< Matendo 8 >

1 Naye Sauli alikuwepo pale, akiridhia kuuawa kwa Stefano. Siku ile kukatukia mateso makuu dhidi ya kanisa huko Yerusalemu, waumini wote isipokuwa mitume wakatawanyika, wakakimbilia Uyahudi na Samaria.
Sawluh naw Stephen ami hnim vai jah tängpüiki. Acuna mhnüp üng Jerusalem mlüha veki sangcim cun aktäa mkhuimkhanak kham lawki he; acunakyase, Ngsäe däk ve hüt u se, jumeikie naküt cun Judah ja Samarih hnea ngpyeng hükie.
2 Watu wacha Mungu wakamzika Stefano na kumwombolezea sana.
Acunüng, Pamhnam jumkie naw, Stephen cun k’ut u lü, aktäa ami kya.
3 Lakini kwa habari ya Sauli alikuwa analiharibu kanisa, akiingia nyumba kwa nyumba, akiwaburuta wanawake na wanaume na kuwatupa gerezani.
Acunüng, Sawluh naw sangcime aktäa a jah khuimkha, im naküt üng lut hü lü jumeikia nghnumi kpamie jah man lü jah kaih hü lü, thawngim üng a jah khyum.
4 Kwa hiyo wale waliotawanyika wakalihubiri neno la Mungu kila mahali walipokwenda.
Acunüng, pyeng hükia jumkie naw hne naküt üng cit u lü ngthu pyen hükie.
5 Filipo akateremkia mji mmoja wa Samaria akawahubiria habari za Kristo
Philip cun Samarih hnea mlüh ktunga ju citki naw, Mesijaha mawng khyange veia a ju pyen.
6 Watu walipomsikia Filipo na kuona ishara na miujiza aliyofanya, wakasikiliza kwa bidii yale aliyosema.
Khyange naw, ngja u lü Philip naw a mdana müncam phyaki he ami jah hmu üng, a ngthu pyen cun aktäa ami ngaih.
7 Pepo wachafu wakawa wakiwatoka watu wengi huku wakipiga kelele na wengi waliopooza na viwete wakaponywa.
Isetiakyaküng, khawksea jah venake ami k'um üngka naw khawyaie ngpyang u lü lut lawki he. A khaw kceke ja xokie pi ami daw law bea phäha kyaki.
8 Hivyo pakawa na furaha kuu katika mji huo.
Acuna mlüh üngkae cun aktäa jekyaikie.
9 Basi mtu mmoja jina lake Simoni alikuwa amefanya uchawi kwa muda mrefu katika mji huo akiwashangaza watu wote wa Samaria. Alijitapa kwamba yeye ni mtu mkuu,
Sihmon ngming nakia khyang mat veki; ani naw, ajana acuna mlüh üng, sui pawh lü Samarih khyange jah cäicatsak khawikia kyaki. “Kei cun khyang sawxat am ni” a ti.
10 nao watu wote wakubwa kwa wadogo wakamsikiliza na kumaka, wakisema “Mtu huyu ndiye uweza wa Mungu ujulikanao kama ‘Uweza Mkuu.’”
Mlüha veki naküt khyang akdik akdäm naküt naw “Ani hin ‘Hlüngtaikia Johit’ tia ngthangkia Pamhnama Johit ni” ti lü a ngthu pyen cun mcek lü ngaikie.
11 Wakamfuata kwa sababu kwa muda mrefu alikuwa amewashangaza kwa uchawi wake.
A sui bilaw am, aksoa cäicat kphyaki he a ja bilawh khawha phäha, a ngthu cun aktäa ami münnak.
12 Lakini watu walipomwamini Filipo alipohubiri habari njema za Ufalme wa Mungu na jina la Yesu Kristo, wakabatizwa wanaume na wanawake.
Acunsepi, Pamhnama pe thangkdaw ja Jesuh Khritawa ngming thangkdaw Philipa pyen ami jum ja, nghnumi kpami Baptican khan lawki he.
13 Simoni naye akaamini na akabatizwa. Akamfuata Filipo kila mahali, akistaajabishwa na ishara kuu na miujiza aliyoiona.
Sihmon naw pi jum law hnga lü Baptican a kham law päng ja Philipa hlawnga ve lü, müncamkse ja müncamnak a jah pawh cun hmu lü cäiki.
14 Basi mitume waliokuwa Yerusalemu waliposikia kuwa Samaria wamelipokea neno la Mungu, wakawatuma Petro na Yohana waende huko.
