< Matendo 8 >
1 Naye Sauli alikuwepo pale, akiridhia kuuawa kwa Stefano. Siku ile kukatukia mateso makuu dhidi ya kanisa huko Yerusalemu, waumini wote isipokuwa mitume wakatawanyika, wakakimbilia Uyahudi na Samaria.
扫罗也认可了对司提芬的杀戮。从那天起,耶路撒冷的教会受到严重迫害。除了使徒以外,其他信徒都散落到犹太和撒玛利亚各地。
2 Watu wacha Mungu wakamzika Stefano na kumwombolezea sana.
(有些虔诚之人怀着巨大的悲痛安葬了司提芬)。
3 Lakini kwa habari ya Sauli alikuwa analiharibu kanisa, akiingia nyumba kwa nyumba, akiwaburuta wanawake na wanaume na kuwatupa gerezani.
扫罗却开始残害教会,挨家挨户地将男男女女拖出去坐监。
4 Kwa hiyo wale waliotawanyika wakalihubiri neno la Mungu kila mahali walipokwenda.
那些散落各地的信徒,会在所到之处传扬上帝之道。
5 Filipo akateremkia mji mmoja wa Samaria akawahubiria habari za Kristo
腓利来到了撒玛利亚城,向民众宣讲基督。
6 Watu walipomsikia Filipo na kuona ishara na miujiza aliyofanya, wakasikiliza kwa bidii yale aliyosema.
群众听到腓利所讲,看见他所行神迹,于是便全心聆听他的一字一句。
7 Pepo wachafu wakawa wakiwatoka watu wengi huku wakipiga kelele na wengi waliopooza na viwete wakaponywa.
许多魔鬼附体之人得救了,他们身上的恶灵嚎叫着被驱赶出来,还有许多瘫痪和残疾之人都得到痊愈。
8 Hivyo pakawa na furaha kuu katika mji huo.
城里的民众们欢天喜地。
9 Basi mtu mmoja jina lake Simoni alikuwa amefanya uchawi kwa muda mrefu katika mji huo akiwashangaza watu wote wa Samaria. Alijitapa kwamba yeye ni mtu mkuu,
城里有一人名叫西门,善用邪术。他自称是一位重要的大人物,让撒玛利亚人为之而惊叹。
10 nao watu wote wakubwa kwa wadogo wakamsikiliza na kumaka, wakisema “Mtu huyu ndiye uweza wa Mungu ujulikanao kama ‘Uweza Mkuu.’”
城中之人无论高高在上还是卑微在下,都听从于他,说:“这就是那‘大能上帝’之人。”
11 Wakamfuata kwa sababu kwa muda mrefu alikuwa amewashangaza kwa uchawi wake.
因为他长久以来用邪术蒙蔽众人,让他们对之感到信服。
12 Lakini watu walipomwamini Filipo alipohubiri habari njema za Ufalme wa Mungu na jina la Yesu Kristo, wakabatizwa wanaume na wanawake.
腓利来此向他们传递上帝之国的福音,宣讲耶稣基督之名,于是众人相信了腓利,男女女女均受了洗。
13 Simoni naye akaamini na akabatizwa. Akamfuata Filipo kila mahali, akistaajabishwa na ishara kuu na miujiza aliyoiona.
连西门自己也相信并受洗,然后跟随腓利,为所目睹的神迹和奇迹而惊叹不已。
14 Basi mitume waliokuwa Yerusalemu waliposikia kuwa Samaria wamelipokea neno la Mungu, wakawatuma Petro na Yohana waende huko.
听说撒玛利亚的居民接受了上帝之道,耶路撒冷的使徒就派彼得和约翰到那里去。
15 Nao walipofika wakawaombea ili wampokee Roho Mtakatifu,
二人赶到后就为改变信仰的信徒祷告,让他们接受圣灵。
16 kwa sababu Roho Mtakatifu alikuwa bado hajawashukia hata mmoja ila wamebatizwa tu katika jina la Bwana Yesu.
但圣灵尚未降在他们任何一个身上,他们只是以耶稣之名受了洗。
17 Ndipo Petro na Yohana wakaweka mikono yao juu ya wale waliobatizwa, nao wakapokea Roho Mtakatifu.
使徒为他们行按手礼,他们便接受了圣灵。
18 Simoni alipoona kuwa watu wanapokea Roho Mtakatifu mitume walipoweka mikono juu yao, akataka kuwapa fedha
西门看见使徒按手后就有圣灵降临,就拿出钱给使徒,
19 akisema, “Nipeni na mimi uwezo huu ili kila mtu nitakayeweka mikono yangu juu yake apate kupokea Roho Mtakatifu.”
他请求道:“把这力量也给我吧,让我为谁按手,谁就可以接受圣灵。”
20 Petro akamjibu, “Fedha yako na iangamie pamoja nawe, kwa sababu ulidhani unaweza kununua karama ya Mungu kwa fedha!
彼得对他说:“让你的钱跟你一同灭亡吧!你居然以为上帝的恩赐可以用钱购买!
