< Matendo 5 >

1 Lakini mtu mmoja jina lake Anania pamoja na mkewe Safira waliuza kiwanja.
But a certain man named Ananias, together with Sapphira his wife,
2 Huku mkewe akijua kikamilifu, Anania alificha sehemu ya fedha alizopata, akaleta kiasi kilichobaki na kukiweka miguuni pa mitume.
sold a possession, and secreted part of the price, his wife also being conscious to it; and bringing: some part, laid it at the feet of the apostles.
3 Petro akamuuliza, “Anania, mbona Shetani ameujaza moyo wako ili kumwambia uongo Roho Mtakatifu, ukaficha sehemu ya fedha ulizopata kutokana na kiwanja?
But Peter said, Ananias, why hath Satan so filled thine heart, that thou shouldst lie to the holy Ghost, and keep back part of the price of the land?
4 Je, kabla hujauza hicho kiwanja si kilikuwa mali yako? Hata baada ya kukiuza, fedha ulizopata si zilikuwa kwenye uwezo wako? Kwa nini basi umewaza hila hii moyoni mwako kufanya jambo kama hili? Wewe hukumwambia uongo mwanadamu bali Mungu.”
While it remained, did it not remain thy own? and when sold, was it not in thy own power? what is the meaning that thou hast taken this into thine heart? Thou hast not lyed to men, but to God.
5 Anania aliposikia maneno haya akaanguka chini na kufa. Hofu kuu ikawapata wote waliosikia jambo lililokuwa limetukia.
And Ananias at the hearing of these words fell down and expired: and great fear came on all that heard these things.
6 Vijana wakaja, wakaufunga mwili wake sanda, wakamchukua nje kumzika.
And some of the young men arose, and wrapped him up; and they carried him out, and buried him.
7 Saa tatu baadaye mkewe Anania akaingia, naye hana habari ya mambo yaliyotukia.
And about the space of three hours after, his wife also came in, not knowing what had happened.
8 Petro akamuuliza, “Niambie, je, mliuza kiwanja kwa thamani hii?” Akajibu, “Ndiyo, tuliuza kwa thamani hiyo.”
And Peter said to her, Tell me whether ye sold the land for so much. And she said, Yes, for so much.
9 Ndipo Petro akamwambia, “Imekuwaje mkakubaliana kumjaribu Roho wa Bwana? Tazama! Nyayo za vijana waliomzika mumeo ziko mlangoni, wewe nawe watakuchukua nje.”
Then Peter said unto her, Wherefore have ye agreed together to tempt the Spirit of the Lord? behold the feet of those, who have been burying thy husband, now at the door, and they shall carry thee out.
10 Saa ile ile akaanguka chini miguuni mwake na kufa. Nao wale vijana wakaingia, wakamkuta amekufa, wakamchukua wakamzika kando ya mumewe.
And immediately she fell down at his feet and expired: and the young men coming in found her dead, and they carried her out and buried her by her husband.
11 Hofu kuu ikalipata kanisa lote pamoja na watu wote waliosikia juu ya matukio haya.
And great fear came upon the whole assembly, and upon all that heard these things.
12 Mitume wakafanya ishara nyingi na miujiza miongoni mwa watu. Walioamini wote walikuwa wakikusanyika katika ukumbi wa Solomoni.
And by the hands of the apostles were many signs and wonders done among the people: And they all met with one accord in Solomon's portico:
13 Hakuna mtu mwingine aliyethubutu kuambatana nao ijapokuwa waliheshimiwa sana na watu.
but no other presumed to join himself to them; however the people magnified them.
14 Hata hivyo, waliomwamini Bwana wakazidi kuongezeka, wanaume na wanawake.
And true believers were the more willingly added to the Lord, even multitudes both of men and women.
15 Hata wakawa wanawaleta wagonjwa na kuwalaza kwenye magodoro na kwenye vitanda barabarani ili yamkini Petro akipita kivuli chake kiwaguse baadhi yao.
insomuch that they brought the sick out into the streets, and laid them on beds and couches, that at lest the shadow of Peter, as he came by, might pass over some of them.
