< Matendo 4 >
1 Wakati Petro na Yohana walipokuwa wakisema na watu, makuhani, mkuu wa walinzi wa Hekalu na Masadukayo wakawajia,
Dok su oni još govorili narodu, priđu im svećenici, hramski zapovjednik i saduceji,
2 huku wakiwa wamekasirika sana kwa sababu mitume walikuwa wanawafundisha watu na kuhubiri kwamba kuna ufufuo wa wafu ndani ya Yesu.
ozlovoljeni što uče narod i navješćuju - u Isusu - uskrsnuće od mrtvih;
3 Wakawakamata Petro na Yohana na kuwatia gerezani mpaka kesho yake kwa kuwa ilikuwa jioni.
pograbe ih i bace u tamnicu do sutra jer već bijaše večer.
4 Lakini wengi waliosikia lile neno waliamini, idadi yao ilikuwa yapata wanaume 5,000.
Ipak mnogi od onih koji su čuli Riječ, povjerovaše te broj vjernika poraste nekako do pet tisuća.
5 Kesho yake, viongozi wa Kiyahudi, wazee na walimu wa sheria wakakusanyika Yerusalemu.
Sutradan se sastadoše u Jeruzalemu glavari, starješine i pismoznanci -
6 Walikuwepo kuhani mkuu Anasi, Kayafa, Yohana, Iskanda, na wengi wa jamaa ya kuhani mkuu.
i veliki svećenik Ana, i Kajfa, i Ivan, i Aleksandar, i svi od roda velikosvećeničkoga.
7 Baada ya kuwasimamisha Petro na Yohana katikati yao, wakawauliza, “Ni kwa uwezo gani au kwa jina la nani mmefanya jambo hili?”
Izvedoše apostole preda se pa ih stadoše ispitivati: “Kojom snagom ili po kojem imenu vi to učiniste?”
8 Petro, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akajibu, “Enyi watawala na wazee wa watu,
Onda Petar pun Duha Svetoga reče: “Glavari narodni i starješine!
9 kama leo tukihojiwa kwa habari ya mambo mema aliyotendewa yule kiwete na kuulizwa jinsi alivyoponywa,
Zar mi danas odgovaramo zbog dobra djela učinjena bolesnu čovjeku? Po kome je ovaj spašen?
10 ijulikane kwenu nyote na kwa watu wote wa Israeli kwamba: Ni kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye ninyi mlimsulubisha lakini Mungu akamfufua kutoka kwa wafu, kwa jina hilo mtu huyu anasimama mbele yenu akiwa mzima kabisa.
Neka bude znano svima vama i svemu narodu Izraelovu: po imenu Isusa Krista Nazarećanina, kojega ste vi raspeli, a kojega Bog uskrisi od mrtvih! Po njemu ovaj stoji pred vama zdrav!
11 Huyu ndiye “‘jiwe ambalo ninyi wajenzi mlilikataa, ambalo limekuwa jiwe kuu la pembeni.’
On je onaj kamen koji vi graditelji odbaciste, ali koji postade kamen zaglavni.
12 Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hakuna jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.”
I nema ni u kome drugom spasenja. Nema uistinu pod nebom drugoga imena dana ljudima po kojemu se možemo spasiti.”
13 Wale viongozi na wazee walipoona ujasiri wa Petro na Yohana na kujua ya kuwa walikuwa watu wa kawaida, wasio na elimu, walishangaa sana, wakatambua kwamba hawa watu walikuwa na Yesu.
Kad vidješe neustrašivost Petrovu i Ivanovu, a znajući da su to ljudi nepismeni i neuki, bijahu u čudu; znali su ih, da bijahu s Isusom, ali
14 Lakini kwa kuwa walikuwa wanamwona yule kiwete aliyeponywa amesimama pale pamoja nao, hawakuweza kusema lolote kuwapinga.
videći gdje s njima stoji izliječeni čovjek, nisu mogli ništa protusloviti.
15 Wakawaamuru watoke nje ya Baraza la Wayahudi wakati wakisemezana jambo hilo wao kwa wao.
Stoga zapovjediše da izađu iz vijećnice pa stadoše raspravljati:
16 Wakaulizana, “Tuwafanyie nini watu hawa? Hatuwezi kukanusha muujiza huu mkubwa walioufanya ambao ni dhahiri kwa kila mtu Yerusalemu.
“Što ćemo s tim ljudima? Ta učinili su očit znak, poznat svim Jeruzalemcima, ne možemo ga nijekati;
17 Lakini ili kuzuia jambo hili lisiendelee kuenea zaidi kwa watu, ni lazima tuwaonye watu hawa ili wasiseme tena na mtu yeyote kwa jina la Yesu.”
ali da se još više ne razglasi u narod, zaprijetimo im da nikomu živom o tom Imenu više ne govore.”
18 Kisha wakawaita tena ndani na kuwaamuru wasiseme wala kufundisha kamwe kwa hili jina la Yesu.
Pozvaše ih i zapovjediše im da podnipošto ne zbore niti naučavaju u ime Isusovo.
19 Lakini Petro na Yohana wakajibu, “Amueni ninyi wenyewe iwapo ni haki mbele za Mungu kuwatii ninyi kuliko kumtii Mungu.
Ali im Petar i Ivan odgovoriše: “Sudite je li pred Bogom pravo slušati radije vas nego Boga.