Acunüng, Jerusalema vekia Ngsäe naw Samarih hnea khyange naw pi Pamhnama ngthu jumkie tia ami ksing law üng, ami veia Pita ja Johan ami jah tüih;
15 Nao walipofika wakawaombea ili wampokee Roho Mtakatifu,
acu xawi ani ju pha üng, Ngmüimkhya Ngcim ami yahnak vaia ami jah ktaiyü pet.
16 kwa sababu Roho Mtakatifu alikuwa bado hajawashukia hata mmoja ila wamebatizwa tu katika jina la Bwana Yesu.
Am acun ham üng ta ua khana Ngmüimkhya Ngcim am pha law; Bawi Jesuha ngming am Baptican däk va khan hamkiea kyaki.
17 Ndipo Petro na Yohana wakaweka mikono yao juu ya wale waliobatizwa, nao wakapokea Roho Mtakatifu.
Angsä xawi naw ami khana ani kut taih ni se, Ngmüimkhya Ngcim yaheikie.
18 Simoni alipoona kuwa watu wanapokea Roho Mtakatifu mitume walipoweka mikono juu yao, akataka kuwapa fedha
Acunüng, Ngsäea kut taiha phäha Ngmüimkhya Ngcim pha lawki ti cun Sihmon naw a hmuh. Acunüng ngui cun Pita ja Johana veia lawpüiki naw,
19 akisema, “Nipeni na mimi uwezo huu ili kila mtu nitakayeweka mikono yangu juu yake apate kupokea Roho Mtakatifu.”
“Kei pi, khyange khana ka kut taih ngüse, Ngmüimkhya Ngcim ami yahnak thei vaia johit na pe nia” ti lü a jah kthäh.
20 Petro akamjibu, “Fedha yako na iangamie pamoja nawe, kwa sababu ulidhani unaweza kununua karama ya Mungu kwa fedha!
Pamhnama bäkhäknak cun a ngui am khyäi khaia a büa phäha, Pita naw, “Na xünak ja na ngui mulaia cit ni se,
21 Wewe huna sehemu wala fungu katika huduma hii kwa kuwa moyo wako si mnyofu mbele za Mungu.
na mlung Pamhnama hmaia käh ngsungpyunkia kyase, hin üng käh na ngpüi hngaki, na ham pi am ve;
22 Kwa hiyo tubu kwa uovu huu wako na umwombe Bwana. Yamkini aweza kukusamehe mawazo uliyo nayo moyoni mwako.
acunakyase, na mkhyekatnak ngjut lü Bawipa veia ktaiyüa, acunüng, na mlung üng na ngaihnak ni mhlät khai ni.
23 Kwa maana ninaona kwamba wewe umejawa na uchungu na ni mfungwa wa dhambi.”
“Nang cun püi ng’eihnak am bebang lü mkhyekatnaka thawng kyuma na kyaki ti ksing veng” a ti.
24 Ndipo Simoni akajibu, “Niombeeni kwa Bwana, ili hayo mliyosema lolote yasinitukie.”
Acunüng, Sihmon naw, nani pyen ka khana am a pha lawnak vaia, nangni naw Bawipa veia na ktaiyü pe nia” ti lü Pita ja Johan a jah mtheh.
25 Nao walipokwisha kutoa ushuhuda na kuhubiri neno la Bwana, wakarudi Yerusalemu wakihubiri Injili katika vijiji vingi vya Samaria.
Acunüng, ani xawi naw saksi ja Bawipa ngthu ami ksingsak käna, Jerusalem mlüha citbeki xawi. Ani ceh sawa Samarih ngnam khawhah üng Thangkdaw sangki xawi.
26 Basi malaika wa Bwana akamwambia Filipo, “Nenda upande wa kusini kwenye ile barabara itokayo Yerusalemu kuelekea Gaza ambayo ni jangwa.”
Bawipaa khankhawngsä mat naw Philipa veia, “Tho law lü Jerusalem üngkhyüh Kaza khawa cehnaka lam üng cita” a ti (Acuna lam cun tuh ta am sumei ti u.)
27 Hivyo akaondoka. Akiwa njiani akakutana na towashi wa Kushi, aliyekuwa afisa mkuu, mwenye mamlaka juu ya hazina zote za Kandake, Malkia wa Kushi. Huyu towashi alikuwa amekwenda Yerusalemu ili kuabudu,
Acunüng, tho law lü citki. Acua Ethiopia khawa Candace, Ethiopia upki nghnumia khawthem naküt msümcei lü nghnumi awmki cun Jerusalem khawa Pamhnam va hjawkhah khaia citki;
28 naye akiwa njiani kurudi nyumbani alikuwa ameketi garini mwake akisoma kitabu cha nabii Isaya.
a nglat law be lama, a senghlea khana ngaw lü sahma Hesajah cauk üngka kheki.