21 Wewe huna sehemu wala fungu katika huduma hii kwa kuwa moyo wako si mnyofu mbele za Mungu.
你不属于这里,这里的一切也不属于你,因为在上帝眼中,你的态度大错特错。
22 Kwa hiyo tubu kwa uovu huu wako na umwombe Bwana. Yamkini aweza kukusamehe mawazo uliyo nayo moyoni mwako.
为自己的罪恶行径忏悔吧!祈求主,请求他原谅你这样的想法。
23 Kwa maana ninaona kwamba wewe umejawa na uchungu na ni mfungwa wa dhambi.”
我可以看出你心中满是强烈的嫉妒,被你的恶所捆绑。”
24 Ndipo Simoni akajibu, “Niombeeni kwa Bwana, ili hayo mliyosema lolote yasinitukie.”
西门回答:“请为我求主,别让你们说的事情发生在我身上!”
25 Nao walipokwisha kutoa ushuhuda na kuhubiri neno la Bwana, wakarudi Yerusalemu wakihubiri Injili katika vijiji vingi vya Samaria.
使徒作了见证并宣讲了主的道,然后就返回耶路撒冷,沿途在撒玛利亚人的许多村庄里传扬福音。
26 Basi malaika wa Bwana akamwambia Filipo, “Nenda upande wa kusini kwenye ile barabara itokayo Yerusalemu kuelekea Gaza ambayo ni jangwa.”
主的天使对腓利说:“准备好向南走,你要去耶路撒冷到迦萨的那条荒漠道路。”
27 Hivyo akaondoka. Akiwa njiani akakutana na towashi wa Kushi, aliyekuwa afisa mkuu, mwenye mamlaka juu ya hazina zote za Kandake, Malkia wa Kushi. Huyu towashi alikuwa amekwenda Yerusalemu ili kuabudu,
于是腓利动身出发,路上遇到一名衣索匹亚人,是衣索匹亚女王干大基手下一名位高权重的官员,掌管女王全部国库。他去耶路撒冷去礼拜。
28 naye akiwa njiani kurudi nyumbani alikuwa ameketi garini mwake akisoma kitabu cha nabii Isaya.
在回来的路上,坐在马车上翻看以赛亚先知的书。
29 Roho Mtakatifu akamwambia Filipo, “Nenda kwenye lile gari ukae karibu nalo.”
圣灵对腓利说:“走过去,走近那车子。”
30 Ndipo Filipo akakimbilia lile gari na kumsikia yule mtu anasoma kitabu cha nabii Isaya. Filipo akamuuliza, “Je, unaelewa hayo usomayo?”
于是腓利跑过去,听见那官员在读以赛亚先知的书,就询问:“你明白自己看到的内容吗?”
31 Yule towashi akasema, “Nitawezaje kuelewa mtu asiponifafanulia?” Hivyo akamkaribisha Filipo ili apande na kuketi pamoja naye.
那官员说:“没有人指导,我怎能明白呢?”于是就请腓利上车,坐在他身边。
32 Huyu towashi alikuwa anasoma fungu hili la Maandiko: “Aliongozwa kama kondoo aendaye machinjoni, kama mwana-kondoo anyamazavyo mbele yake yule amkataye manyoya, hivyo hakufungua kinywa chake.
他当时在读的那段经文是:“他像绵羊一样被牵走宰杀,又像羔羊一样在剪羊毛之人面前沉默无声,他一句话也不说。
33 Katika kufedheheshwa kwake alinyimwa haki yake. Nani awezaye kueleza juu ya kizazi chake? Kwa maana maisha yake yaliondolewa kutoka duniani.”
他受尽屈辱,得不到公平的审判。没有人知道他的后裔会是谁,因为他的生命走向终点。”
34 Yule towashi akamuuliza Filipo, “Tafadhali niambie, nabii huyu anena habari zake mwenyewe au habari za mtu mwingine?”
那官员对腓利说:“请问先知这番话是在说谁?他自己?还是指别人?”
35 Ndipo Filipo akaanza kutumia fungu lile la Maandiko, akamweleza habari njema za Yesu.
腓利开始解释,从这段经文开始,向他传讲耶稣。
36 Walipokuwa wakiendelea na safari wakafika mahali palipokuwa na maji, yule towashi akamuuliza Filipo, “Tazama, hapa kuna maji. Kitu gani kitanizuia nisibatizwe?” [
他们一路走下去,来到一处溪流,官员说:“你看,这里有水,为什么我不受洗呢?”
37 Filipo akamwambia, “Kama ukiamini kwa moyo wako wote unaweza kubatizwa.” Akajibu, “Naamini kuwa Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu.”]
38 Naye akaamuru lile gari lisimamishwe. Wakateremka kwenye maji wote wawili, yule towashi na Filipo, naye Filipo akambatiza.
于是官员吩咐停车,腓利和他两人走到水中,腓利给他施洗。
39 Nao walipopanda kutoka kwenye maji, ghafula Roho wa Bwana akamnyakua Filipo, naye towashi hakumwona tena, lakini akaenda zake akifurahi.
他们从水里出来时,主的圣灵就把腓利带走了,送到了亚锁都。官员再也没有见到他,但仍满心喜悦地继续旅程。
40 Filipo akajikuta yuko Azoto, akasafiri akihubiri Injili katika miji yote mpaka alipofika Kaisaria.
腓利在亚锁都走遍各城,传讲福音,最终来到该撒利亚。