< Matendo 1 >

1 Katika kitabu changu cha kwanza nilikuandikia, mpendwa Theofilo, kuhusu mambo yote Yesu aliyofanya na kufundisha tangu mwanzo,
Le premier livre que j'ai écrit, Théophile, concerne tout ce que Jésus a commencé à faire et à enseigner,
2 hadi siku ile alipochukuliwa kwenda mbinguni, baada ya kuwapa maagizo kupitia kwa Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua.
jusqu'au jour où il a été reçu, après avoir donné ses ordres par le Saint-Esprit aux apôtres qu'il avait choisis.
3 Baada ya mateso yake, alijionyesha kwao na kuwathibitishia kwa njia nyingi kwamba yeye yu hai. Katika muda wa siku arobaini baada ya kufufuka kwake aliwatokea na kunena kuhusu Ufalme wa Mungu.
C'est à eux aussi qu'il s'est montré vivant après avoir souffert, par de nombreuses preuves, en leur apparaissant pendant quarante jours et en leur parlant du royaume de Dieu.
4 Wakati mmoja alipokuwa pamoja nao, aliwapa amri hii, “Msitoke Yerusalemu, bali ingojeni ahadi ya Baba, ambayo mmenisikia nikisema habari zake.
Puis, s'étant réuni avec eux, il leur donna cet ordre: Ne partez pas de Jérusalem, mais attendez la promesse du Père, que vous avez entendue de ma part.
5 Yohana aliwabatiza kwa maji, lakini baada ya siku chache mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu.”
En effet, Jean a baptisé dans l'eau, mais vous, dans peu de jours, vous serez baptisés dans l'Esprit Saint. »
6 Mitume walipokuwa wamekusanyika pamoja, wakamuuliza Yesu, “Bwana, je, huu ndio wakati wa kuwarudishia Israeli ufalme?”
C'est pourquoi, s'étant réunis, ils lui demandèrent: « Seigneur, est-ce maintenant que tu rétablis le royaume d'Israël? »
7 Yesu akawaambia, “Si juu yenu kujua nyakati na majira ambayo Baba ameyaweka katika mamlaka yake mwenyewe.
Il leur dit: « Ce n'est pas à vous de connaître les temps et les moments que le Père a fixés de son propre chef.
8 Lakini mtapokea nguvu akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu, nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, Uyahudi kote na Samaria, hadi miisho ya dunia.”
Mais vous recevrez une puissance, lorsque le Saint-Esprit sera descendu sur vous. Vous serez mes témoins à Jérusalem, dans toute la Judée et la Samarie, et jusqu'aux extrémités de la terre. »
9 Baada ya kusema mambo haya, walipokuwa wanatazama, akachukuliwa juu mbinguni mbele ya macho yao na wingu likampokea wasimwone tena.
Après avoir dit ces choses, comme ils regardaient, il fut enlevé, et une nuée le déroba à leurs yeux.
10 Walipokuwa bado wakikaza macho yao kuelekea juu alipokuwa akienda zake Mbinguni, tazama ghafula, wanaume wawili waliovaa mavazi meupe wakasimama karibu nao,
Comme ils regardaient fixement le ciel pendant qu'il s'en allait, voici, deux hommes en vêtements blancs se tenaient près d'eux.
11 wakasema, “Enyi watu wa Galilaya, mbona mnasimama mkitazama juu angani? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda Mbinguni, atarudi tena jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake Mbinguni.”
Ils dirent aussi: Hommes de Galilée, pourquoi restez-vous là à regarder le ciel? Ce Jésus, qui a été enlevé d'entre vous dans le ciel, reviendra de la même manière que vous l'avez vu aller dans le ciel. »
12 Ndipo waliporudi Yerusalemu kutoka Mlima wa Mizeituni, uliokuwa karibu na Yerusalemu, umbali wa mwendo wa Sabato kutoka mjini.
Puis ils retournèrent à Jérusalem, de la montagne appelée oliviers, qui est près de Jérusalem, à une distance d'un jour de sabbat.
13 Walipowasili mjini Yerusalemu, walikwenda ghorofani kwenye chumba walichokuwa wakiishi. Wale waliokuwepo walikuwa: Petro, Yohana, Yakobo, Andrea, Filipo, Tomaso, Bartholomayo, Mathayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni Zelote na Yuda mwana wa Yakobo.