16 Pia watu wakakusanyika kutoka miji iliyokuwa karibu na Yerusalemu, wakileta wagonjwa na watu walioteswa na pepo wachafu. Hao wote wakaponywa.
And a great number out of the cities round about also came together to Jerusalem, bringing those that were infirm and that were troubled with impure spirits; and they were all cured.
17 Kisha kuhani mkuu na wenzake wote waliokuwa pamoja naye, waliokuwa wa kundi la Masadukayo, wakajawa na wivu.
Then the high priest rose up, and all that were with him, (being of the sect of the sadducees, ) and were filled with rage:
18 Wakawakamata mitume na kuwatia gerezani.
and laid their hands on the apostles, and put them in the public prison.
19 Lakini wakati wa usiku, malaika wa Bwana akaja, akafungua milango ya gereza na akawatoa nje. Akawaambia,
But an angel of the Lord opened the doors of the prison by night, and having brought them out said,
20 “Nendeni, mkasimame Hekaluni mkawaambie watu maneno yote ya uzima huu mpya.”
"Go stand and speak in the temple to the people all the words of this life."
21 Waliposikia haya wakaenda Hekaluni alfajiri wakaendelea kufundisha watu. Kuhani mkuu na wale waliokuwa pamoja nao walipowasili, alikusanya baraza na wazee wote wa Israeli wakatuma wale mitume waletwe kutoka gerezani.
And hearing this, they went early in the morning into the temple and taught the people. But the high priest being come, and they that were with him, to the council-chamber, they called together the Sanhedrim, and all the senate of the children of Israel, and sent orders to the prison that they should be brought before them.
22 Lakini wale walinzi wa Hekalu walipokwenda gerezani hawakuwakuta mitume mle. Kwa hiyo wakarudi na kutoa habari.
But when the officers came they found them not in the prison: so they returned,
23 Wakasema, “Tumekuta milango ya gereza imefungwa sawasawa na askari wa gereza wamesimama nje ya mlango, lakini tulipofungua milango hakuwepo mtu yeyote ndani.”
and told them, saying, the prison we found shut with all safety, and the keepers standing without before the doors: but when we opened them, we found no body within.
24 Basi mkuu wa walinzi wa Hekalu na viongozi wa makuhani waliposikia haya, wakafadhaika na kushangaa sana kwa ajili yao kwamba jambo hili litakuwaje.
Now when the high priest, and the captain of the temple, and the chief priests heard these words, they were in doubt concerning them, what this would come to;
25 Ndipo mtu mmoja akaja akawaambia, “Tazameni watu mliowatia gerezani wako Hekaluni wakiwafundisha watu.”
when there came one and told them, saying, behold, the men whom ye put in prison, are in the temple teaching the people.
26 Ndipo yule mkuu wa walinzi wa Hekalu wakaenda pamoja na askari wakawaleta wale mitume, lakini bila ghasia kwa sababu waliogopa kupigwa mawe na watu.
Then the captain went with the officers and brought them, but not with violence; for they were afraid of the people least they should be stoned:
27 Wakiisha kuwaleta mitume wakawaamuru kusimama mbele ya baraza ili kuhani mkuu awahoji.
and when they had brought them, they set them before the council. And the high priest asked them,
28 “Tuliwaonya kwa nguvu msifundishe kwa jina hili, lakini ninyi mmeijaza Yerusalemu yote mafundisho yenu na tena mmekusudia kuleta damu ya mtu huyu juu yetu.”
saying, Did not we strictly charge you not to teach in this name? and behold ye have filled Jerusalem with your doctrine, and would bring this man's blood upon us.
29 Petro na wale mitume wengine wakajibu, “Imetupasa kumtii Mungu kuliko wanadamu.
But Peter, and the other apostles, answered, and said, We ought to obey God rather than men.
