< Amosi 2 >

1 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Moabu, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu alichoma mifupa ya mfalme wa Edomu, ikawa kama chokaa.
Yahweh says: “For three transgressions of Moab, yes, for four, I will not turn away its punishment, because he burned the bones of the king of Edom into lime;
2 Nitatuma moto juu ya Moabu ambao utateketeza ngome za Keriothi. Moabu ataanguka kwa ghasia kubwa katikati ya vilio vya vita na mlio wa tarumbeta.
but I will send a fire on Moab, and it will devour the palaces of Kerioth; and Moab will die with tumult, with shouting, and with the sound of the trumpet;
3 Nitamwangamiza mtawala wake na kuwaua maafisa wake wote pamoja naye,” asema Bwana.
and I will cut off the judge from among them, and will kill all its princes with him,” says Yahweh.
4 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Yuda, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu wameikataa sheria ya Bwana na hawakuzishika amri zake, kwa sababu wamepotoshwa na miungu ya uongo, miungu ambayo babu zao waliifuata.
Yahweh says: “For three transgressions of Judah, yes, for four, I will not turn away its punishment, because they have rejected Yahweh’s law, and have not kept his statutes, and their lies have led them astray, after which their fathers walked;
5 Nitatuma moto juu ya Yuda ambao utateketeza ngome za Yerusalemu.”
but I will send a fire on Judah, and it will devour the palaces of Jerusalem.”
6 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Israeli, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Wanawauza wenye haki kwa fedha, na maskini kwa jozi ya viatu.
Yahweh says: “For three transgressions of Israel, yes, for four, I will not turn away its punishment, because they have sold the righteous for silver, and the needy for a pair of sandals;
7 Wanakanyaga juu ya vichwa vya maskini, kama vile juu ya mavumbi ya nchi, na kukataa haki kwa walioonewa. Baba na mwanawe hushiriki msichana mmoja, kwa hivyo hulinajisi Jina langu takatifu.
They trample the heads of the poor into the dust of the earth and deny justice to the oppressed. A man and his father use the same maiden, to profane my holy name.
8 Watu hulala kando ya kila madhabahu juu ya nguo zilizowekwa rehani. Katika nyumba ya mungu wao hunywa mvinyo ulionunuliwa kwa fedha walizotozwa watu.
They lay themselves down beside every altar on clothes taken in pledge. In the house of their God they drink the wine of those who have been fined.
9 “Nilimwangamiza Mwamori mbele yao, ingawa alikuwa mrefu kama mierezi, na mwenye nguvu kama mialoni. Niliyaangamiza matunda yake juu na mizizi yake chini.
Yet I destroyed the Amorite before them, whose height was like the height of the cedars, and he was strong as the oaks; yet I destroyed his fruit from above, and his roots from beneath.
10 “Niliwapandisha toka Misri, na nikawaongoza miaka arobaini jangwani niwape nchi ya Waamori.
Also I brought you up out of the land of Egypt and led you forty years in the wilderness, to possess the land of the Amorite.
11 Pia niliinua manabii kutoka miongoni mwa wana wenu na Wanadhiri kutoka miongoni mwa vijana wenu. Je, hii si kweli, enyi watu wa Israeli?” asema Bwana.
I raised up some of your sons for prophets, and some of your young men for Nazirites. Isn’t this true, you children of Israel?” says Yahweh.
12 “Lakini mliwafanya Wanadhiri kunywa mvinyo na kuwaamuru manabii wasitoe unabii.
“But you gave the Nazirites wine to drink, and commanded the prophets, saying, ‘Don’t prophesy!’
13 “Sasa basi, nitawaponda kama gari lipondavyo wakati limejazwa nafaka.
Behold, I will crush you in your place, as a cart crushes that is full of grain.
14 Mkimbiaji hodari hatanusurika, wenye nguvu wataishiwa nguvu zao, na shujaa hataweza kuokoa maisha yake.
Flight will perish from the swift. The strong won’t strengthen his force. The mighty won’t deliver himself.
15 Mpiga upinde atakimbia, askari wapiga mbio hawataweza kutoroka, na mpanda farasi hataokoa maisha yake.
He who handles the bow won’t stand. He who is swift of foot won’t escape. He who rides the horse won’t deliver himself.
16 Hata askari walio mashujaa sana siku hiyo watakimbia uchi,” asema Bwana.
He who is courageous among the mighty will flee away naked on that day,” says Yahweh.

< Amosi 2 >