< Matendo 1 >
1 Katika kitabu changu cha kwanza nilikuandikia, mpendwa Theofilo, kuhusu mambo yote Yesu aliyofanya na kufundisha tangu mwanzo,
Pierwsze wprawdzie księgi napisałem, o Teofilu! o wszystkiem, co począł Jezus i czynić, i uczyć.
2 hadi siku ile alipochukuliwa kwenda mbinguni, baada ya kuwapa maagizo kupitia kwa Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua.
Aż do dnia onego, którego dawszy rozkazanie Apostołom, które był przez Ducha Świętego obrał, wzięty jest w górę.
3 Baada ya mateso yake, alijionyesha kwao na kuwathibitishia kwa njia nyingi kwamba yeye yu hai. Katika muda wa siku arobaini baada ya kufufuka kwake aliwatokea na kunena kuhusu Ufalme wa Mungu.
Którym też samego siebie po męce swojej żywym stawił w wielu niewątpliwych dowodach, przez czterdzieści dni ukazując się im i mówiąc o królestwie Bożem.
4 Wakati mmoja alipokuwa pamoja nao, aliwapa amri hii, “Msitoke Yerusalemu, bali ingojeni ahadi ya Baba, ambayo mmenisikia nikisema habari zake.
A zgromadziwszy je przykazał im, aby nie odchodzili z Jeruzalemu, ale iżby czekali obietnicy ojcowskiej, o którejście mówić słyszeli ode mnie.
5 Yohana aliwabatiza kwa maji, lakini baada ya siku chache mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu.”
Albowiemci Jan chrzcił wodą; ale wy będziecie ochrzczeni Duchem Świętym po niewielu tych dniach.
6 Mitume walipokuwa wamekusanyika pamoja, wakamuuliza Yesu, “Bwana, je, huu ndio wakati wa kuwarudishia Israeli ufalme?”
A tak oni zszedłszy się, pytali go, mówiąc: Panie! izali w tym czasie naprawisz królestwo Izraelskie?
7 Yesu akawaambia, “Si juu yenu kujua nyakati na majira ambayo Baba ameyaweka katika mamlaka yake mwenyewe.
Lecz on rzekł do nich: Nie wasza rzecz jest, znać czasy i chwile, które Ojciec w swojej mocy położył.
8 Lakini mtapokea nguvu akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu, nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, Uyahudi kote na Samaria, hadi miisho ya dunia.”
Ale przyjmiecie moc Ducha Świętego, który przyjdzie na was; i będziecie mi świadkami i w Jeruzalemie, i we wszystkiej Judzkiej ziemi, i w Samaryi, aż do ostatniego kraju ziemi.
9 Baada ya kusema mambo haya, walipokuwa wanatazama, akachukuliwa juu mbinguni mbele ya macho yao na wingu likampokea wasimwone tena.
A to rzekłszy, gdy oni patrzali, w górę podniesiony jest, a obłok wziął go od oczów ich.
10 Walipokuwa bado wakikaza macho yao kuelekea juu alipokuwa akienda zake Mbinguni, tazama ghafula, wanaume wawili waliovaa mavazi meupe wakasimama karibu nao,
A gdy za nim do nieba idącym pilnie patrzali, oto dwaj mężowie stanęli przy nich w białem odzieniu,
11 wakasema, “Enyi watu wa Galilaya, mbona mnasimama mkitazama juu angani? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda Mbinguni, atarudi tena jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake Mbinguni.”
I rzekli: Mężowie Galilejscy! przecz stoicie, patrząc w niebo? Ten Jezus, który w górę wzięty jest od was do nieba, tak przyjdzie, jakoście go widzieli idącego do nieba.
12 Ndipo waliporudi Yerusalemu kutoka Mlima wa Mizeituni, uliokuwa karibu na Yerusalemu, umbali wa mwendo wa Sabato kutoka mjini.
Tedy się wrócili do Jeruzalemu od góry, którą zowią oliwną, która jest blisko Jeruzalemu, mając drogi przez jeden sabat.
13 Walipowasili mjini Yerusalemu, walikwenda ghorofani kwenye chumba walichokuwa wakiishi. Wale waliokuwepo walikuwa: Petro, Yohana, Yakobo, Andrea, Filipo, Tomaso, Bartholomayo, Mathayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni Zelote na Yuda mwana wa Yakobo.