30 Mungu wa baba zetu alimfufua Yesu kutoka kwa wafu, ambaye ninyi mlimuua kwa kumtundika kwenye msalaba.
The God of our fathers hath raised up Jesus whom ye slew and hanged on a tree.
31 Mungu alimtukuza, akamweka mkono wake wa kuume kuwa Kiongozi na Mwokozi ili awape Israeli toba na msamaha wa dhambi.
Him hath God exalted with his right hand as a prince and saviour, to give repentance to Israel, and remission of sins:
32 Nasi tu mashahidi wa mambo haya, vivyo hivyo na Roho Mtakatifu ambaye Mungu amewapa wale wanaomtii.”
and we are his witnesses of what we declare; and so is the holy Spirit, whom God hath given to them that obey Him.
33 Wale wajumbe wa baraza la wazee waliposikia haya, walijawa na ghadhabu, wakataka kuwaua mitume.
And when they heard this, they were cut to the heart, and took counsel to put them to death.
34 Lakini Farisayo mmoja, jina lake Gamalieli, aliyekuwa mwalimu wa sheria, aliyeheshimiwa na watu wote, akasimama mbele ya baraza akaamuru mitume watolewe nje kwa muda.
But a certain pharisee, named Gamaliel, a doctor of the law, held in much esteem by all the people, stood up in the council, and ordered the apostles to be taken out a little while; and then he said unto them,
35 Ndipo alipowaambia wajumbe wa baraza, “Enyi watu wa Israeli, fikirini kwa uangalifu mnayotaka kuwatendea watu hawa.
Men of Israel, take heed to yourselves, what ye are about to do, as to these men.
36 Kwa maana wakati uliopita, aliinuka mtu mmoja jina lake Theuda, alijidai kuwa yeye ni mtu maarufu, akapata wafuasi wapatao 400 walioambatana naye. Lakini aliuawa, na wafuasi wake wote wakatawanyika, wakawa si kitu.
For some time ago one Theudas arose, pretending to be some extraordinary person, to whom was joined a number of men, about four hundred: who was slain, and all that followed him were dispersed and came to nothing.
37 Baada yake, alitokea Yuda Mgalilaya wakati wa kuorodhesha watu, naye akaongoza kundi la watu kuasi. Yeye pia aliuawa, nao wafuasi wake wakatawanyika.
After him arose Judas the Galilean, at the time of the registring, and drew much people after him: but he also perished, and all that followed him were dispersed.
38 Kwa hiyo, kwa habari ya jambo hili nawashauri, jiepusheni na watu hawa. Waacheni waende zao! Kwa maana kama kusudi lao na shughuli yao imetokana na mwanadamu, haitafanikiwa.
And therefore as to the present affair I advise you to refrain from these men and let them alone: for if this counsel or this work be of men, it will come to nothing;
39 Lakini ikiwa imetoka kwa Mungu, hamtaweza kuwazuia watu hawa. Badala yake mtajikuta mnapigana na Mungu.”
but if it be of God, ye cannot defeat it, least ye be found fighting even against God.
40 Wakapokea ushauri wa Gamalieli. Wakawaita mitume ndani, wakaamuru wachapwe mijeledi, kisha wakawaagiza wasinene tena kwa jina la Yesu, wakawaachia waende zao.
So they took his advice, and having called for the apostles and scourged them, they charged them not to speak in the name of Jesus, and let them go.
41 Nao mitume wakatoka nje ya baraza, wakiwa wamejaa furaha kwa sababu wamehesabiwa kustahili kupata aibu kwa ajili ya jina la Yesu.
And they departed from the presence of the council rejoicing that they were counted worthy to suffer disgrace for his name.
42 Kila siku, Hekaluni na nyumba kwa nyumba, hawakuacha kufundisha na kuhubiri habari njema kwamba Yesu ndiye Kristo.
And every day in the temple and from house to house they ceased not from teaching and preaching that Jesus was the Christ.

< Matendo 5 >