< Matendo 6 >

1 Basi ikawa katika siku hizo, wakati idadi ya wanafunzi ilipokuwa ikiongezeka sana, palitokea manungʼuniko kati ya Wayahudi wa Kiyunani, dhidi ya Waebrania kwa sababu wajane wao walisahaulika katika mgawanyo wa chakula wa kila siku.
V te dní pa, ko so se učenci množili, vstane godrnjanje Grkov zoper Hebrejce, da se pri vsakdanjej delitvi njih vdove zanemarjajo.
2 Wale mitume kumi na wawili wakakusanya wanafunzi wote pamoja wakasema, “Haitakuwa vyema sisi kuacha huduma ya neno la Mungu ili kuhudumu mezani.
In dvanajsteri pokličejo množico učencev, in rekó: To ne gre, da bi mi besedo Božjo opuščali, in oskrbljevali mize.
3 Kwa hiyo ndugu, chagueni watu saba miongoni mwenu, watu wenye sifa njema, waliojawa na Roho Mtakatifu na hekima, ambao tunaweza kuwakabidhi kazi hii,
Ozrite se torej, bratje, po sedmih možéh poštenih izmed sebe, kteri so polni Duha svetega in modrosti, da jih postavimo nad tem opravilom;
4 nasi tutatumia muda wetu kuomba na huduma ya neno.”
A mi se bomo molitve in službe besede držali.
5 Yale waliyosema yakawapendeza watu wote, nao wakamchagua Stefano (mtu aliyejawa na imani na Roho Mtakatifu) pamoja na Filipo, Prokoro, Nikanori, Timoni, Parmena na Nikolao, mwongofu kutoka Antiokia.
In ta beseda je bila vsej množici po godi; ter izvolijo Štefana, moža polnega vere in Duha svetega, in Filipa, in Prohora, in Nikanora, Timona in Parmena, in Nikolaja izpreobrnjenca iz Antijohije.
6 Wakawaleta watu hawa mbele ya mitume, nao wakawaombea na kuwawekea mikono juu yao.
Te postavijo pred aposteljne; in molivši, položé na-nje roke.
7 Neno la Mungu likazidi kuenea. Idadi ya wanafunzi ikazidi kuongezeka sana katika Yerusalemu hata makuhani wengi wakaitii ile imani.
In beseda Božja je rastla, in število učencev se je silno množilo v Jeruzalemu; tudi velika truma duhovnov je bila pokorna veri.
8 Stefano, akiwa amejaa neema na nguvu za Mungu, alifanya ishara na miujiza mikubwa miongoni mwa watu.
Štefan pa, poln vere in moči, delal je čudeže in velika znamenja med ljudmi.
9 Hata hivyo, ukainuka upinzani wa watu wa Sinagogi la Watu Huru (kama lilivyokuwa linaitwa), la Wayahudi wa Kirene na wa Iskanderia, na wengine kutoka Kilikia na Asia. Watu hawa wakaanza kupingana na Stefano.
In vstane jih nekaj iz shajališča, ktero se imenuje Libertinsko in Cirenejsko in Aleksandrinsko, in teh, kteri so bili iz Cilicije in Azije, in prepirali so se s Štefanom;
10 Lakini hawakuweza kushindana na hekima yake wala huyo Roho ambaye alisema kwake.
Ali niso se mogli upirati modrosti in Duhu, po kterem je govoril.
11 Ndipo kwa siri wakawashawishi watu fulani waseme, “Tumemsikia Stefano akisema maneno ya kufuru dhidi ya Mose na dhidi ya Mungu.”
Tedaj podšuntajo možé, kteri naj bi rekli: Slišali smo ga govoriti kletvine zoper Mojzesa in Boga.
12 Wakawachochea watu, wazee na walimu wa Sheria, nao wakamkamata Stefano wakamfikisha mbele ya baraza.
Ter nadražijo ljudstvo in starešine in pismarje, in napadejo in zgrabijo ga, in pripeljejo v zbor,
13 Wakaweka mashahidi wa uongo ambao walishuhudia wakisema, “Mtu huyu kamwe haachi kusema dhidi ya mahali hapa patakatifu na dhidi ya Sheria.
In postavijo krive priče, ktere so govorile: Ta človek ne neha govoriti kletvin zoper to sveto mesto in postavo.
14 Kwa maana tumemsikia akisema kwamba Yesu wa Nazareti atapaharibu mahali patakatifu na kubadili desturi zote tulizopewa na Mose.”
Slišali smo ga namreč, da pravi: Ta Jezus Nazarečan bo razdel to mesto, in premenil bo šege, ktere nam je izročil Mojzes.
15 Watu wote waliokuwa wameketi katika baraza wakimkazia macho Stefano, wakaona uso wake unangʼaa kama uso wa malaika.
In pogledavši na-nj vsi, kteri so sedeli v zboru, videli so obličje njegovo kakor obličje angelja.

< Matendo 6 >