< Amosi 2 >

1 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Moabu, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu alichoma mifupa ya mfalme wa Edomu, ikawa kama chokaa.
Tak mówi Pan: Dla trzech występków Moaba, owszem, dla czterech, nie przepuszczę mu, przeto, iż spalił kości króla Edomskiego na popiół;
2 Nitatuma moto juu ya Moabu ambao utateketeza ngome za Keriothi. Moabu ataanguka kwa ghasia kubwa katikati ya vilio vya vita na mlio wa tarumbeta.
Ale poślę ogień na Moaba, który pożre pałace Karyjot; i umrze Moab w huku, w krzyku i w głosie trąby.
3 Nitamwangamiza mtawala wake na kuwaua maafisa wake wote pamoja naye,” asema Bwana.
I wygładzę sędziów z pośrodku jego, i wszystkich książąt jego pobiję z nim, mówi Pan.
4 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Yuda, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu wameikataa sheria ya Bwana na hawakuzishika amri zake, kwa sababu wamepotoshwa na miungu ya uongo, miungu ambayo babu zao waliifuata.
Tak mówi Pan: Dla trzech występków Judzkich, owszem, dla czterech, nie przepuszczę mu, przeto, że odrzucają zakon Pański, i ustaw jego nie przestrzegają, a dadzą się zwodzić kłamstwom swoim, których naśladowali ojcowie ich;
5 Nitatuma moto juu ya Yuda ambao utateketeza ngome za Yerusalemu.”
Ale poślę ogień na Judę, który pożre pałace Jeruzalemskie.
6 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Israeli, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Wanawauza wenye haki kwa fedha, na maskini kwa jozi ya viatu.
Tak mówi Pan: Dla trzech występków Izraelskich, owszem, dla czterech, nie przepuszczę mu, przeto, że sprawiedliwego za pieniądze sprzedawają, a ubogiego za parę trzewików;
7 Wanakanyaga juu ya vichwa vya maskini, kama vile juu ya mavumbi ya nchi, na kukataa haki kwa walioonewa. Baba na mwanawe hushiriki msichana mmoja, kwa hivyo hulinajisi Jina langu takatifu.
Którzy usiłują, aby na proch potarli głowy ubogich, a drogę pokornych podwracają; nadto syn i ojciec jego wchodzą do jednejże dziewki, aby splugawili imię świętobliwości mojej;
8 Watu hulala kando ya kila madhabahu juu ya nguo zilizowekwa rehani. Katika nyumba ya mungu wao hunywa mvinyo ulionunuliwa kwa fedha walizotozwa watu.
I na szatach zastawionych kłaniają się przy każdym ołtarzu, a wino tych, co podpadli pod kaźń, piją w domu bogów swoich.
9 “Nilimwangamiza Mwamori mbele yao, ingawa alikuwa mrefu kama mierezi, na mwenye nguvu kama mialoni. Niliyaangamiza matunda yake juu na mizizi yake chini.
Chociażem Ja wytracił Amorejczyka od oblicza ich, którego wysokość była jako wysokość cedrów, aczkolwiek warownie stał jako dąb, wszakżem skaził owoc jego z wierzchu, a korzenie jego ze spodku.
10 “Niliwapandisha toka Misri, na nikawaongoza miaka arobaini jangwani niwape nchi ya Waamori.
A was wywiodłem z ziemi Egipskiej, i prowadziłem was po puszczy czterdzieści lat, żebyście posiedli ziemię Amorejczyka.
11 Pia niliinua manabii kutoka miongoni mwa wana wenu na Wanadhiri kutoka miongoni mwa vijana wenu. Je, hii si kweli, enyi watu wa Israeli?” asema Bwana.
Nadto wzbudzałem z synów waszych proroków, a z młodzieńców waszych Nazarejczyków; izali nie tak jest, o synowie Izraelowi? mówi Pan.
12 “Lakini mliwafanya Wanadhiri kunywa mvinyo na kuwaamuru manabii wasitoe unabii.
Aleście wy napawali Nazarejczyków winem, a prorokom zakazywaliście, mówiąc: Nie prorokujcie.
13 “Sasa basi, nitawaponda kama gari lipondavyo wakati limejazwa nafaka.
Oto Ja ścisnę ziemię waszę, tak jako ciśnie wóz napełniony snopami.
14 Mkimbiaji hodari hatanusurika, wenye nguvu wataishiwa nguvu zao, na shujaa hataweza kuokoa maisha yake.
I zginie ucieczka od prędkiego, a mocarz nie pokrzepi mocy swojej, i duży nie wybawi duszy swojej;
15 Mpiga upinde atakimbia, askari wapiga mbio hawataweza kutoroka, na mpanda farasi hataokoa maisha yake.
A ten, który trzyma łuk, nie ostoi się, i prędki na nogi swe nie uciecze, a ten, który jeździ na koniu, nie zachowa duszy swej,
16 Hata askari walio mashujaa sana siku hiyo watakimbia uchi,” asema Bwana.
Ale i rycerz serca zmężałego między mocarzami nago uciecze w on dzień, mówi Pan.

< Amosi 2 >