< Matendo 6 >

1 Basi ikawa katika siku hizo, wakati idadi ya wanafunzi ilipokuwa ikiongezeka sana, palitokea manungʼuniko kati ya Wayahudi wa Kiyunani, dhidi ya Waebrania kwa sababu wajane wao walisahaulika katika mgawanyo wa chakula wa kila siku.
A w tych dniach, gdy liczba uczniów wzrastała, helleniści zaczęli szemrać przeciwko Żydom, że zaniedbywano w codziennym posługiwaniu ich wdowy.
2 Wale mitume kumi na wawili wakakusanya wanafunzi wote pamoja wakasema, “Haitakuwa vyema sisi kuacha huduma ya neno la Mungu ili kuhudumu mezani.
Wtedy dwunastu, zwoławszy [całe] mnóstwo uczniów, powiedziało: Nie jest rzeczą słuszną, żebyśmy porzucili słowo Boże, a obsługiwali stoły.
3 Kwa hiyo ndugu, chagueni watu saba miongoni mwenu, watu wenye sifa njema, waliojawa na Roho Mtakatifu na hekima, ambao tunaweza kuwakabidhi kazi hii,
Upatrzcie więc, bracia, spośród siebie siedmiu mężczyzn, mających dobre świadectwo, pełnych Ducha Świętego i mądrości, którym zlecimy tę sprawę.
4 nasi tutatumia muda wetu kuomba na huduma ya neno.”
My zaś oddamy się modlitwie i posłudze słowa.
5 Yale waliyosema yakawapendeza watu wote, nao wakamchagua Stefano (mtu aliyejawa na imani na Roho Mtakatifu) pamoja na Filipo, Prokoro, Nikanori, Timoni, Parmena na Nikolao, mwongofu kutoka Antiokia.
I spodobało się to całej gromadzie [zebranych]. Wybrali więc Szczepana, męża pełnego wiary i Ducha Świętego, Filipa, Prochora, Nikanora, Tymona, Parmenasa i Mikołaja, prozelitę z Antiochii.
6 Wakawaleta watu hawa mbele ya mitume, nao wakawaombea na kuwawekea mikono juu yao.
Przedstawili ich apostołom, którzy modląc się, położyli na nich ręce.
7 Neno la Mungu likazidi kuenea. Idadi ya wanafunzi ikazidi kuongezeka sana katika Yerusalemu hata makuhani wengi wakaitii ile imani.
I rozszerzało się słowo Boże, i liczba uczniów w Jerozolimie bardzo się pomnażała; także bardzo wielu kapłanów stawało się posłusznych wierze.
8 Stefano, akiwa amejaa neema na nguvu za Mungu, alifanya ishara na miujiza mikubwa miongoni mwa watu.
A Szczepan, pełen wiary i mocy, czynił cuda i wielkie znaki wśród ludzi.
9 Hata hivyo, ukainuka upinzani wa watu wa Sinagogi la Watu Huru (kama lilivyokuwa linaitwa), la Wayahudi wa Kirene na wa Iskanderia, na wengine kutoka Kilikia na Asia. Watu hawa wakaanza kupingana na Stefano.
Wtedy niektórzy z synagogi zwanej [synagogą] Libertynów i Cyrenejczyków, i Aleksandryjczyków oraz tych, którzy pochodzili z Cylicji i Azji, wystąpili do rozprawy ze Szczepanem.
10 Lakini hawakuweza kushindana na hekima yake wala huyo Roho ambaye alisema kwake.
Lecz nie mogli sprostać mądrości i duchowi, z którym mówił.
11 Ndipo kwa siri wakawashawishi watu fulani waseme, “Tumemsikia Stefano akisema maneno ya kufuru dhidi ya Mose na dhidi ya Mungu.”
Podstawili więc ludzi, którzy zeznali: Słyszeliśmy, jak mówił bluźnierstwa przeciwko Mojżeszowi i przeciwko Bogu.
12 Wakawachochea watu, wazee na walimu wa Sheria, nao wakamkamata Stefano wakamfikisha mbele ya baraza.
I tak podburzyli lud, starszych i uczonych w Piśmie; a gdy przybiegli do niego, porwali go i przyprowadzili do Rady.
13 Wakaweka mashahidi wa uongo ambao walishuhudia wakisema, “Mtu huyu kamwe haachi kusema dhidi ya mahali hapa patakatifu na dhidi ya Sheria.
I podstawili fałszywych świadków, którzy zeznali: Ten człowiek nie przestaje mówić bluźnierstw przeciwko temu świętemu miejscu i [przeciwko] prawu.
14 Kwa maana tumemsikia akisema kwamba Yesu wa Nazareti atapaharibu mahali patakatifu na kubadili desturi zote tulizopewa na Mose.”
Słyszeliśmy bowiem, jak mówił, że ten Jezus z Nazaretu zburzy to miejsce i zmieni zwyczaje, które nam przekazał Mojżesz.
15 Watu wote waliokuwa wameketi katika baraza wakimkazia macho Stefano, wakaona uso wake unangʼaa kama uso wa malaika.
A wszyscy, którzy zasiadali w Radzie, przyglądali mu się uważnie i zobaczyli, że jego twarz jest jak oblicze anioła.

< Matendo 6 >