< Matendo 3 >
1 Siku moja Petro na Yohana walikuwa wanapanda kwenda Hekaluni kusali yapata saa tisa alasiri.
(upon it *k*) Peter now and John were going up into the temple at the hour of prayer the ninth.
2 Basi palikuwa na mtu mmoja aliyekuwa kiwete tangu kuzaliwa. Alichukuliwa na kuwekwa kwenye lango la Hekalu liitwalo Zuri, kila siku ili aombe msaada kwa watu wanaoingia Hekaluni.
And a certain man lame from womb of mother of him being was being carried, whom they were placing every day at the gate of the temple which is being named Beautiful to ask for alms from those who were going into the temple.
3 Huyu mtu alipowaona Petro na Yohana wakikaribia kuingia Hekaluni, akawaomba wampe sadaka.
who having seen Peter and John being about to enter into the temple was asking alms to receive.
4 Wakamkazia macho, kisha Petro akamwambia, “Tutazame sisi.”
Having looked intently now Peter upon him with John he said; do look unto us.
5 Hivyo yule mtu akawatazama, akitazamia kupata kitu kutoka kwao.
And he was giving heed to them expecting something from them to receive.
6 Ndipo Petro akamwambia, “Sina fedha wala dhahabu, lakini nilicho nacho ndicho nikupacho. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, tembea!”
Said however Peter; Silver and gold none there is to me; what however I have, this to you I give. In the name of Jesus Christ of Nazareth (do rise up *N(k)O*) and do walk.
7 Petro akamshika yule mtu kwa mkono wa kuume akamwinua, mara nyayo zake na vifundo vya miguu yake vikapata nguvu.
And having taken him by the right hand he raised up him. immediately then were strengthened the feet of him and the ankles,
8 Akaruka juu na kusimama, akaanza kutembea. Kisha akaingia Hekaluni pamoja na Petro na Yohana, huku akitembea na kurukaruka na kumsifu Mungu.
And leaping up he stood and was walking and he entered with them into the temple walking and leaping and praising God.
9 Watu wote walipomwona akitembea na kumsifu Mungu,
And saw all the people him walking and praising God.
10 wakamtambua kuwa ni yule mtu aliyekuwa akiketi nje ya Hekalu penye lango liitwalo Zuri akiomba msaada, nao wakajawa na mshangao, wakastaajabu juu ya yale yaliyomtukia.
They were recognizing (then *N(k)O*) him that (he himself *N(k)O*) was the [one] for the alms sitting at the Beautiful Gate of the temple, and they were filled with wonder and amazement at that having happened to him.
11 Aliyeponywa alipokuwa akiambatana na Petro na Yohana, watu wote walishangaa mno, wakaja wakiwakimbilia pale ukumbi wa Solomoni.
When is clinging now (he *N(k)O*) (having been healed lame [one] *K*) to Peter and (*no*) John ran together all the people to them in the porch which is being called Solomon’s greatly amazed.
12 Petro alipoona watu wamekusanyika akawaambia, “Enyi Waisraeli, kwa nini mnastaajabu kuhusu jambo hili? Mbona mnatukazia macho kwa mshangao kana kwamba ni kwa uwezo wetu au utakatifu wetu tumemfanya mtu huyu kutembea?
Having seen [it] however (*no*) Peter answered to the people: Men Israelites, why wonder you at this? Or on us why you look intently as if by [our] own power or godliness having made to walk him?
13 Mungu wa Abrahamu na Isaki na Yakobo, Mungu wa baba zetu amemtukuza Mwanawe Yesu, ambaye ninyi mlimtoa ahukumiwe kifo na mkamkana mbele ya Pilato, ingawa yeye alikuwa ameamua kumwachia aende zake.
