< Amosi 1 >

1 Maneno ya Amosi, mmoja wa wachunga wanyama wa Tekoa: yale aliyoyaona kuhusu Israeli miaka miwili kabla ya tetemeko la ardhi, wakati Uzia alikuwa mfalme wa Yuda, na Yeroboamu mwana wa Yehoashi alikuwa mfalme wa Israeli.
Słowa Amosa, który był między pasterzami z Tekua, które widział o Izraelu za dni Uzyjasza, króla Judzkiego, i za dni Jeroboama, syna Joazowego, króla Izraelskiego, dwa lata przed trzęsieniem ziemi.
2 Alisema: “Bwana ananguruma toka Sayuni, pia ananguruma kutoka Yerusalemu; malisho ya wachunga wanyama yanakauka, kilele cha Karmeli kinanyauka.”
i rzekł: Zaryczy Pan z Syonu, z Jeruzalemu wyda głos swój; i będą płakały mieszkania pasterzy, a wyschną pola najwyborniejsze.
3 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Dameski, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu aliipura Gileadi kwa vyombo vya chuma vyenye meno.
Tak mówi Pan: Dla trzech występków Damaszku, owszem, dla czterech, nie przepuszczę mu, przeto, że młócili wozami żelaznemi Galaada;
4 Nitatuma moto juu ya nyumba ya Hazaeli ambao utateketeza ngome za Ben-Hadadi.
Ale poślę ogień na dom Hazaela, który pożre pałace Benadadowe.
5 Nitalivunja lango la Dameski; nitamwangamiza mfalme aliyeko katika Bonde la Aveni, na yeye ambaye anaishika fimbo ya utawala katika Beth-Edeni. Watu wote wa Aramu watakwenda uhamishoni huko Kiri,” asema Bwana.
Połamię też zaworę w Damaszku, a wykorzenię obywatela z doliny Awen, i tego, który trzyma sceptr z domu Heden; i pójdzie w niewolę lud Syryjski do Kir, mówi Pan.
6 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Gaza, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu walichukua mateka jumuiya nzima na kuwauza kwa Edomu,
Tak mówi Pan: Dla trzech występków Gazy, owszem, dla czterech, nie przepuszczę im, przeto, że ich pojmawszy, w więzienie wieczne podawali Edomczykom;
7 nitatuma moto juu ya kuta za Gaza ambao utateketeza ngome zake.
Ale poślę ogień na mur Gazy, który pożre pałace jej.
8 Nitamwangamiza mfalme wa Ashdodi na yeye aishikaye fimbo ya utawala katika Ashkeloni. Nitaugeuza mkono wangu dhidi ya Ekroni, hadi Mfilisti wa mwisho atakapokufa,” asema Bwana Mwenyezi.
Wykorzenię też obywatela z Azotu, i tego, który trzyma sceptr z Aszkalonu, i obrócę rękę moję przeciwko Akkaronowi, że zginie ostatek Filistynów, mówi panujący Pan.
9 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Tiro, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu ameuza jumuiya nzima ya mateka kwa Edomu, na kutokujali mapatano ya undugu,
Tak mówi Pan: Dla trzech występków Tyru, owszem, dla czterech, nie przepuszczę mu, przeto, że ich w więzienie wieczne podali Edomczykom, a nie wspomnieli na przymierze braterskie;
10 Nitatuma moto kwenye kuta za Tiro ambao utateketeza ngome zake.”
Ale poślę ogień na mur Tyrski, który pożre pałace jego.
11 Hili ndilo Bwana asemalo: “Kwa dhambi tatu za Edomu, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu alimfuatia ndugu yake kwa upanga, alikataa kuonyesha huruma yoyote, kwa sababu hasira yake kali iliendelea kupanda wakati wote na ghadhabu iliwaka bila kuzuiliwa.
Tak mówi Pan: Dla trzech występków Edoma, owszem, dla czterech, nie przepuszczę mu, przeto, że zepsowawszy w sobie wszelaką litość swoję prześladuje mieczem brata swego, a gniewem swym ustawicznie pała, owszem, zapalczywość jego rozsila się bez przestania;
12 Nitatuma moto juu ya Temani ambao utateketeza ngome za Bosra.”
Ale poślę ogień na Teman, i pożre pałace w Bocra.
13 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Amoni, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu aliwatumbua wanawake wajawazito wa Gileadi ili kuongeza mipaka yake.
Tak mówi Pan: Dla trzech występków synów Amonowych, owszem, dla czterech, nie przepuszczę mu, przeto, iż rozcinali brzemienne w Galaad, tylko aby rozszerzali granice swoje;
14 Nitatuma moto kwenye kuta za Raba ambao utateketeza ngome zake katikati ya vilio vya vita katika siku ya mapigano, katikati ya upepo mkali katika siku ya dhoruba.
Ale rozniecę ogień na murze Rabby, który pożre pałace jego z krzykiem w dzień wojny, i z wichrem w dzień niepogody.
15 Mfalme wake atakwenda uhamishoni, yeye pamoja na maafisa wake,” asema Bwana.
I pójdzie król ich w niewolę, on i książęta jego z nim, mówi Pan.

< Amosi 1 >