20 Lakini sisi hatuwezi kuacha kusema yale tuliyoyaona na kuyasikia.”
Mi doista ne možemo ne govoriti što vidjesmo i čusmo.”
21 Baada ya vitisho vingi, wakawaacha waende zao. Hawakuona njia yoyote ya kuwaadhibu, kwa sababu ya watu, kwa kuwa watu wote walikuwa wakimsifu Mungu kwa kile kilichokuwa kimetukia.
Ali oni ne našavši kako da ih kazne, opet im zaprijete pa ih otpuste poradi naroda jer su svi slavili Boga zbog onoga što se dogodilo.
22 Kwa kuwa umri wa yule mtu aliyekuwa ameponywa kwa muujiza ulikuwa zaidi ya miaka arobaini.
Jer čovjeku na kom se dogodi čudo ozdravljenja bijaše više od četrdeset godina.
23 Punde Petro na Yohana walipoachiliwa, walirudi kwa waumini wenzao wakawaeleza waliyoambiwa na viongozi wa makuhani na wazee.
Otpušteni, odoše svojima i javiše što im rekoše veliki svećenici i starješine.
24 Watu waliposikia hayo, wakainua sauti zao, wakamwomba Mungu kwa pamoja, wakisema, “Bwana Mwenyezi, uliyeziumba mbingu na nchi na bahari, na vitu vyote vilivyomo.
Kad su oni to čuli, jednodušno podigoše glas k Bogu i rekoše: “Gospodine, ti si stvorio nebo i zemlju i more i sve što je u njima!
25 Wewe ulisema kwa Roho Mtakatifu kupitia kwa kinywa cha baba yetu Daudi, mtumishi wako, ukasema: “‘Mbona mataifa wanaghadhibika, na kabila za watu zinawaza ubatili?
Ti si na usta oca našega, sluge svoga Davida, po Duhu Svetom rekao: Zašto se bune narodi, zašto puci ludosti snuju?
26 Wafalme wa dunia wamejipanga, na watawala wanakusanyika pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.’
Ustaju kraljevi zemaljski, Knezovi se rotÄe protiv Gospodina i protiv Pomazanika njegova.
27 Ni kweli Herode na Pontio Pilato pamoja na watu wa Mataifa na Waisraeli, walikusanyika katika mji huu dhidi ya mwanao mtakatifu Yesu uliyemtia mafuta.
RotÄe se, uistinu, u ovome gradu na svetog Slugu tvoga Isusa, kog pomaza, rotÄe se Herod i Poncije Pilat zajedno s narodima i pucima izraelskim
28 Wao wakafanya yale ambayo uweza wako na mapenzi yako yalikuwa yamekusudia yatokee tangu zamani.
da učine što tvoja ruka i tvoja volja predodredi da se zbude.
29 Sasa, Bwana angalia vitisho vyao na utuwezeshe sisi watumishi wako kulinena neno lako kwa ujasiri mkuu.
I evo sada, Gospodine, promotri prijetnje njihove i daj slugama svojim sa svom smjelošću navješćivati riječ tvoju!
30 Nyoosha mkono wako ili kuponya wagonjwa na kutenda ishara na miujiza kwa jina la Mwanao mtakatifu Yesu.”
Pruži ruku svoju da bude ozdravljenja, znamenja i čudesa po imenu svetoga Sluge tvoga Isusa.”
31 Walipokwisha kuomba, mahali walipokuwa wamekutanika pakatikiswa, wote wakajazwa na Roho Mtakatifu, wakanena neno la Mungu kwa ujasiri.
I pošto se pomoliše, potrese se mjesto gdje bijahu sabrani, i svi se napuniše Duha Svetoga te stanu navješćivati riječ Božju smjelo.
32 Wale walioamini wote walikuwa na moyo mmoja na nia moja. Wala hakuna hata mmoja aliyesema chochote alichokuwa nacho ni mali yake mwenyewe, lakini walishirikiana kila kitu walichokuwa nacho.
U mnoštva onih što prigrliše vjeru bijaše jedno srce i jedna duša. I nijedan od njih nije svojim zvao ništa od onoga što je imao, nego im sve bijaše zajedničko.
33 Mitume wakatoa ushuhuda wa kufufuka kwa Bwana Yesu kwa nguvu nyingi na neema ya Mungu ilikuwa juu yao wote.
Apostoli pak velikom silom davahu svjedočanstvo o uskrsnuću Gospodina Isusa i svi uživahu veliku naklonost.
34 Wala hapakuwepo mtu yeyote miongoni mwao aliyekuwa mhitaji, kwa sababu mara kwa mara wale waliokuwa na mashamba na nyumba waliviuza, wakaleta thamani ya vitu vilivyouzwa,
Doista, nitko među njima nije oskudijevao jer koji bi god posjedovali zemljišta ili kuće, prodavali bi ih i utržak donosili
35 wakaiweka miguuni pa mitume, kila mtu akagawiwa kadiri ya mahitaji yake.
i stavljali pred noge apostolima. A dijelilo se svakomu koliko je trebao.
36 Yosefu, Mlawi kutoka Kipro, ambaye mitume walimwita Barnaba (maana yake Mwana wa Faraja),
A Josip, od apostola prozvan Barnaba, što znači Sin utjehe, levit, rodom Cipranin,
37 aliuza shamba alilokuwa nalo, akaleta hizo fedha alizopata na kuziweka miguuni pa mitume.
posjedovaše jednu njivu; proda je pa donese novac i postavi pred noge apostolima.