< Matendo 6 >
1 Basi ikawa katika siku hizo, wakati idadi ya wanafunzi ilipokuwa ikiongezeka sana, palitokea manungʼuniko kati ya Wayahudi wa Kiyunani, dhidi ya Waebrania kwa sababu wajane wao walisahaulika katika mgawanyo wa chakula wa kila siku.
tasmin samayE ziSyANAM bAhulyAt prAtyahikadAnasya vizrANanai rbhinnadEzIyAnAM vidhavAstrIgaNa upEkSitE sati ibrIyalOkaiH sahAnyadEzIyAnAM vivAda upAtiSThat|
2 Wale mitume kumi na wawili wakakusanya wanafunzi wote pamoja wakasema, “Haitakuwa vyema sisi kuacha huduma ya neno la Mungu ili kuhudumu mezani.
tadA dvAdazaprEritAH sarvvAn ziSyAn saMgRhyAkathayan Izvarasya kathApracAraM parityajya bhOjanagavESaNam asmAkam ucitaM nahi|
3 Kwa hiyo ndugu, chagueni watu saba miongoni mwenu, watu wenye sifa njema, waliojawa na Roho Mtakatifu na hekima, ambao tunaweza kuwakabidhi kazi hii,
atO hE bhrAtRgaNa vayam EtatkarmmaNO bhAraM yEbhyO dAtuM zaknuma EtAdRzAn sukhyAtyApannAn pavitrENAtmanA jnjAnEna ca pUrNAn sapprajanAn yUyaM svESAM madhyE manOnItAn kuruta,
4 nasi tutatumia muda wetu kuomba na huduma ya neno.”
kintu vayaM prArthanAyAM kathApracArakarmmaNi ca nityapravRttAH sthAsyAmaH|
5 Yale waliyosema yakawapendeza watu wote, nao wakamchagua Stefano (mtu aliyejawa na imani na Roho Mtakatifu) pamoja na Filipo, Prokoro, Nikanori, Timoni, Parmena na Nikolao, mwongofu kutoka Antiokia.
EtasyAM kathAyAM sarvvE lOkAH santuSTAH santaH svESAM madhyAt stiphAnaH philipaH prakharO nikAnOr tIman parmmiNA yihUdimatagrAhI-AntiyakhiyAnagarIyO nikalA EtAn paramabhaktAn pavitrENAtmanA paripUrNAn sapta janAn
6 Wakawaleta watu hawa mbele ya mitume, nao wakawaombea na kuwawekea mikono juu yao.
prEritAnAM samakSam Anayan, tatastE prArthanAM kRtvA tESAM ziraHsu hastAn Arpayan|
7 Neno la Mungu likazidi kuenea. Idadi ya wanafunzi ikazidi kuongezeka sana katika Yerusalemu hata makuhani wengi wakaitii ile imani.
aparanjca Izvarasya kathA dEzaM vyApnOt vizESatO yirUzAlami nagarE ziSyANAM saMkhyA prabhUtarUpENAvarddhata yAjakAnAM madhyEpi bahavaH khrISTamatagrAhiNO'bhavan|
8 Stefano, akiwa amejaa neema na nguvu za Mungu, alifanya ishara na miujiza mikubwa miongoni mwa watu.
stiphAnO vizvAsEna parAkramENa ca paripUrNaH san lOkAnAM madhyE bahuvidham adbhutam AzcaryyaM karmmAkarOt|
9 Hata hivyo, ukainuka upinzani wa watu wa Sinagogi la Watu Huru (kama lilivyokuwa linaitwa), la Wayahudi wa Kirene na wa Iskanderia, na wengine kutoka Kilikia na Asia. Watu hawa wakaanza kupingana na Stefano.
tEna libarttinIyanAmnA vikhyAtasagghasya katipayajanAH kurINIyasikandarIya-kilikIyAzIyAdEzIyAH kiyantO janAzcOtthAya stiphAnEna sArddhaM vyavadanta|
10 Lakini hawakuweza kushindana na hekima yake wala huyo Roho ambaye alisema kwake.
kintu stiphAnO jnjAnEna pavitrENAtmanA ca IdRzIM kathAM kathitavAn yasyAstE ApattiM karttuM nAzaknuvan|
11 Ndipo kwa siri wakawashawishi watu fulani waseme, “Tumemsikia Stefano akisema maneno ya kufuru dhidi ya Mose na dhidi ya Mungu.”
pazcAt tai rlObhitAH katipayajanAH kathAmEnAm akathayan, vayaM tasya mukhatO mUsA Izvarasya ca nindAvAkyam azrauSma|
12 Wakawachochea watu, wazee na walimu wa Sheria, nao wakamkamata Stefano wakamfikisha mbele ya baraza.
tE lOkAnAM lOkaprAcInAnAm adhyApakAnAnjca pravRttiM janayitvA stiphAnasya sannidhim Agatya taM dhRtvA mahAsabhAmadhyam Anayan|
13 Wakaweka mashahidi wa uongo ambao walishuhudia wakisema, “Mtu huyu kamwe haachi kusema dhidi ya mahali hapa patakatifu na dhidi ya Sheria.
tadanantaraM katipayajanESu mithyAsAkSiSu samAnItESu tE'kathayan ESa jana EtatpuNyasthAnavyavasthayO rnindAtaH kadApi na nivarttatE|
14 Kwa maana tumemsikia akisema kwamba Yesu wa Nazareti atapaharibu mahali patakatifu na kubadili desturi zote tulizopewa na Mose.”
phalatO nAsaratIyayIzuH sthAnamEtad ucchinnaM kariSyati mUsAsamarpitam asmAkaM vyavaharaNam anyarUpaM kariSyati tasyaitAdRzIM kathAM vayam azRNuma|
15 Watu wote waliokuwa wameketi katika baraza wakimkazia macho Stefano, wakaona uso wake unangʼaa kama uso wa malaika.
tadA mahAsabhAsthAH sarvvE taM prati sthirAM dRSTiM kRtvA svargadUtamukhasadRzaM tasya mukham apazyan|