29 Roho Mtakatifu akamwambia Filipo, “Nenda kwenye lile gari ukae karibu nalo.”
Acunüng, Ngmüimkhya naw Philipa veia, “Cana senghle veia cit lü a hlawnga va vea” a ti.
30 Ndipo Filipo akakimbilia lile gari na kumsikia yule mtu anasoma kitabu cha nabii Isaya. Filipo akamuuliza, “Je, unaelewa hayo usomayo?”
Acunüng, Philip cun acuna ngvaia veia va cit lü sahma Hesajaha cauk khe se ngjaki naw, “Na khea asuilam na ksingki aw?” a ti.
31 Yule towashi akasema, “Nitawezaje kuelewa mtu asiponifafanulia?” Hivyo akamkaribisha Filipo ili apande na kuketi pamoja naye.
Ani naw, “U naw am a na mtheh cun ihawkba ka ksing thei khai ni?” a ti. Acunüng, a veia ngaw hnga khaia Philip cun a khü.
32 Huyu towashi alikuwa anasoma fungu hili la Maandiko: “Aliongozwa kama kondoo aendaye machinjoni, kama mwana-kondoo anyamazavyo mbele yake yule amkataye manyoya, hivyo hakufungua kinywa chake.
Acunüng, Cangcim a khe cun: “Hnim vaia toa mäiha ani cun ami cehpüi; To a mu ami kteih üng käh khihkheh lü a vea mäiha, ani pi käh khihkheh lü veki;
33 Katika kufedheheshwa kwake alinyimwa haki yake. Nani awezaye kueleza juu ya kizazi chake? Kwa maana maisha yake yaliondolewa kutoka duniani.”
Ani cun hnemnak a khamei üng, am cangkia lei ami mtai pet; u naw pi a mjükphyüi mawng am pyen khawh u, isetiakyaküng khawmdeka ania sak cun päihki” kyaki.
34 Yule towashi akamuuliza Filipo, “Tafadhali niambie, nabii huyu anena habari zake mwenyewe au habari za mtu mwingine?”
Acunüng, ngvai naw Philipa veia, “Sahma naw hin hin ua mawng ni a pyen? Amäta mawng mä, khyang kcea mawng mä? Ni kthäh veng na mtheha” a ti.
35 Ndipo Filipo akaanza kutumia fungu lile la Maandiko, akamweleza habari njema za Yesu.
Philip naw, thangkdaw cun ahina Cangcim üngkhyüh tünei lü Jesuha mawng cun a mtheh.
36 Walipokuwa wakiendelea na safari wakafika mahali palipokuwa na maji, yule towashi akamuuliza Filipo, “Tazama, hapa kuna maji. Kitu gani kitanizuia nisibatizwe?” [
Acunüng, lam ani ceh k'um üng, tuia venak pha ni se; ngvai naw, “Tenga, hin üng tui ve ve, Baptican kham vaia i naw na kyawhki ni?” ti se,
37 Filipo akamwambia, “Kama ukiamini kwa moyo wako wote unaweza kubatizwa.” Akajibu, “Naamini kuwa Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu.”]
Philip naw, “Na mlungmthin avan am na jumei üng na kham theiki” ti se; ngvai naw, “Jesuh Khritaw, Pamhnama Cakpaa kyaki ti ka jumki” ti lü a msang.
38 Naye akaamuru lile gari lisimamishwe. Wakateremka kwenye maji wote wawili, yule towashi na Filipo, naye Filipo akambatiza.
Acunüng, angvai naw senghle ngdüihsak lü, Philipa dä ngvai cun tui da citki xawi. Acun üng Philip naw Baptican a khamsak.
39 Nao walipopanda kutoka kwenye maji, ghafula Roho wa Bwana akamnyakua Filipo, naye towashi hakumwona tena, lakini akaenda zake akifurahi.
Acunüng, tui üngka naw ani thaw law be ja, Bawipaa Ngmüimkhya naw Philip cun cehpüi. Angvai naw Philip am hmu ti kyaw lüpi jekyainak am amäta lama citbeki.
40 Filipo akajikuta yuko Azoto, akasafiri akihubiri Injili katika miji yote mpaka alipofika Kaisaria.
Acunsepi, Philip cun Azuk mlüha ngdang law be lü; a ceh sawa acuna mlüh üngkhyüh Ketarih am a pha hama küt üng, mlüh naküt üng thangkdaw sang hüki.

< Matendo 8 >