< Matendo 3 >

1 Siku moja Petro na Yohana walikuwa wanapanda kwenda Hekaluni kusali yapata saa tisa alasiri.
Now Peter and John were going up together into the temple at the hour (the ninth) of prayer.
2 Basi palikuwa na mtu mmoja aliyekuwa kiwete tangu kuzaliwa. Alichukuliwa na kuwekwa kwenye lango la Hekalu liitwalo Zuri, kila siku ili aombe msaada kwa watu wanaoingia Hekaluni.
And a certain man, who had actually been lame from his mother's womb, was being carried (they would lay him daily at the temple gate, the one called Beautiful, to ask alms from those who entered the temple),
3 Huyu mtu alipowaona Petro na Yohana wakikaribia kuingia Hekaluni, akawaomba wampe sadaka.
who, upon seeing Peter and John about to go into the temple, began asking for alms.
4 Wakamkazia macho, kisha Petro akamwambia, “Tutazame sisi.”
So Peter, with John, fastening his gaze on him said, “Look at us.”
5 Hivyo yule mtu akawatazama, akitazamia kupata kitu kutoka kwao.
So he gave them his attention, expecting to receive something from them.
6 Ndipo Petro akamwambia, “Sina fedha wala dhahabu, lakini nilicho nacho ndicho nikupacho. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, tembea!”
But Peter said: “I do not have silver and gold, but what I do have I give you. In the name of Jesus Christ the Natsorean, get up and walk!”
7 Petro akamshika yule mtu kwa mkono wa kuume akamwinua, mara nyayo zake na vifundo vya miguu yake vikapata nguvu.
And grasping him by his right hand he lifted him up; immediately his feet and ankles were strengthened.
8 Akaruka juu na kusimama, akaanza kutembea. Kisha akaingia Hekaluni pamoja na Petro na Yohana, huku akitembea na kurukaruka na kumsifu Mungu.
So jumping up he stood, and began to walk! And he entered the temple with them, walking and leaping and praising God.
9 Watu wote walipomwona akitembea na kumsifu Mungu,
Well all the people saw him walking and praising God;
10 wakamtambua kuwa ni yule mtu aliyekuwa akiketi nje ya Hekalu penye lango liitwalo Zuri akiomba msaada, nao wakajawa na mshangao, wakastaajabu juu ya yale yaliyomtukia.
and they recognized him—that he was the one who used to sit at the Beautiful Gate of the temple, with a view to alms—and they were filled with wonder and amazement because of what had happened to him.
11 Aliyeponywa alipokuwa akiambatana na Petro na Yohana, watu wote walishangaa mno, wakaja wakiwakimbilia pale ukumbi wa Solomoni.
Now as the lame man who had been healed held on to Peter and John, all the people ran together to them in the portico, the one called ‘Solomon's’, really wondering.
12 Petro alipoona watu wamekusanyika akawaambia, “Enyi Waisraeli, kwa nini mnastaajabu kuhusu jambo hili? Mbona mnatukazia macho kwa mshangao kana kwamba ni kwa uwezo wetu au utakatifu wetu tumemfanya mtu huyu kutembea?
So upon observing this Peter responded to the people: “Men of Israel, why are you marveling at this, or why are you staring at us as if we have made him walk by our own power or godliness?
13 Mungu wa Abrahamu na Isaki na Yakobo, Mungu wa baba zetu amemtukuza Mwanawe Yesu, ambaye ninyi mlimtoa ahukumiwe kifo na mkamkana mbele ya Pilato, ingawa yeye alikuwa ameamua kumwachia aende zake.
The God of Abraham and Isaac and Jacob, the God of our fathers, glorified His Servant Jesus, whom you delivered up; and you repudiated Him to Pilate's face, when he was intending to release Him.
14 Ninyi mlimkataa huyo Mtakatifu na Mwenye Haki mkaomba mpewe yule muuaji.
Yes you repudiated the holy and righteous One, and you asked that a murderer be granted to you,
15 Hivyo mkamuua aliye chanzo cha uzima, lakini Mungu akamfufua kutoka kwa wafu. Sisi tu mashahidi wa mambo haya.
while you killed the Originator of the Life, whom God raised from among the dead, to which we are witnesses.
16 Kwa imani katika jina la Yesu, huyu mtu mnayemwona na kumfahamu ametiwa nguvu. Ni kwa jina la Yesu na imani itokayo kwake ambayo imemponya kabisa huyu mtu, kama ninyi wote mnavyoona.
Well His name, based on faith in His name, made this man strong, whom you see and know. Yes, the faith that is through Him has given him this wholeness in the presence of you all.
17 “Sasa ndugu zangu, najua ya kuwa ninyi mlitenda bila kujua, kama walivyofanya viongozi wenu.
“So now, brothers, I know that you did it in ignorance, as also your rulers.
18 Lakini kwa njia hii Mungu alitimiza kile ambacho alikuwa ametabiri kwa vinywa vya manabii wake wote, kwamba Kristo atateswa.
But the things that God foretold through the mouth of all His prophets, that the Messiah would suffer, He has thus fulfilled.
19 Tubuni basi mkamgeukie Mungu, dhambi zenu zifutwe, ili zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwepo kwake Bwana,
Repent therefore, and turn around, so that your sins may be erased, in order that times of refreshing may come from the Lord's face
20 naye apate kumtuma Kristo, ambaye ameteuliwa kwa ajili yenu, yaani Yesu.
and that He may send Jesus, who had been ordained to be your Messiah,
21 Ilimpasa mbingu zimpokee mpaka wakati wa kufanywa upya kila kitu, kama Mungu alivyoahidi zamani kupitia kwa vinywa vya manabii wake watakatifu. (aiōn g165)
whom Heaven must receive until the times of restoration of all things, of which times God spoke long ago by the mouth of all His holy prophets. (aiōn g165)
22 Kwa maana Mose alisema, ‘Bwana Mungu wenu atawainulia nabii kama mimi kutoka miongoni mwa ndugu zenu. Itawapasa kumtii huyo kwa kila jambo atakalowaambia.
“For example, Moses said to the fathers: ‘The Lord our God will raise up for you a Prophet, like me, from among your brothers. You must listen to Him, in all that He may say to you.
23 Mtu yeyote ambaye hatamsikiliza huyo nabii, atatupiliwa mbali kabisa na watu wake.’
It will be that every person who will not listen to that Prophet will be extirpated from among the people.’
24 “Naam, manabii wote tangu Samweli na waliokuja baada yake, wote walitabiri kuhusu siku hizi.
“Yes and all the prophets, from Samuel on down, as many as have spoken, have also foretold these days.
25 Ninyi ndio wana wa manabii na wa Agano ambalo Mungu alifanya na baba zenu, akimwambia Abrahamu, ‘Kupitia kwa uzao wako, watu wote wa ulimwengu watabarikiwa.’
You are sons of the prophets, and of the covenant which God made with our fathers, saying to Abraham, ‘Yes, in your seed all the families of the earth will be blessed.’
26 Mungu alipomfufua Yesu Mwanawe, alimtuma kwenu kwanza, ili awabariki kwa kumgeuza kila mmoja wenu kutoka njia yake mbaya.”
God, having raised up His Servant Jesus, sent Him to you first, to bless you by turning each of you away from your iniquities.”

< Matendo 3 >