< Matendo 3 >
1 Siku moja Petro na Yohana walikuwa wanapanda kwenda Hekaluni kusali yapata saa tisa alasiri.
Now Peter and John were going up to the temple together at the hour of prayer, which is the ninth hour.
2 Basi palikuwa na mtu mmoja aliyekuwa kiwete tangu kuzaliwa. Alichukuliwa na kuwekwa kwenye lango la Hekalu liitwalo Zuri, kila siku ili aombe msaada kwa watu wanaoingia Hekaluni.
And a certain man who had been lame from his birth was carried along; whom they laid every day at the gate of the temple, which is called Beautiful, to ask alms of those that were going into the temple:
3 Huyu mtu alipowaona Petro na Yohana wakikaribia kuingia Hekaluni, akawaomba wampe sadaka.
who seeing Peter and John about to go into the temple, asked alms of them.
4 Wakamkazia macho, kisha Petro akamwambia, “Tutazame sisi.”
But Peter, and John, looking earnestly at him said, Look on us.
5 Hivyo yule mtu akawatazama, akitazamia kupata kitu kutoka kwao.
And he fixed his eyes upon them, expecting to receive something from them.
6 Ndipo Petro akamwambia, “Sina fedha wala dhahabu, lakini nilicho nacho ndicho nikupacho. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, tembea!”
But Peter said, Silver and gold I have not; but what I have I give thee: In the name of Jesus Christ of Nazareth, rise up and walk.
7 Petro akamshika yule mtu kwa mkono wa kuume akamwinua, mara nyayo zake na vifundo vya miguu yake vikapata nguvu.
And taking him by the right hand, he raised him up: and immediately his feet and ancles were strengthened:
8 Akaruka juu na kusimama, akaanza kutembea. Kisha akaingia Hekaluni pamoja na Petro na Yohana, huku akitembea na kurukaruka na kumsifu Mungu.
and leaping up he stood firm, and walked; and entered with them into the temple, walking, and leaping, and praising God.
9 Watu wote walipomwona akitembea na kumsifu Mungu,
And all the people saw him walking and praising God:
10 wakamtambua kuwa ni yule mtu aliyekuwa akiketi nje ya Hekalu penye lango liitwalo Zuri akiomba msaada, nao wakajawa na mshangao, wakastaajabu juu ya yale yaliyomtukia.
and knew that it was he who sat to ask for alms at the Beautiful gate of the temple: and they were filled with astonishment and extasy at what had befallen him.
11 Aliyeponywa alipokuwa akiambatana na Petro na Yohana, watu wote walishangaa mno, wakaja wakiwakimbilia pale ukumbi wa Solomoni.
And as the lame man that was healed had hold of Peter and John, all the people being astonished ran together to them to the porch called Solomon's porch.
12 Petro alipoona watu wamekusanyika akawaambia, “Enyi Waisraeli, kwa nini mnastaajabu kuhusu jambo hili? Mbona mnatukazia macho kwa mshangao kana kwamba ni kwa uwezo wetu au utakatifu wetu tumemfanya mtu huyu kutembea?
And Peter seeing this said to the people, Men of Israel, why marvel ye at this, or why look ye so earnestly on us, as if by our own power or piety we had made this man able to walk?
13 Mungu wa Abrahamu na Isaki na Yakobo, Mungu wa baba zetu amemtukuza Mwanawe Yesu, ambaye ninyi mlimtoa ahukumiwe kifo na mkamkana mbele ya Pilato, ingawa yeye alikuwa ameamua kumwachia aende zake.
The God of Abraham and of Isaac and of Jacob, the God of our fathers hath glorified his son Jesus, whom ye delivered up, and denied before Pilate, when he determined to release Him.
14 Ninyi mlimkataa huyo Mtakatifu na Mwenye Haki mkaomba mpewe yule muuaji.
But ye refused the holy and righteous One, and desired a murderer to be granted unto you:
15 Hivyo mkamuua aliye chanzo cha uzima, lakini Mungu akamfufua kutoka kwa wafu. Sisi tu mashahidi wa mambo haya.
and put to death the prince of life; whom God hath raised from the dead, of which we are witnesses.
16 Kwa imani katika jina la Yesu, huyu mtu mnayemwona na kumfahamu ametiwa nguvu. Ni kwa jina la Yesu na imani itokayo kwake ambayo imemponya kabisa huyu mtu, kama ninyi wote mnavyoona.
And through faith in his name, hath strengthened this man, whom ye see and know: his name, I say, and saith in Him, hath wrought this perfect cure before you all.
17 “Sasa ndugu zangu, najua ya kuwa ninyi mlitenda bila kujua, kama walivyofanya viongozi wenu.
And now, brethren, I know that ye did it through ignorance, as did also your rulers:
18 Lakini kwa njia hii Mungu alitimiza kile ambacho alikuwa ametabiri kwa vinywa vya manabii wake wote, kwamba Kristo atateswa.
but thus hath God accomplished those things which He had foretold by the mouth of all his prophets, that Christ should suffer.
19 Tubuni basi mkamgeukie Mungu, dhambi zenu zifutwe, ili zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwepo kwake Bwana,
Repent therefore and be converted, that your sins may be blotted out: that seasons of refreshing may come upon you from the presence of the Lord;
20 naye apate kumtuma Kristo, ambaye ameteuliwa kwa ajili yenu, yaani Yesu.
and He may send Jesus Christ, who was before preached unto you:
21 Ilimpasa mbingu zimpokee mpaka wakati wa kufanywa upya kila kitu, kama Mungu alivyoahidi zamani kupitia kwa vinywa vya manabii wake watakatifu. (aiōn )
whom heaven must indeed receive till the times of settling all things, of which God hath spoken by the mouth of all his holy prophets from the beginning. (aiōn )
22 Kwa maana Mose alisema, ‘Bwana Mungu wenu atawainulia nabii kama mimi kutoka miongoni mwa ndugu zenu. Itawapasa kumtii huyo kwa kila jambo atakalowaambia.
For Moses said unto the fathers, the Lord your God will raise up a prophet unto you, of your brethren, like me, Him shall ye hear in all things whatever He shall say unto you;
23 Mtu yeyote ambaye hatamsikiliza huyo nabii, atatupiliwa mbali kabisa na watu wake.’
and every soul, who will not hearken to that prophet, shall be destroyed from among the people: yea and all the prophets from Samuel,
24 “Naam, manabii wote tangu Samweli na waliokuja baada yake, wote walitabiri kuhusu siku hizi.
and those that followed, as many as have prophesied, have also foretold these days.
25 Ninyi ndio wana wa manabii na wa Agano ambalo Mungu alifanya na baba zenu, akimwambia Abrahamu, ‘Kupitia kwa uzao wako, watu wote wa ulimwengu watabarikiwa.’
Now ye are the children of the prophets, and of the covenant, which God made with our fathers, saying to Abraham, "And in thy seed shall all the families of the earth be blessed:"
26 Mungu alipomfufua Yesu Mwanawe, alimtuma kwenu kwanza, ili awabariki kwa kumgeuza kila mmoja wenu kutoka njia yake mbaya.”
and to you first God having raised up his son Jesus, sent Him to bless you; in your turning away every one of you from your iniquities.