The God of Abraham and (the God *n*) of Isaac and (the God *n*) of Jacob, the God of the fathers of us, has glorified the servant of Him Jesus whom you yourselves (indeed *no*) delivered up and disowned (him *ko*) in [the] presence of Pilate having adjudged that one to release;
14 Ninyi mlimkataa huyo Mtakatifu na Mwenye Haki mkaomba mpewe yule muuaji.
You yourselves however the Holy and Righteous One denied and requested a man a murderer to be granted to you,
15 Hivyo mkamuua aliye chanzo cha uzima, lakini Mungu akamfufua kutoka kwa wafu. Sisi tu mashahidi wa mambo haya.
and the Author of life you killed whom God has raised up out from [the] dead, whereof we ourselves witnesses are.
16 Kwa imani katika jina la Yesu, huyu mtu mnayemwona na kumfahamu ametiwa nguvu. Ni kwa jina la Yesu na imani itokayo kwake ambayo imemponya kabisa huyu mtu, kama ninyi wote mnavyoona.
And on the faith in the name of Him this [man] whom you see and know has strengthened the name of Him and the faith which [is] through Him has given to him complete soundness this before all of you.
17 “Sasa ndugu zangu, najua ya kuwa ninyi mlitenda bila kujua, kama walivyofanya viongozi wenu.
And now, brothers, I know that in ignorance you acted, as also the rulers of you;
18 Lakini kwa njia hii Mungu alitimiza kile ambacho alikuwa ametabiri kwa vinywa vya manabii wake wote, kwamba Kristo atateswa.
But God who foretold through [the] mouth of all the prophets [the] suffering [of] the Christ of Him He has fulfilled thus.
19 Tubuni basi mkamgeukie Mungu, dhambi zenu zifutwe, ili zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwepo kwake Bwana,
do repent therefore and do turn again (for *NK(o)*) the blotting out of your sins, so that maybe may come times of refreshing from [the] presence of the Lord
20 naye apate kumtuma Kristo, ambaye ameteuliwa kwa ajili yenu, yaani Yesu.
and [that] He may send the [One] (appointed *N(K)O*) to you Christ Jesus
21 Ilimpasa mbingu zimpokee mpaka wakati wa kufanywa upya kila kitu, kama Mungu alivyoahidi zamani kupitia kwa vinywa vya manabii wake watakatifu. (aiōn )
whom it behooves heaven indeed to receive until [the] times of restoration of all things of which spoke God through [the] mouth (of all *K*) the holy from [the] age of Him prophets. (aiōn )
22 Kwa maana Mose alisema, ‘Bwana Mungu wenu atawainulia nabii kama mimi kutoka miongoni mwa ndugu zenu. Itawapasa kumtii huyo kwa kila jambo atakalowaambia.
Moses indeed (for to the fathers *K*) said that A prophet to you will raise up [the] Lord the God (of you *NK(o)*) out from the brothers of you like me myself; to Him You will listen in all things as much as maybe He may say to you.
23 Mtu yeyote ambaye hatamsikiliza huyo nabii, atatupiliwa mbali kabisa na watu wake.’
It will be [that] now every soul who (only *N(k)O*) unless shall heed the prophet that will be utterly destroyed out from the people.’
24 “Naam, manabii wote tangu Samweli na waliokuja baada yake, wote walitabiri kuhusu siku hizi.
And all now the prophets from Samuel and those subsequently as many as spoke also (told of *N(K)O*) days these,
25 Ninyi ndio wana wa manabii na wa Agano ambalo Mungu alifanya na baba zenu, akimwambia Abrahamu, ‘Kupitia kwa uzao wako, watu wote wa ulimwengu watabarikiwa.’
You yourselves are (the *no*) sons of the prophets and of the covenant that made God with the fathers (of you *N(K)O*) saying to Abraham; And in the seed of you (will be blessed *NK(o)*) all the families of the earth.’
26 Mungu alipomfufua Yesu Mwanawe, alimtuma kwenu kwanza, ili awabariki kwa kumgeuza kila mmoja wenu kutoka njia yake mbaya.”
To you first having raised up God the servant of Him (Jesus *k*) sent Him blessing you in turning away each from the wickednesses of you.