A gdy weszli, wstąpili na salę, gdzie mieszkali Piotr, i Jakób, i Jan, i Andrzej, i Filip, i Tomasz, Bartłomiej, i Mateusz, Jakób Alfeuszowy, i Szymon Zelotes, i Judas Jakóbowy.
14 Hawa wote waliungana pamoja katika maombi. Pamoja nao walikuwepo wanawake kadha, na Maria mama yake Yesu, pamoja na ndugu zake Yesu.
Ci wszyscy trwali jednomyślnie na modlitwie i prośbach, z żonami i z Maryją, matką Jezusową, i z braćmi jego.
15 Katika siku hizo Petro akasimama katikati ya waumini (jumla yao wote walikuwa watu wapatao 120), akasema,
A w oneż dni, powstawszy Piotr w pośrodku uczniów, rzekł: (A był poczet osób wespół zgromadzonych około sta i dwudziestu):
16 “Ndugu zangu, ilibidi Andiko litimie ambalo Roho Mtakatifu alitabiri kupitia kwa Daudi kumhusu Yuda aliyewaongoza wale waliomkamata Yesu.
Mężowie bracia! musiało się wypełnić ono pismo, które opowiedział Duch Święty przez usta Dawidowe o Judaszu, który był wodzem tych, co pojmali Jezusa;
17 Yuda alikuwa mmoja wetu, kwa maana na yeye alichaguliwa ashiriki katika huduma hii.”
Bo był policzony z nami i dostał był cząstki tego usługiwania.
18 (Basi Yuda alinunua shamba kwa zile fedha za uovu alizopata; akiwa huko shambani akaanguka, akapasuka na matumbo yote yakatoka nje.
Tenci wprawdzie otrzymał rolę z zapłaty niesprawiedliwości, a powiesiwszy się, rozpukł się na poły i wypłynęły wszystkie wnętrzności jego.
19 Kila mtu Yerusalemu akasikia habari hizi, kwa hiyo wakapaita mahali hapo kwa lugha yao, Akeldama, yaani Shamba la Damu).
I było to jawne wszystkim mieszkającym w Jeruzalemie, tak iż nazwano onę rolę własnym ich językiem Akieldama, to jest rola krwi.
20 “Kama vile ilivyoandikwa katika kitabu cha Zaburi, “‘Mahali pake na pawe ukiwa, wala asiwepo yeyote atakayeishi humo,’ na, “‘Mtu mwingine aichukue nafasi yake ya uongozi.’
Albowiem napisano w księgach Psalmów: Niechaj będzie mieszkanie jego puste, a niech nie będzie, kto by w niem mieszkał, a biskupstwo jego niech weźmie inny.
21 Kwa hiyo inatubidi tumchague mtu mwingine miongoni mwa wale ambao wamekuwa pamoja nasi wakati wote Bwana Yesu alipoingia na kutoka katikati yenu,
Potrzeba tedy, aby jeden z tych mężów, którzy z nami bywali po wszystek czas, który Pan Jezus przebywał między nami,
22 kuanzia ubatizo wa Yohana mpaka siku aliyochukuliwa kutoka kwetu kwenda Mbinguni. Kwa kuwa mmoja wao inabidi awe shahidi pamoja nasi wa ufufuo wake.”
Począwszy od chrztu Janowego, aż do tego dnia, którego jest wzięty w górę od nas, był z nami świadkiem zmartwychwstania jego.
23 Wakapendekeza majina ya watu wawili: Yosefu, aitwaye Barsaba (ambaye pia alijulikana kama Yusto) na Mathiya.
I postawili dwóch: Józefa, którego zwano Barsabaszem, którego też nazywano Justem, i Macieja.
24 Kisha wakaomba, wakasema, “Bwana, wewe waujua moyo wa kila mtu. Tuonyeshe ni yupi kati ya hawa wawili uliyemchagua
A modląc się mówili: Ty Panie! który znasz serca wszystkich, okaż z tych dwóch jednego, któregoś obrał;
25 ili achukue nafasi ya huduma ya utume ambayo Yuda aliiacha ili aende mahali pake mwenyewe.”
Aby przyjął cząstkę usługiwania tego i apostolstwa, z którego wypadł Judasz, aby odszedł na miejsce swoje.
26 Kisha wakawapigia kura, nayo kura ikamwangukia Mathiya, naye akaongezwa kwenye wale mitume kumi na mmoja.
I rzucili losy ich. I padł los na Macieja; a przyłączony jest spólnem zdaniem do jedenastu Apostołów.