< Amosi 2 >
1 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Moabu, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu alichoma mifupa ya mfalme wa Edomu, ikawa kama chokaa.
This is what the Lord says: The people of Moab have repeatedly sinned and so I will not hesitate to punish them, because they desecrated the bones of the king of Edom by burning them, turning them into lime.
2 Nitatuma moto juu ya Moabu ambao utateketeza ngome za Keriothi. Moabu ataanguka kwa ghasia kubwa katikati ya vilio vya vita na mlio wa tarumbeta.
So I will send down fire on Moab, and I will burn up the fortresses of Kerioth, and the people of Moab will die in the midst of uproar, battle cries, and the sound of the trumpet.
3 Nitamwangamiza mtawala wake na kuwaua maafisa wake wote pamoja naye,” asema Bwana.
I will cut down their king and all their princes with him, says the Lord.
4 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Yuda, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu wameikataa sheria ya Bwana na hawakuzishika amri zake, kwa sababu wamepotoshwa na miungu ya uongo, miungu ambayo babu zao waliifuata.
This is what the Lord says: The people of Judah have repeatedly sinned and so I will not hesitate to punish them, because they rejected the law of the Lord and have not kept his commands. Their lies have led them astray, the same lies that their forefathers followed.
5 Nitatuma moto juu ya Yuda ambao utateketeza ngome za Yerusalemu.”
So I will send down fire on Judah, and I will burn up the fortresses of Jerusalem.
6 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Israeli, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Wanawauza wenye haki kwa fedha, na maskini kwa jozi ya viatu.
This is what the Lord says: The people of Israel have repeatedly sinned and so I will not hesitate to punish them, because they sell good people for silver, and poor people for a pair of sandals.
7 Wanakanyaga juu ya vichwa vya maskini, kama vile juu ya mavumbi ya nchi, na kukataa haki kwa walioonewa. Baba na mwanawe hushiriki msichana mmoja, kwa hivyo hulinajisi Jina langu takatifu.
They trample the heads of the poor into the dust, and push the needy out of the way. A man and his father have sex with the same servant girl so that my holy name is profaned.
8 Watu hulala kando ya kila madhabahu juu ya nguo zilizowekwa rehani. Katika nyumba ya mungu wao hunywa mvinyo ulionunuliwa kwa fedha walizotozwa watu.
At every altar they stretch themselves out in clothes taken from debtors as collateral, in the temple of their god they drink wine taken from the people they fined.
9 “Nilimwangamiza Mwamori mbele yao, ingawa alikuwa mrefu kama mierezi, na mwenye nguvu kama mialoni. Niliyaangamiza matunda yake juu na mizizi yake chini.
Yet it was I was the one who destroyed the Amorites before you, even though they were as tall as cedars and as strong as oaks. I destroyed them root and branch.
10 “Niliwapandisha toka Misri, na nikawaongoza miaka arobaini jangwani niwape nchi ya Waamori.
It was I who brought you out of the land of Egypt and led you through the desert for forty years so that you could take the Amorites' land.
11 Pia niliinua manabii kutoka miongoni mwa wana wenu na Wanadhiri kutoka miongoni mwa vijana wenu. Je, hii si kweli, enyi watu wa Israeli?” asema Bwana.
I appointed some of your sons to be prophets, and some of your young men to be Nazirites. Isn't this true, people of Israel?
12 “Lakini mliwafanya Wanadhiri kunywa mvinyo na kuwaamuru manabii wasitoe unabii.
But you made the Nazirites sin by drinking wine, and you told the prophets, “Don't tell us what God says.”
13 “Sasa basi, nitawaponda kama gari lipondavyo wakati limejazwa nafaka.
Now see what I am going to do. I will crush you where you are, as if crushed by a heavy cart loaded down with sheaves of grain.
14 Mkimbiaji hodari hatanusurika, wenye nguvu wataishiwa nguvu zao, na shujaa hataweza kuokoa maisha yake.
Not even your fastest runners will escape; strong men will lose their strength. Even the greatest warrior will not be able to save his life.
15 Mpiga upinde atakimbia, askari wapiga mbio hawataweza kutoroka, na mpanda farasi hataokoa maisha yake.
The archer will not stand his ground. The quickest on his feet will not be able to get away, and even those on horseback will not save themselves.
16 Hata askari walio mashujaa sana siku hiyo watakimbia uchi,” asema Bwana.
On that day even the bravest of the mighty warriors will run away naked, says the Lord.