< Matendo 9 >
1 Wakati ule ule, Sauli alikuwa bado anazidisha vitisho vya kuua wanafunzi wa Bwana, akamwendea kuhani mkuu,
But Saul still breathing out threatnings and slaughter against the disciples of the Lord, came to the high priest, and desired of him letters to the synagogues at Damascus,
2 naye akamwomba kuhani mkuu ampe barua za kwenda kwenye masinagogi huko Dameski, ili akimkuta mtu yeyote wa Njia Ile, akiwa mwanaume au mwanamke, aweze kuwafunga na kuwaleta Yerusalemu.
that if he should find any of this persuasion, men or women, he might bring them bound to Jerusalem.
3 Basi akiwa katika safari yake, alipokaribia Dameski, ghafula nuru kutoka mbinguni ikamwangaza kotekote.
And as he was on his journey, and came near to Damascus, suddenly there shone round about him a light from heaven;
4 Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia, “Sauli, Sauli, mbona unanitesa?”
and he fell to the ground, and heard a voice saying to him, Saul, Saul, why persecutest thou me?
5 Sauli akajibu, “U nani wewe, Bwana?” Ile sauti ikajibu, “Mimi ni Yesu unayemtesa.
And he said, Who art Thou, Lord? And the Lord said, I am Jesus the Nazarene whom thou art persecuting: it is hard for thee to kick against the goads.
6 Sasa inuka uingie mjini, nawe utaambiwa yakupasayo kutenda.”
And he trembling and astonished said, Lord, what wilt Thou have me to do? And the Lord said unto him, Arise and go into the city, and it shall be told thee, what thou must do.
7 Watu waliokuwa wakisafiri pamoja na Sauli wakasimama bila kuwa na la kusema, kwa sababu walisikia sauti lakini hawakumwona aliyekuwa akizungumza.
And the men that went along with him, stood astonished, hearing the voice, but seeing no one.
8 Sauli akainuka kutoka pale chini na alipojaribu kufungua macho yake hakuweza kuona kitu chochote. Basi wakamshika mkono wakamwongoza mpaka Dameski.
And Saul rose from the earth, but when he opened his eyes he could not see: so they led him by the hand, and brought him to Damascus.
9 Naye kwa muda wa siku tatu alikuwa kipofu naye hakula wala kunywa chochote.
And he was three days without sight, and did neither eat nor drink.
10 Huko Dameski alikuwepo mwanafunzi mmoja jina lake Anania. Bwana alimwita katika maono, “Anania!” Akajibu, “Mimi hapa Bwana.”
Now there was a certain disciple at Damascus, named Ananias, and the Lord said to him in a vision, Ananias, and he said, Behold, I am here, Lord.
11 Bwana akamwambia, “Ondoka uende katika barabara iitwayo Nyofu ukaulize katika nyumba ya Yuda mtu kutoka Tarso, jina lake Sauli, kwa maana wakati huu anaomba,
And the Lord said unto him, Arise and go into the street which is called Strait, and enquire in the house of Judas for one Saul, of Tarsus:
12 katika maono amemwona mtu aitwaye Anania akija na kuweka mikono juu yake ili apate kuona tena.”
for behold he is praying, and hath seen in a vision a man named Ananias, coming in and putting his hand upon him, that he might recover his sight.
13 Anania akajibu, “Bwana, nimesikia kutoka kwa watu wengi habari nyingi kuhusu mtu huyu na madhara yote aliyowatendea watakatifu wako huko Yerusalemu.
And Ananias answered, Lord, I have heard from many of this man, how much mischief he hath done to thy saints at Jerusalem:
14 Naye amekuja hapa Dameski akiwa na mamlaka kutoka kwa viongozi wa makuhani ili awakamate wote wanaotaja jina lako.”
and here too he hath authority from the chief priests to apprehend all that call upon thy name.
15 Lakini Bwana akamwambia Anania, “Nenda! Mtu huyu ni chombo changu kiteule nilichokichagua, apate kulichukua Jina langu kwa watu wa Mataifa na wafalme wao na mbele ya watu wa Israeli.
