< Matendo 6 >
1 Basi ikawa katika siku hizo, wakati idadi ya wanafunzi ilipokuwa ikiongezeka sana, palitokea manungʼuniko kati ya Wayahudi wa Kiyunani, dhidi ya Waebrania kwa sababu wajane wao walisahaulika katika mgawanyo wa chakula wa kila siku.
Neil päevil, kui jüngrite arv kasvas, hakkasid Kreeka päritolu juudid kurtma Heebrea päritolu juutide üle, et igapäevase toidu jagamisel nende leskedega ei arvestata.
2 Wale mitume kumi na wawili wakakusanya wanafunzi wote pamoja wakasema, “Haitakuwa vyema sisi kuacha huduma ya neno la Mungu ili kuhudumu mezani.
Siis kutsusid need kaksteist kokku kõik jüngrid ja sõnasid: „See ei oleks õige, kui jätaksime Jumala sõnaga teenimise unarusse, et teenida toidulauas.
3 Kwa hiyo ndugu, chagueni watu saba miongoni mwenu, watu wenye sifa njema, waliojawa na Roho Mtakatifu na hekima, ambao tunaweza kuwakabidhi kazi hii,
Seepärast, vennad ja õed, valige endi hulgast seitse meest, kes on täis Püha Vaimu ja tarkust. Me anname selle vastutuse neile üle
4 nasi tutatumia muda wetu kuomba na huduma ya neno.”
ja pühendume ise palvele ja sõna teenimisele.“
5 Yale waliyosema yakawapendeza watu wote, nao wakamchagua Stefano (mtu aliyejawa na imani na Roho Mtakatifu) pamoja na Filipo, Prokoro, Nikanori, Timoni, Parmena na Nikolao, mwongofu kutoka Antiokia.
See ettepanek meeldis kõigile. Nad valisid Stefanose, mehe täis usku ja Püha Vaimu, samuti Filippuse, Prokorose, Nikanori, Timoni, Parmenase ja Nikolase Antiookiast, kes oli pöördunud juudiusku.
6 Wakawaleta watu hawa mbele ya mitume, nao wakawaombea na kuwawekea mikono juu yao.
Need mehed tõid nad apostlite ette, ja kui nad palvetasid, panid nad oma käed nende peale.
7 Neno la Mungu likazidi kuenea. Idadi ya wanafunzi ikazidi kuongezeka sana katika Yerusalemu hata makuhani wengi wakaitii ile imani.
Nõndaviisi levis Jumala sõna. Jüngrite arv Jeruusalemmas kasvas väga suureks; ka paljud preestrid võtsid usu omaks.
8 Stefano, akiwa amejaa neema na nguvu za Mungu, alifanya ishara na miujiza mikubwa miongoni mwa watu.
Aga Stefanos, täis Jumala armu ja väge, tegi imetegusid ja suuri tunnustähti inimeste hulgas.
9 Hata hivyo, ukainuka upinzani wa watu wa Sinagogi la Watu Huru (kama lilivyokuwa linaitwa), la Wayahudi wa Kirene na wa Iskanderia, na wengine kutoka Kilikia na Asia. Watu hawa wakaanza kupingana na Stefano.
Aga vastuseis kasvas vabakslastute sünagoogi liikmete hulgas, kelle seas olid juudid Küreenest ja Aleksandriast, samuti Kiliikia ja Aasia provintsidest. Need mehed püüdsid Stefanosega vaielda,
10 Lakini hawakuweza kushindana na hekima yake wala huyo Roho ambaye alisema kwake.
ent ei suutnud vastu seista tarkusele ega Vaimule, kes tema läbi rääkis.
11 Ndipo kwa siri wakawashawishi watu fulani waseme, “Tumemsikia Stefano akisema maneno ya kufuru dhidi ya Mose na dhidi ya Mungu.”
Siis nad ärgitasid mõndasid ütlema: „Me oleme kuulnud Stefanost rääkivat teotavaid sõnu Moosese ja Jumala vastu.“
12 Wakawachochea watu, wazee na walimu wa Sheria, nao wakamkamata Stefano wakamfikisha mbele ya baraza.
Ja nõnda nad ässitasid rahvast, vanemaid ja kirjatundjaid. Nad võtsid Stefanose kinni ja viisid ta Suurkohtu ette.
13 Wakaweka mashahidi wa uongo ambao walishuhudia wakisema, “Mtu huyu kamwe haachi kusema dhidi ya mahali hapa patakatifu na dhidi ya Sheria.
Nad tõid kohale valetunnistajaid, kes kinnitasid: „See mees ei lakka rääkimast püha paiga ja Seaduse vastu,
14 Kwa maana tumemsikia akisema kwamba Yesu wa Nazareti atapaharibu mahali patakatifu na kubadili desturi zote tulizopewa na Mose.”
sest me oleme kuulnud teda ütlemas, et Naatsareti Jeesus hävitab selle koha ja muudab ära Moosese antud kombed.“
15 Watu wote waliokuwa wameketi katika baraza wakimkazia macho Stefano, wakaona uso wake unangʼaa kama uso wa malaika.
Ja kui kõik Suurkohtus istujad Stefanost tähelepanelikult vaatasid, nägid nad tema palge olevat otsekui inglil.