< Amosi 1 >

1 Maneno ya Amosi, mmoja wa wachunga wanyama wa Tekoa: yale aliyoyaona kuhusu Israeli miaka miwili kabla ya tetemeko la ardhi, wakati Uzia alikuwa mfalme wa Yuda, na Yeroboamu mwana wa Yehoashi alikuwa mfalme wa Israeli.
word Amos which to be in/on/with shepherd from Tekoa which to see upon Israel in/on/with day (Uzziah *L(abh)*) king Judah and in/on/with day Jeroboam son: child Joash king Israel year to/for face: before [the] quaking
2 Alisema: “Bwana ananguruma toka Sayuni, pia ananguruma kutoka Yerusalemu; malisho ya wachunga wanyama yanakauka, kilele cha Karmeli kinanyauka.”
and to say LORD (from Zion *L(abh)*) to roar and from Jerusalem to give: cry out voice his and to mourn habitation [the] to pasture and to wither head: top [the] Carmel
3 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Dameski, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu aliipura Gileadi kwa vyombo vya chuma vyenye meno.
thus to say LORD upon three transgression Damascus and upon four not to return: repent him upon to tread they in/on/with sharp [the] iron [obj] [the] Gilead
4 Nitatuma moto juu ya nyumba ya Hazaeli ambao utateketeza ngome za Ben-Hadadi.
and to send: depart fire in/on/with house: household Hazael and to eat citadel: fortress Ben-hadad Ben-hadad
5 Nitalivunja lango la Dameski; nitamwangamiza mfalme aliyeko katika Bonde la Aveni, na yeye ambaye anaishika fimbo ya utawala katika Beth-Edeni. Watu wote wa Aramu watakwenda uhamishoni huko Kiri,” asema Bwana.
and to break bar Damascus and to cut: eliminate to dwell from (Aven) Valley (Valley of) Aven and to grasp tribe: staff from Beth-eden Beth-eden and to reveal: remove people Syria Kir [to] to say LORD
6 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Gaza, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu walichukua mateka jumuiya nzima na kuwauza kwa Edomu,
thus to say LORD upon three transgression Gaza and upon four not to return: repent him upon to reveal: remove they captivity complete to/for to shut to/for Edom
7 nitatuma moto juu ya kuta za Gaza ambao utateketeza ngome zake.
and to send: depart fire in/on/with wall Gaza and to eat citadel: fortress her
8 Nitamwangamiza mfalme wa Ashdodi na yeye aishikaye fimbo ya utawala katika Ashkeloni. Nitaugeuza mkono wangu dhidi ya Ekroni, hadi Mfilisti wa mwisho atakapokufa,” asema Bwana Mwenyezi.
and to cut: eliminate to dwell from Ashdod and to grasp tribe: staff from Ashkelon and to return: turn back hand: power my upon Ekron and to perish remnant Philistine to say Lord YHWH/God
9 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Tiro, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu ameuza jumuiya nzima ya mateka kwa Edomu, na kutokujali mapatano ya undugu,
thus to say LORD upon three transgression Tyre and upon four not to return: repent him upon to shut they captivity complete to/for Edom and not to remember covenant brother: compatriot
10 Nitatuma moto kwenye kuta za Tiro ambao utateketeza ngome zake.”
and to send: depart fire in/on/with wall Tyre and to eat citadel: fortress her
11 Hili ndilo Bwana asemalo: “Kwa dhambi tatu za Edomu, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu alimfuatia ndugu yake kwa upanga, alikataa kuonyesha huruma yoyote, kwa sababu hasira yake kali iliendelea kupanda wakati wote na ghadhabu iliwaka bila kuzuiliwa.
thus to say LORD upon three transgression Edom and upon four not to return: repent him upon to pursue he in/on/with sword brother: male-sibling his and to ruin compassion his and to tear to/for perpetuity face: anger his and fury his to keep: obey her perpetuity
12 Nitatuma moto juu ya Temani ambao utateketeza ngome za Bosra.”
and to send: depart fire in/on/with Teman and to eat citadel: fortress Bozrah
13 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Amoni, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu aliwatumbua wanawake wajawazito wa Gileadi ili kuongeza mipaka yake.
thus to say LORD upon three transgression son: descendant/people Ammon and upon four not to return: repent him upon to break up/open they pregnant [the] Gilead because to enlarge [obj] border: boundary their
14 Nitatuma moto kwenye kuta za Raba ambao utateketeza ngome zake katikati ya vilio vya vita katika siku ya mapigano, katikati ya upepo mkali katika siku ya dhoruba.
and to kindle fire in/on/with wall Rabbah and to eat citadel: fortress her in/on/with shout in/on/with day battle in/on/with tempest in/on/with day (whirlwind *L(abh)*)
15 Mfalme wake atakwenda uhamishoni, yeye pamoja na maafisa wake,” asema Bwana.
and to go: went king their in/on/with captivity he/she/it and ruler his together to say LORD

< Amosi 1 >