But the Lord said unto him, Go thy way, for he is the instrument I have chosen, to bear my name before the Gentiles, and kings, and the children of Israel:
16 Nami nitamwonyesha jinsi impasavyo kuteseka kwa ajili ya Jina langu.”
for I will shew him how great sufferings he must endure for my name.
17 Kisha Anania akaenda kwenye ile nyumba, akaingia ndani. Akaweka mikono yake juu ya Sauli akasema, “Ndugu Sauli, Bwana Yesu aliyekutokea njiani amenituma kwako ili upate kuona tena na ujazwe Roho Mtakatifu.”
And Ananias went away and came into the house; and putting his hands on him, said, "Brother Saul, the Lord, even Jesus, who appeared to thee on the way as thou camest, hath sent me, that thou mightest receive thy sight, and be filled with the holy Spirit."
18 Ghafula vitu kama magamba vikaanguka chini, kutoka machoni mwa Sauli, akapata kuona tena. Akasimama, akabatizwa.
And immediately there fell from his eyes as it were scales; and he instantly recovered his sight, and arose and was baptized.
19 Baada ya kula chakula, akapata nguvu tena. Sauli akakaa siku kadhaa pamoja na wanafunzi huko Dameski.
And when he had taken some nourishment, he was strengthened. Now Saul was with the disciples at Damascus for some time.
20 Papo hapo akaanza kuhubiri kwenye masinagogi kwamba “Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu”
And he immediately preached Christ in the synagogues, that He is the Son of God.
21 Watu wote waliomsikia Sauli walishangaa na kuuliza, “Huyu si yule mtu aliyesababisha maangamizi makuu huko Yerusalemu miongoni mwa watu waliolitaja jina hili? Naye si amekuja hapa kwa kusudi la kuwakamata na kuwapeleka wakiwa wafungwa mbele ya viongozi wa makuhani?”
But all that heard him, were amazed, and said, Is not this he that persecuted those in Jerusalem who called on this name, and came hither for this end, that he might carry them bound to the chief priests?
22 Sauli akazidi kuwa hodari na kuwashangaza Wayahudi walioishi Dameski kwa kuthibitisha kuwa Yesu ndiye Kristo.
But Saul prevailed more and more, and confounded the Jews that dwelt at Damascus, fully proving that this same Jesus is the Christ.
23 Baada ya siku nyingi kupita, Wayahudi wakafanya shauri kumuua Sauli.
And after a considerable time, the Jews conspired to kill him:
24 Lakini shauri lao likajulikana kwa Sauli. Wayahudi wakawa wanalinda malango yote ya mji, usiku na mchana ili wapate kumuua.
but Saul was apprised of their design. And they watched the gates day and night, to make away with him:
25 Lakini wafuasi wake wakamchukua usiku wakamshusha akiwa ndani ya kapu kupitia mahali penye nafasi ukutani.
but the disciples took him by night, and let him down by the wall, in a basket.
26 Sauli alipofika Yerusalemu akajaribu kujiunga na wanafunzi lakini wote walimwogopa, kwa maana hawakuamini kwamba kweli naye alikuwa mwanafunzi.
And when Saul was come to Jerusalem, he attempted to associate with the disciples: and they were all afraid of him, not believing that he was a disciple.
27 Lakini Barnaba akamchukua, akampeleka kwa wale mitume. Akawaeleza jinsi Sauli akiwa njiani alivyomwona Bwana, jinsi Bwana alivyosema naye na jinsi alivyohubiri kwa ujasiri kwa jina la Yesu huko Dameski.
But Barnabas took and brought him to the apostles, and related to them, how he had seen the Lord in the way, and that He had spoken to him; and how he had preached boldly at Damascus in the name of Jesus.
28 Kwa hiyo Sauli akakaa nao akitembea kwa uhuru kila mahali huko Yerusalemu, akihubiri kwa ujasiri katika jina la Bwana.