Après leur arrivée, ils montèrent dans la chambre haute où ils séjournaient, c'est-à-dire Pierre, Jean, Jacques, André, Philippe, Thomas, Barthélemy, Matthieu, Jacques, fils d'Alphée, Simon le Zélote, et Judas, fils de Jacques.
14 Hawa wote waliungana pamoja katika maombi. Pamoja nao walikuwepo wanawake kadha, na Maria mama yake Yesu, pamoja na ndugu zake Yesu.
Tous ceux-là, d'un commun accord, persévéraient dans la prière et la supplication, ainsi que les femmes, Marie, mère de Jésus, et ses frères.
15 Katika siku hizo Petro akasimama katikati ya waumini (jumla yao wote walikuwa watu wapatao 120), akasema,
En ces jours-là, Pierre se leva au milieu des disciples (dont le nombre était d'environ cent vingt), et dit:
16 “Ndugu zangu, ilibidi Andiko litimie ambalo Roho Mtakatifu alitabiri kupitia kwa Daudi kumhusu Yuda aliyewaongoza wale waliomkamata Yesu.
Frères, il fallait que s'accomplît cette Écriture, que le Saint-Esprit avait déjà annoncée par la bouche de David au sujet de Judas, qui servait de guide à ceux qui avaient pris Jésus.
17 Yuda alikuwa mmoja wetu, kwa maana na yeye alichaguliwa ashiriki katika huduma hii.”
Car il a été compté parmi nous, et il a reçu sa part dans ce ministère.
18 (Basi Yuda alinunua shamba kwa zile fedha za uovu alizopata; akiwa huko shambani akaanguka, akapasuka na matumbo yote yakatoka nje.
Or, cet homme s'est procuré un champ avec la récompense de sa méchanceté; et, tombant la tête la première, son corps s'est ouvert et tous ses intestins ont jailli.
19 Kila mtu Yerusalemu akasikia habari hizi, kwa hiyo wakapaita mahali hapo kwa lugha yao, Akeldama, yaani Shamba la Damu).
Tous les habitants de Jérusalem apprirent que, dans leur langue, ce champ était appelé « Akeldama », c'est-à-dire « champ du sang ».
20 “Kama vile ilivyoandikwa katika kitabu cha Zaburi, “‘Mahali pake na pawe ukiwa, wala asiwepo yeyote atakayeishi humo,’ na, “‘Mtu mwingine aichukue nafasi yake ya uongozi.’
Car il est écrit dans le livre des Psaumes, « Que sa demeure devienne déserte. Que personne n'y habite. et, « Laissez un autre prendre son poste.
21 Kwa hiyo inatubidi tumchague mtu mwingine miongoni mwa wale ambao wamekuwa pamoja nasi wakati wote Bwana Yesu alipoingia na kutoka katikati yenu,
« Parmi les hommes qui nous ont accompagnés pendant tout le temps où le Seigneur Jésus est entré et sorti au milieu de nous,
22 kuanzia ubatizo wa Yohana mpaka siku aliyochukuliwa kutoka kwetu kwenda Mbinguni. Kwa kuwa mmoja wao inabidi awe shahidi pamoja nasi wa ufufuo wake.”
depuis le baptême de Jean jusqu'au jour où il a été reçu d'entre nous, il faut que l'un d'eux devienne avec nous témoin de sa résurrection. »
23 Wakapendekeza majina ya watu wawili: Yosefu, aitwaye Barsaba (ambaye pia alijulikana kama Yusto) na Mathiya.
Ils en présentèrent deux: Joseph appelé Barsabbas, qu'on appelait aussi Justus, et Matthias.
24 Kisha wakaomba, wakasema, “Bwana, wewe waujua moyo wa kila mtu. Tuonyeshe ni yupi kati ya hawa wawili uliyemchagua
Ils prièrent et dirent: « Toi, Seigneur, qui connais le cœur de tous les hommes, montre lequel de ces deux-là tu as choisi
25 ili achukue nafasi ya huduma ya utume ambayo Yuda aliiacha ili aende mahali pake mwenyewe.”
pour participer à ce ministère et à cet apostolat dont Judas s'est dépouillé, afin qu'il aille à sa place. »
26 Kisha wakawapigia kura, nayo kura ikamwangukia Mathiya, naye akaongezwa kwenye wale mitume kumi na mmoja.
On tira au sort pour eux, et le sort tomba sur Matthias; il fut compté parmi les onze apôtres.

< Matendo 1 >