< Matendo 6 >
1 Basi ikawa katika siku hizo, wakati idadi ya wanafunzi ilipokuwa ikiongezeka sana, palitokea manungʼuniko kati ya Wayahudi wa Kiyunani, dhidi ya Waebrania kwa sababu wajane wao walisahaulika katika mgawanyo wa chakula wa kila siku.
Men da i de Dage Disciplenes Antal forøgedes, begyndte Hellenisterne at knurre imod Hebræerne", fordi deres Enker bleve tilsidesatte ved den daglige Uddeling.
2 Wale mitume kumi na wawili wakakusanya wanafunzi wote pamoja wakasema, “Haitakuwa vyema sisi kuacha huduma ya neno la Mungu ili kuhudumu mezani.
Da sammenkaldte de tolv Disciplenes Skare og sagde: "Det huer os ikke at forlade Guds Ord for at tjene ved Bordene.
3 Kwa hiyo ndugu, chagueni watu saba miongoni mwenu, watu wenye sifa njema, waliojawa na Roho Mtakatifu na hekima, ambao tunaweza kuwakabidhi kazi hii,
Udser derfor, Brødre! iblandt eder syv Mænd, som have godt Vidnesbyrd og ere fulde af Ånd og Visdom; dem ville vi så indsætte til denne Gerning.
4 nasi tutatumia muda wetu kuomba na huduma ya neno.”
Men vi ville holde trolig ved i Bønnen og Ordets Tjeneste."
5 Yale waliyosema yakawapendeza watu wote, nao wakamchagua Stefano (mtu aliyejawa na imani na Roho Mtakatifu) pamoja na Filipo, Prokoro, Nikanori, Timoni, Parmena na Nikolao, mwongofu kutoka Antiokia.
Og denne Tale behagede hele Mængden; og de udvalgte Stefanus. en Mand fuld af Tro og den Helligånd, og Filip og Prokorus og Nikaiior og Timon og Parmenas og Nikolaus, en Proselyt fra Antiokia;
6 Wakawaleta watu hawa mbele ya mitume, nao wakawaombea na kuwawekea mikono juu yao.
dem stillede de frem for Apostlene; og disse bade og lagde Hænderne på dem.
7 Neno la Mungu likazidi kuenea. Idadi ya wanafunzi ikazidi kuongezeka sana katika Yerusalemu hata makuhani wengi wakaitii ile imani.
Og Guds Ord havde Fremgang og Disciplenes Tal forøgedes meget i Jerusalem; og en stor Mængde af Præsterne adløde Troen.
8 Stefano, akiwa amejaa neema na nguvu za Mungu, alifanya ishara na miujiza mikubwa miongoni mwa watu.
Men Stefanus, fuld af Nåde og Kraft, gjorde Undere og store Tegn iblandt Folket,
9 Hata hivyo, ukainuka upinzani wa watu wa Sinagogi la Watu Huru (kama lilivyokuwa linaitwa), la Wayahudi wa Kirene na wa Iskanderia, na wengine kutoka Kilikia na Asia. Watu hawa wakaanza kupingana na Stefano.
Da stod der nogle frem af den Synagoge, som kaldes de frigivnes og Kyrenæernes og Aleksandrinernes, og nogle af dem fra Kilikien og Asien, og de tvistedes med Stefanus.
10 Lakini hawakuweza kushindana na hekima yake wala huyo Roho ambaye alisema kwake.
Og de kunde ikke modstå den Visdom og den Ånd, som han talte af.
11 Ndipo kwa siri wakawashawishi watu fulani waseme, “Tumemsikia Stefano akisema maneno ya kufuru dhidi ya Mose na dhidi ya Mungu.”
Da fik de hemmeligt nogle Mænd til at sige: "Vi have hørt ham tale bespottelige Ord imod Moses og imod Gud."
12 Wakawachochea watu, wazee na walimu wa Sheria, nao wakamkamata Stefano wakamfikisha mbele ya baraza.
Og de ophidsede Folket og de Ældste og de skriftkloge, og de overfaldt ham og slæbte ham med sig og førte ham for Rådet;
13 Wakaweka mashahidi wa uongo ambao walishuhudia wakisema, “Mtu huyu kamwe haachi kusema dhidi ya mahali hapa patakatifu na dhidi ya Sheria.
og de fremstillede falske Vidner, som sagde: "Dette Menneske holder ikke op med at tale Ord imod dette hellige Sted og imod Loven.
14 Kwa maana tumemsikia akisema kwamba Yesu wa Nazareti atapaharibu mahali patakatifu na kubadili desturi zote tulizopewa na Mose.”
Thi vi have hørt ham sige, at denne Jesus af Nazareth skal nedbryde dette Sted og forandre de Skikke, som Moses har overgivet os."
15 Watu wote waliokuwa wameketi katika baraza wakimkazia macho Stefano, wakaona uso wake unangʼaa kama uso wa malaika.
Og alle de, som sade i Rådet, stirrede på ham, og de så hans Ansigt som en Engels Ansigt.