< Amosi 2 >

1 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Moabu, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu alichoma mifupa ya mfalme wa Edomu, ikawa kama chokaa.
The Lord God seith these thingis, On thre grete trespassis of Moab, and on foure, Y schal not conuerte it, for it brente the boonys of the kyng of Idumee til to aische.
2 Nitatuma moto juu ya Moabu ambao utateketeza ngome za Keriothi. Moabu ataanguka kwa ghasia kubwa katikati ya vilio vya vita na mlio wa tarumbeta.
And Y schal sende fier in to Moab, and it schal deuoure the housis of Carioth; and Moab schal die in sown, in the noise of a trumpe.
3 Nitamwangamiza mtawala wake na kuwaua maafisa wake wote pamoja naye,” asema Bwana.
And Y schal leese a iuge of the myddis therof, and Y schal sle with it alle the princes therof, seith the Lord.
4 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Yuda, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu wameikataa sheria ya Bwana na hawakuzishika amri zake, kwa sababu wamepotoshwa na miungu ya uongo, miungu ambayo babu zao waliifuata.
The Lord seith these thingis, On thre grete trespassis of Juda, and on foure, Y schal not conuerte hym, for he hath caste awei the lawe of the Lord, and kepte not the comaundementis of hym; for her idols, after whiche the fadris of hem yeden, disseyueden hem.
5 Nitatuma moto juu ya Yuda ambao utateketeza ngome za Yerusalemu.”
And Y schal sende fier in to Juda, and it schal deuoure the housis of Jerusalem.
6 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Israeli, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Wanawauza wenye haki kwa fedha, na maskini kwa jozi ya viatu.
The Lord seith these thingis, On thre grete trespassis of Israel, and on foure, Y schal not conuerte hym, for that that he seelde a iust man for siluer, and a pore man for schoon.
7 Wanakanyaga juu ya vichwa vya maskini, kama vile juu ya mavumbi ya nchi, na kukataa haki kwa walioonewa. Baba na mwanawe hushiriki msichana mmoja, kwa hivyo hulinajisi Jina langu takatifu.
Whiche al to-foulen the heedis of pore men on the dust of erthe, and bowen awei the weie of meke men; and the sone and his fadir yeden to a damesele, that thei schulden defoule myn hooli name.
8 Watu hulala kando ya kila madhabahu juu ya nguo zilizowekwa rehani. Katika nyumba ya mungu wao hunywa mvinyo ulionunuliwa kwa fedha walizotozwa watu.
And thei eeten on clothis leid to wedde bisidis ech auter, and drunken the wyn of dampned men in the hous of her God.
9 “Nilimwangamiza Mwamori mbele yao, ingawa alikuwa mrefu kama mierezi, na mwenye nguvu kama mialoni. Niliyaangamiza matunda yake juu na mizizi yake chini.
Forsothe Y distriede Ammorrei fro the face of hem, whos hiynesse was the hiynesse of cedris, and he was strong as an ook; and Y al to-brak the fruyt of hym aboue, and the rootis of hym bynethe.
10 “Niliwapandisha toka Misri, na nikawaongoza miaka arobaini jangwani niwape nchi ya Waamori.
Y am, that made you to stie fro the lond of Egipt, and ledde you out in desert bi fourti yeer, that ye schulden welde the lond of Ammorrei.
11 Pia niliinua manabii kutoka miongoni mwa wana wenu na Wanadhiri kutoka miongoni mwa vijana wenu. Je, hii si kweli, enyi watu wa Israeli?” asema Bwana.
And Y reiside of youre sones in to profetis, and Nayareis of youre yonge men. Whether it is not so, ye sones of Israel? seith the Lord.
12 “Lakini mliwafanya Wanadhiri kunywa mvinyo na kuwaamuru manabii wasitoe unabii.
And ye birliden wyn to Nayareis, and comaundiden to profetis, and seiden, Profecie ye not.
13 “Sasa basi, nitawaponda kama gari lipondavyo wakati limejazwa nafaka.
Lo! Y schal charke vndur you, as a wayn chargid with hei charkith.
14 Mkimbiaji hodari hatanusurika, wenye nguvu wataishiwa nguvu zao, na shujaa hataweza kuokoa maisha yake.
And fliyt schal perische fro a swift man, and a strong man schal not holde his vertu, and a stalworthe man schal not saue his lijf;
15 Mpiga upinde atakimbia, askari wapiga mbio hawataweza kutoroka, na mpanda farasi hataokoa maisha yake.
and he that holdith a bowe schal not stonde, and a swift man schal not be sauyd by hise feet; and the stiere of an hors schal not saue his lijf,
16 Hata askari walio mashujaa sana siku hiyo watakimbia uchi,” asema Bwana.
and a stronge man of herte schal fle nakid among stronge men in that dai, seith the Lord.

< Amosi 2 >