu na mizizi yake chini.
Аз же отвергох Аморреа от лица их, егоже бе высота якоже высота кедрова, и крепок бяше якоже дуб, и изсуших плод его с верха и корение его из низу.
10 “Niliwapandisha toka Misri, na nikawaongoza miaka arobaini jangwani niwape nchi ya Waamori.
Аз же изведох вы из земли Египетския и обводих вы в пустыни четыредесять лет, еже прияти в наследие землю Аморрейску.
11 Pia niliinua manabii kutoka miongoni mwa wana wenu na Wanadhiri kutoka miongoni mwa vijana wenu. Je, hii si kweli, enyi watu wa Israeli?” asema Bwana.
И поях от сынов ваших во пророки и от юнот ваших во освящение: еда несть сих, сынове Израилевы? Глаголет Господь.
12 “Lakini mliwafanya Wanadhiri kunywa mvinyo na kuwaamuru manabii wasitoe unabii.
И напаясте освященныя вином и пророком заповедасте глаголюще: не прорицайте.
13 “Sasa basi, nitawaponda kama gari lipondavyo wakati limejazwa nafaka.
Сего ради, се, Аз повращу под вами, якоже вратится колесница полна тростия:
14 Mkimbiaji hodari hatanusurika, wenye nguvu wataishiwa nguvu zao, na shujaa hataweza kuokoa maisha yake.
и погибнет бегство от скоротекущаго, и крепкий не удержит крепости своея, и храбрый не спасет души своея,
15 Mpiga upinde atakimbia, askari wapiga mbio hawataweza kutoroka, na mpanda farasi hataokoa maisha yake.
и стреляяй из лука не постоит, и быстрый ногама своима не уцелеет, и конник не спасет души своея,
16 Hata askari walio mashujaa sana siku hiyo watakimbia uchi,” asema Bwana.
и крепкий не обрящет сердца своего в силах, наг побегнет в той день, глаголет Господь.

< Amosi 2 >