And he was with them coming in and going out at Jerusalem, and preaching openly in the name of the Lord Jesus:
29 Alinena na kuhojiana na Wayahudi wenye asili ya Kiyunani lakini wao walijaribu kumuua.
and he talked and disputed with the Hellenists, who attempted to kill him:
30 Wale ndugu walipopata habari wakampeleka hadi Kaisaria, wakamsafirisha kwenda Tarso.
but when the brethren knew it, they brought him down to Cesarea, and sent him away to Tarsus.
31 Ndipo kanisa katika Uyahudi wote, Galilaya na Samaria likafurahia wakati wa amani. Likatiwa nguvu, na kwa faraja ya Roho Mtakatifu, idadi yake ikazidi kuongezeka, na likaendelea kudumu katika kumcha Bwana.
Then the churches throughout all Judea, and Galilee, and Samaria, had rest, being edified and walking in the fear of the Lord; and through the consolation of the holy Spirit were multiplied.
32 Petro alipokuwa akisafiri sehemu mbalimbali, alikwenda kuwatembelea watakatifu walioishi huko Lida.
And it came to pass that as Peter was going through all parts, he came down also to the saints that dwelt at Lydda.
33 Huko alimkuta mtu mmoja aitwaye Ainea, ambaye alikuwa amepooza na kwa muda wa miaka minane alikuwa hajaondoka kitandani.
And there he found a man named Eneas, who had kept his bed eight years, with the palsy.
34 Petro akamwambia, “Ainea, Yesu Kristo anakuponya, inuka utandike kitanda chako.” Mara Ainea akainuka.
And Peter said unto him, Eneas, Jesus the Messiah, healeth thee. Arise, and make thy bed. And he rose up immediately.
35 Watu wote wa Lida na Sharoni walipomwona Ainea akitembea wakamgeukia Bwana.
And all that dwelt at Lydda and in Saron saw him, and turned to the Lord.
36 Huko Yafa palikuwa na mwanafunzi jina lake Tabitha (ambalo kwa Kiyunani ni Dorkasi). Huyu alikuwa mkarimu sana, akitenda mema na kuwasaidia maskini.
And there was at Joppa a certain female disciple named Tabitha, who by interpretation is called in Greek Dorcas: and she was full of good works and alms-deeds.
37 Wakati huo akaugua, akafa na wakiisha kuuosha mwili wake wakauweka katika chumba cha ghorofani.
And it happened, about the same time, that she fell sick and died: and when they had washed her they laid her out in an upper chamber.
38 Kwa kuwa Yafa hapakuwa mbali sana na Lida, wanafunzi waliposikia kwamba Petro yuko huko waliwatuma watu wawili kwake ili kumwomba, “Tafadhali njoo huku pasipo kukawia.”
And as Lydda was near to Joppa, the disciples hearing that Peter was there sent two men to him, intreating him that he would not delay to come to them.
39 Kwa hiyo Petro akainuka akaenda nao, naye alipowasili, wakampeleka hadi kwenye chumba cha ghorofani alipokuwa amelazwa. Wajane wengi walisimama karibu naye wakilia na kuonyesha majoho na nguo nyingine ambazo Dorkasi alikuwa amewashonea alipokuwa pamoja nao.
Then Peter arose, and went with them: and when he was come, they brought him into the upper chamber. And all the widows stood round him weeping, and shewing him the coats and garments which Dorcas made when she was with them.
40 Petro akawatoa wote nje ya kile chumba, kisha akapiga magoti akaomba, akaugeukia ule mwili akasema, “Tabitha, inuka.” Akafumbua macho yake na alipomwona Petro, akaketi.
But Peter, putting them all out, kneeled down and prayed: and then turning to the body he said, Tabitha, arise. And she opened her eyes, and when she saw Peter, she sat up.
41 Petro akamshika mkono akamwinua, ndipo akawaita wale watakatifu na wajane akamkabidhi kwao akiwa hai.
And giving her his hand he raised her up, and calling the saints and widows he presented her alive.
42 Habari hizi zikajulikana sehemu zote za Yafa na watu wengi wakamwamini Bwana.
And it was soon known throughout all Joppa, and many believed on the Lord.
43 Petro akakaa Yafa kwa siku nyingi akiishi na Simoni mtengenezaji ngozi.
And he staid many days in Joppa with one Simon a tanner.