< Amosi 1 >
1 Maneno ya Amosi, mmoja wa wachunga wanyama wa Tekoa: yale aliyoyaona kuhusu Israeli miaka miwili kabla ya tetemeko la ardhi, wakati Uzia alikuwa mfalme wa Yuda, na Yeroboamu mwana wa Yehoashi alikuwa mfalme wa Israeli.
The message of Amos, one of the sheep breeders of Tekoa, which he saw concerning Israel in the reign of King Uzziah of Judah, and in the reign of Jeroboam the son of King Joash of Israel, two years before the earthquake.
2 Alisema: “Bwana ananguruma toka Sayuni, pia ananguruma kutoka Yerusalemu; malisho ya wachunga wanyama yanakauka, kilele cha Karmeli kinanyauka.”
Amos said: Whenever the Lord roars from Zion, and utters his voice from Jerusalem, the pastures of the shepherds dry up, the top of Carmel becomes arid.
3 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Dameski, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu aliipura Gileadi kwa vyombo vya chuma vyenye meno.
The Lord says: For Damascus’ three crimes – no, four! – I will not rescind my judgment. They have threshed Gilead with threshing instruments of iron.
4 Nitatuma moto juu ya nyumba ya Hazaeli ambao utateketeza ngome za Ben-Hadadi.
Therefore I will send fire on Hazael’s house, it will devour the palaces of Ben-hadad.
5 Nitalivunja lango la Dameski; nitamwangamiza mfalme aliyeko katika Bonde la Aveni, na yeye ambaye anaishika fimbo ya utawala katika Beth-Edeni. Watu wote wa Aramu watakwenda uhamishoni huko Kiri,” asema Bwana.
I will break open the gate of Damascus, I will wipe out those who live in the valley of Aven and the sceptered ruler of Beth-Eden. The people of Aram will go into captivity in Kir, says the Lord.
6 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Gaza, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu walichukua mateka jumuiya nzima na kuwauza kwa Edomu,
The Lord says: For Gaza’s three crimes – no, four! – I will not rescind my judgment. They carried away captive a whole nation, sold them as slaves to Edom.
7 nitatuma moto juu ya kuta za Gaza ambao utateketeza ngome zake.
Therefore I will send fire on the wall of Gaza, and it shall devour her palaces.
8 Nitamwangamiza mfalme wa Ashdodi na yeye aishikaye fimbo ya utawala katika Ashkeloni. Nitaugeuza mkono wangu dhidi ya Ekroni, hadi Mfilisti wa mwisho atakapokufa,” asema Bwana Mwenyezi.
And I will wipe out those who live in Ashdod, and the sceptered ruler of Askelon. I will turn my hand against Ekron, and the remnant of the Philistines will perish, says the Lord.
9 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Tiro, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu ameuza jumuiya nzima ya mateka kwa Edomu, na kutokujali mapatano ya undugu,
The Lord says: For Tyre’s three crimes – no, four! – I will not rescind my judgment. They carried away captive a whole people into exile in Edom, and did not remember the brotherly covenant.
10 Nitatuma moto kwenye kuta za Tiro ambao utateketeza ngome zake.”
So I will send fire on the walls of Tyre. It will devour her palaces.
11 Hili ndilo Bwana asemalo: “Kwa dhambi tatu za Edomu, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu alimfuatia ndugu yake kwa upanga, alikataa kuonyesha huruma yoyote, kwa sababu hasira yake kali iliendelea kupanda wakati wote na ghadhabu iliwaka bila kuzuiliwa.
The Lord says: For Edom’s three crimes – no, four! – I will not rescind my judgment. They pursued their relatives with the sword, stilled their pity, cherished their anger continually, retained their fury forever.
12 Nitatuma moto juu ya Temani ambao utateketeza ngome za Bosra.”
So I will send a fire into Teman. It will destroy the palaces of Bozrah.
13 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Amoni, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu aliwatumbua wanawake wajawazito wa Gileadi ili kuongeza mipaka yake.
The Lord says: For Ammonites’ three crimes – no, four! – I will not rescind my judgment. They have ripped open pregnant women in Gilead, in their lust for land.
14 Nitatuma moto kwenye kuta za Raba ambao utateketeza ngome zake katikati ya vilio vya vita katika siku ya mapigano, katikati ya upepo mkali katika siku ya dhoruba.
So I will kindle a fire on the wall of Rabbah. It will destroy her palaces, with a war-cry in the day of battle, with a tempest in the day of the whirlwind.
15 Mfalme wake atakwenda uhamishoni, yeye pamoja na maafisa wake,” asema Bwana.
Their king will go into exile, he and his nobles together, says the Lord.